Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

*MIMBA YA BESTMAN❤️* *SEHEMU YA 11~12

7th Jun, 2025 Views 3

*MIMBA YA BESTMAN❤️*
*SEHEMU YA 11~12*
___________________________________

SEHEMU YA 11
" Unajua siwezi kuvumilia zaidi naomba kesho tuonane hotelini.
" Siwezi kuja huko.
" Kama huwezi kuja basi nitakufuata nyumbani kwako mume wako atakapokuwa kazini.
Alisema Sameer alafu akaenda kwenye friji akachukua chupa ya maji ya kunywa .
" Nipatie korosho mume wako anataka.
" Nenda nitamletea.
Sameer alirudi sebleni na muda huo huo Mulky alipeleka korosho sebleni.

Ilipofika usiku Mulky akiwa kapumzika na mume wake wakifurahia ndoa yao simu ya mulky ilikuwa inaingiza sana messege na Mulky aliopoteza.
" Ni nani huyo anatuma messege kama anakudai?
" Sijui ni nani. Alijibu mulky huku akinyanyuka kitandani kuangalia simu yake.
Alikuta messege kama tano zilitumwa na namba mpya lakini kutokana na maelezo yaliyoandikwa aligundua kuwa ni Sameer alifuta haraka zile messege alafu akazima simu na kurudi kulala , alijikaza kifuani kwa Yasini wakati huo Yasini alikuwa akimuangalia.
" Niambie mume wangu...
" Mmm ni nani amekutuma ujumbe karibia sita kama si kumi?
" Ni kikundi chetu cha wanawake leo alikwenda ndio nilikuwa baoewa taarifa ya walichojadili huko.
" Ndio iwe muda huku kwani hawajui huu muda upo na mumeo?
Mulky alitabasamu
" Watakuja mume wangu alafu naona kama vile una kawivu flani.
" Sio kawivu nina wivu haswaa.
" Lakini sio wanaume ni wanawake wenzangu.
" Basi tupumzike ila waambie hao wenzio kuwa Mida kama hii wasipende kukusumbua kwani ndio muda wangu mzuri wa kupumzika na wewe mke wangu.
" Sawa mume.

Kesho yake asubuhi baada ya mulky kumuandaa mume wake alimbeba pc yake akasindikiwa mpaka kwenye gari waliagana Yasini akapanda kwenye gari akaelekea kazini .
Mulky alirudi ndani akachukua simu yake na kumtafuta Sameer.
" Hallow asali wangu.
" Mmmmh.....
" Mbona unavuna kwani sio kweli?
" Sameer hivi una shida gani na ndoa yangu unataka niachie ndio uhisi amani si ndio?
" Tulia mtoto wa kike unajua hizi shida ndogo ndogo huwa unazotaka mwenyewe ungekuwa unakutana na mimi hata mara mbili kwa wiki basi ungenifanyia nitilize akili yangu ingekuwa sawa lakini wewe unanipuuzia tangia huyo mumeo apone matatizo yake umesahau kama mambo ni kusaidiana nilikutana wakati wa shida na mimi nifae kwa muda huu ambao nateseka kwaajili ya penzi lako .
Mulky akaona haitawezekana kuongea na Sameer kwenye simu akamtaka wakutane sehemu waongee waelewane.
Baada ya kukata simu mulky alienda chumbani kwake akajiandaa kwaajili ya kutoka , alipokuwa tayari alibeba funguo yake ya gari pamoja na pochi yake akatoka chumbani akaenda sebleni, akiwa anaelekea kwenye lango kuu la kutokea nje alisikia geti linafunguliwa na Yasini aliingiza gari .
" Kheeee huyu vipi mbona ametoka hapa sio muda mrefu, kasahau nini?
Mulky alijiuliza maswali huku akiwa kasimama anamsubiri Yasini.
Yasini alipaki gari akashuka na kuelekea ndani alimkuta Mulky kasimama mlangoni.
" Ulikuwa unaenda wapi?
" Hamida kanipigia simu anaumwa nilikuwa naenda kumuangalia.
" Inamaana ulikuwa unaondoka bila kuomba ruhusa kwa mume wako?
" Ilikuwa nikupigie simu nikuombe ruhusa.
"Sio kweli.
" Kweli mume wangu.
Alisema mulky huku akimsogelea Yasini na kumshika kidevu.
" Sawa sasa itakuwaje wakati mimi nimerudi hapa kwaajili yako?
Mulky alimuangalia mume wake alafu akauliza
" Unamaanisha nini unasema hivyo mume wangu?
Yasini alimuangalia Mulky kwa jicho la huba kisha akasema.
" Sikuwahi kujifurahisha kipindi tulipokuwa Fungate sasa nimeamua twende Fungate tukafurahie nikakupe kile ulichokuwa unastahili kupewa.
Mulky alijisikia raha sana kusikia maneno aliyoambiwa na mume wake kwani tangia Yasini awe sawa mahaba yalikuwa motomoto .
" Unanifanya nijisikie fahari sana nakupenda sana mume wangu na naomba unisamehe kwa yale yote niliyokukosea huko mwanzo.
" Haijawahi kunikosoa mke wangu zile zilikuwa changamoto tu. Sasa vipi utaenda kwa Hamida au tutaenda pamoja?
" Hamida hapana siwezi kukataa ofa kubwa na nzuri kama hiyo.
" Basi kajiandae tiketi za ndege zipo tayari.
" Sawa twende pamoja tafadhali.
Waliongozana pamoja huku wakiwa wameshikana mikono wakielekea chumbani kwao .kabla hawajafika chumbani simu ya mulky iliita aliekuwa anapiga alikuwa ni Sameer .
Mulky alipoona namba ya Sameer alimuangalia Yasini usoni.
" Mbona hupikei simu,nani anapiga?
" Hamida.
" Pokea. Alijibu Yasini huku akiwa kasimama akisubiri mulky apokee simu.

