MIMBA YA BESTMAN❤️*
*SEHEMU YA 06
___________________________________
SEHEMU YA 06
Mulky akiwa amezubaa wenzake wakiendelea kuongea na hakuwa anasikia chochote maana akili yake ilikuwa inawaza mbali sana.
Hamida aligundua hilo alimuita
" Mulky, mulky.....
Mulky hakusikia mpaka yule muhudumu aliekuwa akimhudumia aliposhika begani na kumwambia.
" Mulky unaitwa na Hamida.
Mulky alimuangalia Hamida.
" Vipi upo sawa kweli?
" Ndio nipo sawa ulikuwa unasemaje?
" Basi tutaongea badae.
Wakiendelea kupatiwa huduma walipomaliza waliondoka pamoja mulky aliwapa lifti wakaanza kumpeleka mwajuma nyumbani kwake.
Kwenye gari walibaki wawili Hamida na mulky.
Hamida alimuangalia akahisi kuna jambo haliko sawa kwa Mulky na hataki kusema.
" Mulky kuna jambo unanificha?
" Hapana Hamida"
" Kuwa muwazi tafadhali. Au una matatizo kwenye ndoa yako?
" Hamida sijui nianzie wapi kukueleza ....
" Anza popote.
"hebu nipe muda kwanza.
" Kwahiyo unataka kufa na siri so ndio? Na tangia lini tukafichana kwenye mambo yetu unakumbuka siri zangu nyingi na nzito nimekuwa nikikushirikisha vipi wewe unifiche mambo yako?
Mulky alitafuta sehemu akaenda kusimamisha gari kwanza alafu alimgeukia Hamida wakawa wanaangaliana.
" Niambie sasa.
" Hamida nina jambo linaumiza sana kichwa changu na sijui mitatatua vipi shida hii.
" Ndio uniambie tushauriane.
" Hivi una jua tangia nime......
Kabla mulky hajamaliza kuongea alisikia mtu anagonga kwenye kioo cha dirisha la gari yake akageuka kumuangalia na kufungua kioo , alipomuangalia vizuri yule mtu aliachia tabasamu.
" Waoooo Sameer umekuja lini?
" Nina siku mbili tangia nimekuja.
" Mbona Yasini hajaniambia kuwa umerudi?
" Hata nae hana taarifa kama nimerudi nataka kumfanyia surprise na hapa nilipo nilikuwa naelekea nyumbani kwenu.
" Basi sawa acha tuongozane pamoja.
" Kama una mambo yako fanya kwanza.
" Sina cha muhimu .....
" Lakini upo na mwenzio.
" Usijali kuhusu mimi hata hivyo nimefika nilikuwa nasikia hapa. Alisema Hamida na mulky akamuangalia
" Usijali shoga yangu nenda kamuandalia mgeni wako.
" Lakini mimi sio mgeni ni mwenyeji sana. Alisema Sameer .
" Kweli Sameer sio mgeni kwani umesahau?
" Sio kumsahau nahisi simjui kabisa.
" Jamani Hamida huyu si ndio yule bestman wa Yasini aliyesimamia kwenye harusi yangu.
Rafiki kipenzi wa Yasini .
" Hapo nimeshaanza kupata picha , lakini kabadilika .
" Nimekuwa mzee sindio?
Sameer aliongea kama utani.
" Hapana unazidi kuwa handsome.
" Hahahaha masihara hayo.
Baada ya kutambulisha na na kupiga story mbili tatu Sameer alienda kupanda kwenye gari yake na mulky aliachana na Hamida.
" Hamida nikipata muda nitakuja kwako tuongee.
" Sawa fanya hivyo kipenzi.
" Sawa.
Hamida alifungua mlango wa gari akashuka Mulki akapelekwa nyumbani kwake.
Mulky alielekea nyumbani kwake huku wakiwa anafuata gari ya Sameer kwa nyuma hivyo walifika nyumbani pamoja.
" Karibu sana Sameer.
" Asante .
Waliingia ndani huku Sameer akiwa anaangalia mazingira.
" Naona ndoa tamu sana.
Mulky alimuangalia Sameer alafu akacheka kidogo.
" Kwanini unasema hivyo?
" Naona jinsi ulivyonawiri mtoto wa kike.
" Acha utani bwana mbona nipo kawaida.
" Huo ni mtazamo wako lakini kwa upande wangu umependeza jamaa yangu kaweza majukumu yake kama mume.
" Tuachane na hayo niambie unakunywa kinywaji gani?
" Nichaguliwe chochote kilichopo.
" Kuna juice ya mabasi, embe na passion. Pia kuna soda.
" Unajua mimi sio mpenzi wa soda niletee juice.
" Sawa nipe dakika chache.
" Sawa.
Mulky alienda kuchukua juice akamtengea mgeni wake nae akakaa wakawa wanaongea mawili matatu.
Baada ya muda Yasini alirudi kutoka kwenye mihangaiko yake alifurahi kumuona Sameer walikumbatiana na kujuliana hali kwa furaha.
" Mbona umekuja bila kunipa taarifa?
" Nilikuwa nataka kukifanyia surprise.
" Surprise gani? Sijapenda.
" Basi yaishe .
Walienda kukaa wakaendelea na story zao huku mulky akiwaacha na kwenda jikoni kuandaa chakula.
Mara kwa mara Sameer alikuwa akienda nyumbani kwa Yasini walikaa na Mulky wakawa wanapita story mara nyingine walikuwa wanacheza game pamoja hiyo ilikuwa nafuu sana kwa Mulky hakuwa na mawazo sana alifurahia sana uwepo wa Sameer.
Kuna siku wazazi wa Yasini walienda kuwatembelea nyumbani kwao . Shangazi yake Yasini alimuuliza Yasini.
" Yasini mbona unachelewesha mambo nilijua nikija nitakuta hali ipo tofauti.
" Unamaanisha nini shangazi?
" Wifi hebu achana na hayo.
Alisema mama Yasini huku akiwa anamuangalia mulky .
Wakati huo mulky alikosa furaha ghafla.
" Wifi hawa watoto ukisema iwaache hivi utakuta bila kuona mjukuu vijana wa siku hizi hawajali kuhusu familia utandawazi unawamaliza vijana wetu.
Yasini alimuangalia shangazi yake kwa jicho kali kisha akamuangalia Mulky ambae alikuwa kajiinamia .
" Shangazi haya ni maswala yangu na familia yangu nisingependa mtu mwingine aingilie na swala la kupata watoto ni mipango wangu na mke wangu.
" Wifi ona Yasini anavyojibu wakati namtetea yeye mwenyewe.
" Kila jambo na wakati wake wifi sisi ni binadamu hatuwezi kumpangia Mungu.
Yasini hakutaka kuendelea kusikiliza marumbano yao alienda kumchukua mke wake wakaenda ndani.
" Ona sasa wanaondoka na kutuacha hapa hiyo ni heshima ya wapi? Alafu huyu Yasini huyu tangia ameowa amekuwa na dharau flani hivi.
" Umeyataka wifi unafikiri yule mtoto wa watu anajisikiaje na ndio kwanza siku ya kwanza umekuja na maneno ya akitoka hivyo? Na mwanangu hana tabia hiyo usimtoe mdomoni kwa mabaya.
" Kwahiyo wifi wewe imeridhika na hili huna mjukuu au hautaki kulea wajukuu mwenzetu?
" Kama imepangwa miles nitakuwa tu tunatakiwa kuwa na Subra.
Yasini na Mulky walienda chumbani kwao , Yasini alimkalisha mke wake kitandani nae akakaa pembeni.
Full 1000
whatsp 0784468229.