DAAAAAAAH๐๐1
"1~5"
@topfans
Nilikuwa zangu kituo cha daladala nasubiria usafiri..
mbele yangu alikuwepo jamaa mmoja ni kama kuna mtu alikuwa akimsubiri pale kituoni..
Basi katika hali isiyo ya kawaida alikuja mwanaume mmoja nahisi ni konda
Alikuwa na kopo la maji ya kunywa mkononi alipokaribia sehemu aliposimama yule mkaka smart
konda alimtupia kopo mgongoni kisha akawahi kwenye gari na kuondoka
Yule kaka baada ya kupondwa na kopo aligeuka akiwa amekunja sura
Niliogopa nikamwambia siyo mimi wakati namnyoshea mkono kumwambia kuwa ni konda ndo alompiga
Yule kaka aliushika ule mkono akanivuta pembeni kidogo ambapo hakuna watu wengi..
Aliniuliza kwa sauti ya ukali ujinga gani huu umefanya??
Samahani siyo mimi..
Ni wewe๐ก๐ก
No siyo mimi ni konda
Hivi unathubutu kuongea uongo mbele yangu?? Unajiuza siyo??
Kwa taarifa yako mimi sinunuagi malaya na...tafadhali hebu acha upumbavu nani malaya??
Nikutake wewe kwa kipi?? Nakwambia siyo mimi nilokuponda na kopo unanilazimisha hivi unajikuta nani??
Oh unataka kujua mimi ni nani sasa subiri nitakuonyesha mimi ni nani..
Usinitishe bwana hebu peleka ujinga wako huko yani wanaume weupe mna tabia za kike mnafikiri kila mwanamke anawataka mxiiuu
Kauli yangu ilizidi kumpandisha hasira alitaka kuninasa kibao nikainama kibao kikanikosa
Yule mkaka alitoa simu mfukoni kwa hasira akapiga police wakati nashangaa shangaa mara nikashangaa difenda hilo
Ile nataka kukimbia nikazingirwa๐ฅบ๐ฅบile nataka kujielezea nikawekwa chini ya ulinzi mungu wangu
Hivi huyu kaka ana akili kweli??
Sasa unaniitia police mimi nimekufanyia nini??
Msikilizeni alivo na mdomo mchafu hakikisheni mnamshikisha adabu..
Alitoa kauli hiyo na kisha akaondoka nilipigwa pingu nikapakiwa kwenye difenda msobemsobe mpaka kituo cha police..
Niliwekwa lokapu hakuna cha maelezo wala nini nililala kituoni siku tatu bila kuruhusiwa kutoa taarifa nyumbani..
Siku ya nne alikuja Yule jamaa nilivomuona tu nikaanza kusonya na kubinua midomo
Mbwa zingine sijui huwa zinajikuta nani kuna mbwa ninazichukia mimi
Niliongea hivo jamaa akanisikia alitaka kuninasa kibao akaishia kupiga kwenye nondo nilianza kucheka na kumwambia umepata kiboko yako..
Alizidi kupandwa na hasira police mmoja aliekuwa karibu alimtuliza kisha akanifokea na kunitaka nifunge domo langu..
Yule mkaka alimwambia police hakikisha huyu mshenzi hatolewi mpaka awe na adabu..
Aliongea hivo kisha akaanza kuondoka..
Police alimzuia kwa kumuita mkuu lakini sasa huyu binti mpaka sasa hivi hajafunguliwa kesi yoyote
Huenda familia yake inamtafuta..Yule mkaka aliwaza kisha akaamuru nifunguliwe kesi..
Ni kesi ya nini??
Itaendeleaaaaaa
Full 1000
DAAAAAAAH๐๐2
By Babie LOve
Jamani wewe kaka hivi umechanganyikiwa??
Unanifungulia mimi kesi ya nini?.
Si nilikwambia siyo mimi nilokuponda na kopo inamaana hukunielewa??
Okay fine fungua kesi yoyote unayoitaka hata ya mauaji nipatie na uhakikishe ninafia gerezani ili roho yako isuuzike..
Alifyonza kisha akasepa hivi linajikuta nani hili??
Muda huohuo nilitolewa lokapu nikaenda kufunguliwa kesi et ya udhalilishaji jamani..
Kwetu walipewa taarifa wakawa wamefika kituo cha police
walipewa taarifa za kesi yangu na wakaambiwa kesi haiihitaji dhamana..
Wazazi wangu walichanganyikiwa baada ya kunyimwa kuniwekea dhamana..
Ikabidi waanze kumtafuta jamaa aloniweka lokapu..walipeleleza mpaka wakajua sehemu anapokaa
Baba na mama walikwenda mpaka nyumbani kwa huyo mkaka kwa lengo la kwenda kuongea nae..
Huyo kaka alikubali niwekewe dhamana kwa sharti moja tu
Nikubali kumuomba msamaha๐ฅบ๐ฅบniliwaambia wazazi wangu waache niendelee kukaa mahabusu
Sikuwa tyr kuomba msamaha kwa kosa ambalo sijalifanya..
Niliwahakikishia wazazi wangu siyo mimi nilompiga jamaa na kopo la maji..
Wazazi wangu wananiamini sana ila sasa ili nitoke kituo cha police ni lazima niombe msamaha na familia ya yule kijana niliambiwa ni familia yenye nguvu sana
Baba aliniambia siwezi kuachiliwa bila kuomba msamaha..
Niliwaza nikasema okay acha tu nijishushe niombe msamaha ili nitolewe police..
Basi nilitolewa pale kituoni nikapelekwa nyumbani kwa huyo mkaka niende nikaombe msamaha..
Nilienda na wazazi wangu tulikaribishwa nyumbani kwake yeye hakuwepo tuliwakuta wazazi wake..
Tulikaa sebleni baada ya lisaa limoja alifika mlengwa alikuja akaa kwenye kochi akaandika 4 akawa anasubiri niinuke nikamuombe msamaha..
Nilishikwa na hasira lakini sa nitafanyaje
Nilisimama nikapiga hatua mpaka sehemu alipo nilipiga magoti nikamshika miguu nikamwambia sorry naomba unisamehe..
Alinyofoa simu yake mfukoni akapiga police na kuwaambia futeni hiyo kesi haraka..
Yani hasira zilinipanda lakini nikawa najizuia tu..
Kile kitendo cha mimi kumpigia magoti yule mkaka kiliwafurahisha sana wazazi wake..
Wakaanza kuwaambia wazazi wangu binti yenu ana heshima sana anaonekana ni binti alielelewa katika malezi yanayofaa..
Daaaaah๐๐คฃ
Itaendeleaaaaa
Full 1000
DAAAAAAAH๐๐3
By Babie LOve
Niliwaomba wazazi wangu tuondoke kama ni msamaha si tushaomba tunasubiri nini tena?.
Wazazi wa yule mkaka walituzuia walisema sisi ni wageni hatuwezi kuondoka bila kula chochote..
Kula tena๐ฅบ๐ฅบ na hizi hasira nilizonazo nile meza moja na hili limkaka??hapana siwezi..
Wazazi wangu walirudi kukaa yani ndo nikazidi kuchukia yani baba na mama inamaana wanakaa kusubiri chakula hapa??
Jamani mimi naombeni nitangulie nyumbani angalau nikaoge siwezi kula chochote mpaka nioge..
Mama wa yule mkaka aliniambia usijali mwanangu hivi unaitwa nani kwanza??
Naitwa Paris..
Wow jina zuri sanaโค๏ธsubiri nikuitie dada akupeleke bafuni ukaoge..
Yani mimi nioge hapa kwenye hii nyumba๐ฅบ hapana siwezi..
Dada aliitwa akaja akaambiwa anipeleke bafuni haraka nioge kisha aende chumbani kwa Baila anichukulie nguo ya kubadilisha..
Hapana mama nilijaribu kukataa lakini wazazi wangu wakaniambia kwa ishara nikubali..
Basi nilipelekwa bafuni nikaoga nikaletewa nguo nikabadili nikarudi sebleni ni kama vile nilikuwa nasubiriwa mimi tu
Nilivofika tu watu wote tukaombwa tuhamie dinning kwa ajili ya kuweza kupata chakula..
Basi ilibidi tu yani lakini sikupenda kula kwa yule mkaka..
Jina lake ni Bill nilisikia mama yake akimuita hivo na kumuomba aongoze sala ya kuombea chakula..
Aliomba kama mtu vile kumbe linyanyasaji kiukweli hata sikufumba macho wakati anaomba
Nilibaki namwangalia tu huku nikitamani nichukue uma nimtoboe nao ili nilipize kisasi cha yeye kuniweka lokapu kwa makosa ya mtu mwingine..
Tulikula nyumbani kwa Bill mimi hata sikushiba nilipakua kichakula kidogo kama cha mtoto mchanga..
Nilikula haraka haraka nikamaliza nikatulia kuwasubiria wazazi wangu wamalize tuondoke
Baba na mama walimaliza kula wakashukuru baada ya hapo wakaaga..
wazazi wa Bill walitusindikiza nje kwenye gari kabla hatujaondoka waliomba radhi kwa wazazi wangu
Waliomba tumsamehe Bill kwa sababu ni kijana mwema na hilo alilolifanya kunilaza mimi lokapu hata wao hawajalifurahia..
Baada ya wazazi wa Bill kuomba msamaha kidogo hasira zangu zilipungua..
Waliuliza kama tyr nimeshapata ajira wakaambiwa ndo niko nahangaika kutafuta kazi..
Basi wazazi wa Bill waliuliza kazi niloisomea nikawaambia..
Mama Bill alinipatia namba yake akaniambia nikifika nyumbani nimtumie cv zangu za kazi kwenye simu ili azipitie kisha atanipatia kazi ofisini kwake..
Mmhh nilisita lakini wazazi wakaniambia nichukue namba..
Niliwashangaa wazazi wangu๐ฅบhivi nitafanyaje kazi sehemu moja na mzazi wa adui yangu??
Itaendeleaaaaaa
Full 1000
DAAAAAAAH๐๐4
By Babie LOve
Tulifika nyumbani nikaelekea moja kwa moja chumbani kwangu nilikuwa na usingizi wa hela yote..
Nilijitupia kitandani bila hata kuvua viatu..
Muda mfupi mama alikuja chumbani kwangu akiwa na maziwa..
Alinikuta tyr nishalala lakini nilikuwa namsikia..alijisemea masikini mwanangu amejaa mapele ya mbu..
Siku tano nzima amesota na kuteseka kituoni๐mama alinung'unika badae alinifunika akaniacha nilale..
Baada ya mama kuondoka niliamka nikayanywa yale maziwa yote๐คฃnilikuwa na njaa kinoma
Kule kwa Bill sikushiba wala sikutaka kula chakula kwenye ile nyumba nilijilazimisha tu..
Nilimaliza maziwa nikalala siku iliyofuata mapema mama alikuja chumbani kwangu akiwa ameshajiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini..
Yeye ni nesi na baba yangu ni mwalimu wa secondary..
Mama alinijulia hali akaniambia akifika kazini kuna dawa atanitumia za kusafisha damu na kuondoa infection zote nilizozipata huko kituoni..
Sawa mama hata usijali mi niko salama๐ฅฐalinikumbatia kisha tukaagana..
Wakati anatoka alipofika mlangoni aliniuliza kuhusu kutuma cv
Nikamwambia wala sijatuma na siwezi kutuma mama..
Kwani bado una hasira na ile familia??
Ndio mama ninazo haswa kwa Bill namchukia sana siwezi kuwa karibu na mtu yeyote wa familia yake..
Mama aliitikia sawa lakini baba yako alisema nikukumbushe utume cv..
Mxiiuu mama mimi situmi.. haya sawa mimi naondoka..sawa mama kazi njema..
Baada ya mama kuondoka niliendelea kulala..nililala mpaka saa saba mchana nikaamka..
Nilioga kwanza baada ya hapo nilienda jikoni kutafuta chochote kitu nipashe utumbo..
Nilikula chakula nikamaliza nikarudi chumbani.. nilikuta kuna missed call kutoka kwa baba..
Ikabidi nimpigie hello baba..hello Paris unaendeleaje??
Naendelea vizuri baba sijui wewe..mimi sijambo mwanangu vipi umekumbuka kutuma cv kwa mama Bill??
No baba bado sijamtumia..
Kwanini mwanangu?? Hiyo ni bahati mungu kakuletea ya kupata kazi kirahisi ilitakiwa utume cv usiku uleule wa jana..
Lakini baba mimi sitaki kuajiriwa na mama Bill sitaki kuwa karibu na familia ya Bill..
Naelewa mwanangu lakini kufanya kazi ofisini kwa mtu siyo kuwa karibu nae wewe unaenda kufanya kazi utakuwa muajiriwa kama waajiriwa wengine...
Baba alinisihi sana nitume cv nikamwambia sawa alikata simu namimi nikaendelea kulala..
Nililala mpaka usiku waliporudi baba na mama waliniita ili kuniuliza majibu niliyopewa baada ya kutuma cv
Niliwaambia bado sijatuma baba alifoka aliamuru nitume muda uleule akiwa amenisimamia..
Daaaaaaaaah๐ช
Full 1000
DAAAAAAAH๐๐5
Sikuwa na ujanja ilibidi nifanye vile alivyohitaji baba..
Baada ya muda mfupi nilipokea simu kutoka kwa mama Bill alinitaarifu kuwa nijiandae na siku inayofuata nifike ofisini kwa ajili ya kuanza kazi..
Kwa wazazi wangu ilikuwa furaha lakini kwangu ilikuwa chukizo nilienda chumbani kwa hasira nikaanza kuandaa nguo za kuvaa kesho..
Hivi kwanini huyu mama amenipa kazi kiurahisi kiasi hiki?? Utafikili nilimuomba..
Nilianza kugomba peke yangu chumbani niliandaa kila kitu nikapanda kitandani nikalala sikutaka kula hata chakula..
Baba aliamuru niletewe chakula chumbani na nile kwa lazima maana kesho natakiwa kuamka na nguvu nikafanye kazi..
Nilikula hivohivo kwa lazima nikalala siku iliyofuata nilisindikizwa kazini na wazazi wangu..
Tuna gari moja tu hivo ilibidi nipelekwe mimi wa kwanza kisha mama na badae baba maana yeye ndo dereva..
Nilipokelewa kazini na mama Bill nimesomea mambo ya uhasibu na ndo kitengo nilichoajiriwa pale ofisini..
Ni kampuni ya mama Bill yeye ndie Boss pale hata hivo aliniambia mme wake pamoja na Bill wao wanafanya kazi katika kampuni nyingine kubwa zaidi ya ile..
Angalau nilipumua baada ya kusikia Bill hafanyi kazi pale๐ฅฐnilianza kazi na nilikuwa makini sana kazini..
Mama Bill aliniambia chochote kikinitatiza nifike ofisini kwake haraka kwa ajili ya kuomba usaidizi..
Basi alionekana mkarimu kwangu tofauti na toto lake sijui tabia zile limerithi kwa nani..
Nilifanya kazi mpaka jioni muda wa kutoka nikaondoka zangu ofisini..
Baba yangu alikuja kunichukua kwa ajili ya kunirudisha nyumbani๐ฅฐ wakati tuko njiani kurudi nyumbani nilikumbuka kwenye mkoba kuna nguo za Baila..
Zile nilizopewa nyumbani kwa kina Bill siku ile nivae nilikuja nazo ofisini ili nimpe mama Bill kwa bahati mbaya nikasahau..
Nilimwambia baba samahani naomba usimamishe gari..kuna nini Paris??
Kuna nguo za Baila nimesahau kumpatia mama Bill ngoja nimpigie kama bado yuko ofisini turudi nizipeleke..
Sawa..fanya hivo mwanangu..
Sawa baba..
Nilipiga simu kwa mama Bill alipokea na kuniita Paris mwanangu vipi kuna jambo ungependa kuniambia?.
Ndiyo mama..samahani lakini kuna mzigo nilikuja nao nikasahau kukupatia nilikuwa nauliza kama bado uko ofisini niulete hapo..
Hapana Paris mimi nimeshafika nyumbani kama hautojali pitia hapa nyumbani uniletee..
Mmhhh nyumbani si naeza nikakutana na adui yangu Bill๐ชbaba aliniambia wacha nigeuze gari tuelekee nyumbani kwa mama Bill..
Oh God nisaidie tu nisikutane na yule ibilisi wa mguu mmoja๐ช nilianza kufanya maombi kwenye gari..
Tulienda mpaka nyumbani kwa kina Bill tulikaribishwa ndani baba akaniambia niingie mimi nipeleke mzigo yeye ananisubiri nje kwenye gari..
Basi nilifunguliwa geit na mlinzi nikaelekea ndani.. nilifika nikabisha mlangoni akaja kufungua yule yule nisiempenda..
Bill Alishangaa baada ya kuniona pale akaniuliza unataka nin...
Samahani sijakufuata wewe nina shida na mama yako siyo wewe..nilimkatisha kabla hajamaliza kuongea..
Nilimpita na kutaka kuingia ndani lakini alinizuia kwa kunishika mkono..
Hivi unashida gani wewe nimeshakwambia hapa nimekuja nina shida na mama yako siyo wewe hebu achia mkono wangu..
Funga mdomo wako na ujaribu kuongea kwa adabu upo nyumbani kwangu aliongea Bill huku akinitizama kwa hasira..
Sijui likoje๐ชnilifikiri nimeongea taratibu kumbe niliropoka kwa sauti mpaka akanisikia..
Unasemaje๐ฅบ๐ฅบ??aliuliza huku akinisogelea kwa karibu zaidi..
Itaendeleaaaaa
Full 1000.