MIMBA YA BESTMAN 12

Mulky aliiangalia ile simu huku akiwa anajifikiria jinsi ya kupokea na wakati huo Yasini alikuwa akimsubiri apokee.
Mulky alijikaza akapokea.
" Hallow.
" Nimefika hotelini na kungoja......
Kabla Sameer hajamaliza kuongea mulky alimkatiza kwa kusema
" Shoga yangu sitaweza kuja kukuangalia nina safari na mume wangu nikirudi nitakuja kukuona wewe ugua pole.
Mulky alimaliza kuongea kisha akakata simu .
" Twende mume wangu.
Mulky alimwambia mume wake wakaongozana mpaka chumbani kwao.

Kwa upande wa Sameer alikuwa amekaa kwenye chumba cha hotel tena akiwa kajiandaa maana alimpania sana Mulky alihakikisha haziko salama.
" Huu ni ujinga gani sasa nimeacha wagonjwa hospitali nimekuja hapa nimetoka pesa yangu nimechukua chumba, vinywaji alafu ananiambia mambo yake ya kijinga eti oooo mume wangu mfyuuuuuu. Aliongea Sameer huku akiwa kabana pua tena huku akiwa kakasirika.

Mulky na mume wake wakiondoka wakaenda kufurahia penzi lao visiwani kwenye bonge la hotel yenye hadhi ya nyota tano.
Huko ilikuwa ni raha na furaha tupu.
Kuna muda mulky alikuwa anajutia sana kumsaliti mume wake .
Siku moja ilikuwa majira ya saa sita usiku Yasini alikuwa Kalala fofofo huku alikotoka, Mulky alikosa usingizi akawa amekaa kitandani akimuangalia mume wake huku akijisemea.
" Sijui ni shetani gani alinivaa yani nimekuja kukosa Subra dakika za mwisho kabisa, nisamehe mume wangu.

Baada ya kujutia sana alijikuta anakosa usingizi alinyanyuka kitandani akaenda kusimama mbele ya dirisha la chumba cha hotel alafu akafungua upepo mwanana uliingia ndani na kufanya nywele zake ndefu, nyepesi zilizotoka usawa wa mabega yake zipepee . Akiwa anaendelea kushangaa madhari ya kuvutia nyakati za usiku katika eneo lile . Mara aliona simu yake ikitoa mwanga, moja kwa moja alijua ni Sameer maana ndio mwenye tabia ya kumpigia usiku mkubwa.
Alipiga hatua kuifuata simu yake iliyokuwa juu ya droo ya kitanda
Alichukua simu akasngalia kwenye kioo cha screen aliona namba ambayo hajui save lakini aliitambua ilikuwa ni namba ya Sameer ambayo Yasini hakuwa anakifahamu ilitumika kwaajili ya kuwasiliana kwa wao wawili tu.

Mulky alichukua ile simu akatoka ayo nje ya kibaraza , wakati huo simu iliita mpaka kiwa imekata , Mulky alienda uwanja wa ujumbe na kuanza kuandika msg lakini kabla hajamaliza simu ikaanza kuita tena na Mulky akapokea na kuanza kuongea kwa sauti ya chini.
" Unataka nini?
" Hallow mrembo mbona hakujibu messege zangu wala kupokea simu zangu?
Mulky alinyamaza na Sameer akaendelea kuongea
" Kwahiyo uliamua kunidanganya si ndio?
" Nimetoka na mume wangu na unalijua hilo alafu hebu chukulia kilichotokea mwanzo ilikuwa ni bahati mbaya tu , na kukumbusha mimi ni mke wa mtu na mume wangu ni rafiki yako kipenzi sasa usije ukasababisha yatokee mambo ya aibu kati yetu tulimalize hili kwa wema tu.
" Mmmmmh mulky nayajua hayo yote ilamoyo wangu unanisaliti na wewe unatoka nje ya makubaliano yetu .
" Siwezi kuendelea kufanya hivyo na usinipigie tena simu sababu nipo na mume wangu. Aliongea mulky kwa ukali kisha akakata simu .

Mulky aliendelea kusimama huku akiwa anatamani kulia aliwaza atamaliza vipi swala lake na Sameer maana walipokuwa wanaelekea ilikuwa ni mbaya zaidi kwani Sameer alionekana kutokujali muda wa kumtafuta .
Akiwa bado anawaza simu yake iliingiza messege.
" Kesho sasa moja jioni nitakuwepo hapo hotelini ningependa tuonane.
Mulky alisoma alafu akafyonza .
Iliingia messege nyingine ikisema
" Hii ni lazima mimi na wewe kuonana.
Mulky alizidi kuchanganyikiwa aliamua kupiga simu baada ya muda Sameer alipokea.
" Hallow baby.
" Hivi kwanini unanifanyia hivi? Kwani kisa langu kubwa mno ni lipi, una dhamira gani na mimi jamani? Aliongea mulky huku akiwa anataka kulia.
" Hebu tulia usilie twende sawa , unakumbuka nilikutana uwe na furaha, nilijitahidi kufanya kila liwezekanalo ilimradi uwe na tabasamu, pia kumbuka nikipoteza muda wangu kukufariji, nikikupa upendo ambao sijawahi kumpa mwanamke mwingine licha ya kujua ni mke wa mtu. Lakini wewe unataka kujitupa kama takataka bila kujali nilifanya hayo yote kwaajili yangu.
" Nampenda mume wangu na wewe unajua hilo.
" Ukiongea na mimi tafadhali usimuongelee huyo mtu wako.
" Lakini.....
" Inatosha sitamani kusikia neno jingine naomba ulale na hili kesho nitakuwa hapo na nitapita simu tuonane isipo fanya hivyo basi tambua ndoa yako itakuwa matatani nitaivuruga mimi mwenyewe kwa kukuchafua haswa uwe na usiku mwema mpenzi, nakupenda.
Aliongea samez na kukata simu akamuacha mulky kaduwaa asijue inakuwaje anachomokaje kwenye hilo swala ghafla alishitukia anaguswa mabegani.

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MSHANGAZI EPISODE 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 13

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

YAMENIKUTA

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 9

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINSI YA KUTUNZA UKE

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

PART 5 MY HEART

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MY HEART 03--04

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

*MY HEART* *1---2 *

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 7

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

ANIPHA 6--7.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 05

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest