SITOSAHAU YALIYONIKUTA BAADA YA KUIBA NGUO YA NDANI😳 Sehemu... Saba. 👉 Amina upo tayari niteseke kweli mpenzi wangu...👇
" Sahadini napenda uwe mume wangu unaonaje ungenioa kwanza alafu ule tunga la halali.
( Nashangaa akanitoa kwenye kumbato alafu anapiga makofi uku anaruka ruka)
" Amina amina amina umeniambia jambo la maana sana acha nikaonge na wazazi wangu amina upo tayari kuwa na mimi kama mumeo.
" Ndio.
" Naenda narudi naenda kuongea na wazazi wangu.
( Sahadini alifungua mlango akaondoka...mimi tena nimelishika domo langu lililopoka ndoa...nawaza sasa...akiwa mume wangu ndoa itafungwaje je wazazi wangu niwaambie mume wangu ni jini mbona balaa hili ivi majini wanakula chakula tunachokula sisi binadamu wa kawaida...nawaza nawazua usingizi ukanipata nastukia asubuhi kazini nimechelewa tena...mala nagongewa hodi na wamama watu wazima wanakuja kuniambia)
" Amina kamuombe msamaha toboa tobo tunakuomba.
" Nikaombe msamaha wanini?
" Usiku yale majibu yako yatakuletea matatizo.
" Hapana mama zangu mimi siwezi kuomba msamaha kwenye ukweli yule mganga si mtu mzuri ivi chupi tu ukamfanye mtu awashwe yani mfano mtu kaianua kwa bahati mbaya ndio apate iyo azabu.
" Kweli amekosea ila yule roho yake mbaya anaweza kukupa kile alichosema utakuja kufa.
" Acha nife nikiwa nawatetea wengine.
( Wamama wakaondoka uku wananionea huruma mimi....Nikaingia ndani simu yangu inaita anapiga mama yangu mzazi nikapokea)
" Haloo mama.
" Mwanangu njoo nyumbani.
" Kuna nini?
" Njoo wewe mwenzio ninayo furaha hapa njoo chap.
( Nikaona makubwa aya kama ningekuwa kazini je ingekuwaje kwa mama sio mbali na ninapoishi gali shilingi 700 nafika anakaa chamazi magengeni...kweli nikaenda mama ananiambia)
" Mwanangu mtoto wa boss wa baba yako anataka kukuoa.
" Yeye kaniona wapi?
" Baba yako uyo kamuonyesha picha basi hapo hapo akasema mzee mwanao nataka nimuoe na baba yako ndio kaja kuniambia mimi nikwambie wewe mwanangu unaolewa kwenye utajili Hehehehe nicheke mie kuvaa kanga za kuunga unga basi kwisha kabisa.
" Mama mimi siwezi kuolewa na mtu simjui.
" Acha ujinga ngoja nimwambie baba yako aje na picha yake uyo mumeo.
( Mama kapiga simu kwa baba...maana baba yangu ni mlinzi...dk 30 baba kaja na uyo mtoto wa boss wake kweli ni matajili aliponiona akatabasamu alafu akasema mbele ya wazazi wangu)
" Mahari atayotaja amina naweka mala tatu yake aseme mahari yake shilingi ngapi uyu ni mwanamke ametimiza vigezo vya kuwa na mimi.
( Mimi namuwaza sahadini wangu...nawaza nishayatimba kwa mganga namtegemea sahadini alafu nimsaliti sahadini hapa nafanyaje nawaza mama anasema)
" Wewe amina mwenzio anasubili uonge umeduwaa uamini kama umepata bahati mwanangu.
( Nilikaa kimya tu nawaza mtoto wa tajili yule akaingia mfukoni akawapa wazazi wangu milioni mbili anawaambia)
" Hii nimewapa muonge na amina anikubari naisi anaye mtu labla anawaza atamuachaje nipo tayari kulipa ghalama zozote za uyo mtu wewe uwe wangu.
( Mama anapokea pesa uku anatetemeka ajawai sijui kushika milioni mbili...mtoto wa tajili kaondoka tumebaki wenyewe baba anauliza)
" Amina mahari yako shilingi ngapi?
( Mama akadakia)
" Sema milioni kumi yeye akitoa mala mbili yake yani milioni 30 mtaa wote huu chamazi akuna aliyeolewa pesa iyo.
( Mimi nipo kimya mawazo kichwani yanagongana tu mama akanitikisa)
" Amina sema acha kunyamaza.
( Hapa sasa nasema nini ndio nawaza)
Dah yani..
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni