ONE NIGHT ONE MISTAKE ____________________________________* *SEHEMU YA SITA* Siku Iliyofuata Salsa alienda kazini akiwa na shauku ya kusema
Wakati huo Romex nae alikuwa chumbani kwake.
akliangalia ile hereni. "Kwahiyo huyo mwanamke kaamua kumuachia hereni kama ukumbusho wake? lle siku sitakuwa kuisahau itabaki akilini kwangu siku zote za
maisha yangu. Alipomaliza kuangalia ile hereni aliurudisha kwenye bahasha ndogo na kuiweka kwenye mfuko wa suruali alienda kuchukua viatu akavaa kisha akaenda kuchukua koti lake la suti. Lilikuwa ni koti lile alichaguliwa na Salsa ile siku
ya kwanza walipokutana Aliingiza mkono mmoja badae akasita na kuvua,
alinusa lile koti kisha akaanza kuvuta hisia. Kuna kitu.... Alijisemea kisha akaendelea kunusa tena lile koti.
"Hii harufu ya pafyumu sio mgeni kwangu, ni pafyumu ambayo alipulizia yule mwanamke, hil ni harufu ya yule mwanamke. Aliongea Romex kwa msisitizo kisha akavaa kile koti na kuondoka akaelekea kazini.
Laki bmuda wote akiwa kwenye gari alikuwa akimfikiria yule mwanamke aliyelala nae.
Kwanini siku shirika mapema na kumzuia ? Nilizaliwa kuiona sura yake. Na sijui aliingia vipi chumbani kwangu?
Romex alijiuliza maswali mengi ambayo alikosa majibu yake kwa haraka.
Salsa alifika ofisini alikuwa akihisi joto jua likikuwa linapita taratibu kwenye madirisha makubwa ya ofisi, japo kuwa kulikuwa na ac lakini Salsa aliona haitoshi allienda kufungua madirisha ili hewa iingie, alisimama dirishani
huku hewa safı ikiwa inampuliza
Alikuwa akijipanga kumfuata Romex ofisini
kwake lakini moyo wake ukidunda kwa nguvu.
"Hii ni leo, leo lazima nimuambie. alisema kwa sauti ya chini huku akijaribu kujiweka sawa.
kabla hajachukua hatua yoyote ghafla Romex alitokea, akibeba kikombe cha kahawa na keki
ndogo. Aliingia kwa tabasamu huku salsa bado akiwa kasimama dirishani lakini safari hii hakuwa anaangalia nje alikuwa anamuangalia Romex.
"Habari za asubuhil
Salama.
*Vipi unaendeleaje?
"Naendelea vizuri
Safi, natumai tangia uamke haujali kitu chochote, sasa nimekuletea kahawa na keki,
sijui itapanda?
Salsa aliangalia chini kwa hofu
"Lakini kama hautapenda naweza kukuletea chochote unachotaka.
Salsa alikosa maneno. Kila neno la kuongea, maneno na matendo ya Romex ni kama yalimziba mdomo. Alijikuta macho yake yakitoa machozi. hakuwa na nguvu ya kuzungumza
ukweli. Romex alisogea karibu, akamshika mkono
taratibu. "Salsa, tafadhali, niambie kinacho kuumiza, Niko
hapa kwa ajili yako. Romex akimvuta na kumkumbatia, Salsa alihisi ile harufu ya pafyumu yake,
Ghafla alihisi mapigo ya moyo wake ukipiga kwa
kasi, alijitoa haraka na kuziba pua yake, alitoka haraka ofisini na kukimbilia chooni kwenda kutapika "Oooh kumekucha, mimba nyingine bwana ni mtihani.
Baada ya dakika chache Salsa alirudi akiwa amechoka, alienda kukaa kwenye kiti na kujiinamia
"Vipi, unajisikia je kwani? *Kichefuchefu, kuna harufu za marashi huwa sipatani nazo kabisa hasa hiyo yako.
"Oooh samahani.
Romex alivua lile koti na kuliweka mbali kidogo. "Salsa kama hali ni mbaya naweza kukirudisha
kwa daktari.
Hapana, daktari aliniambia hii hali itaendelea kwenye hii miezi ya mwanzo tu baada ya miezi minne nitakuwa sawa. "Sasa itakula hii au nikuletee kitu kingine?
"Usijali nitatumia tu Sawa acha niende kufanya kazi nyingine. Sawa
Siku zilizidi kwenda na Romex alikuwa
alimuhudumia sana, mara kwa mara alikuwa akienda kumchungulia ofisini kwake. Siku moja Salsa alikuwa na usingizi mzito sana,
pia alikuwa akihisi joto aliamua kushuka chini kwenye tiles na kulala usingizi mzito huku pochi
yake akiwa kafanya mto.
Romex alienda tisini kwa Salsa kwaajili ya kumpelekea maji ya baridi kama kawaida yake Jakini hakumuona.
"Huyu kaenda wapi tena?
Akiwa anajiuliza mara akasikia kama kuna mtu anakoroma alipoangalia upande wa dirishani
alimuona salsa akiwa Kalala usingizi mzito
kama yupo kitandani. Romex alijikuta akishituka akasogea karibu yake
na kujaribu kumuamsha. "Salsa, salsa...
"Aaaaah niache bwana
"Hebu amka bwana, kwani unajisikia je? Romex alionekana ana wasiwasi sana na hali ya
Salsa
Salsa aliamka akakaa na kujinyosha. Nimepumzika nipo sawa sasa naweza kufanya
kazi zangu.
Alinyanyuka pale chini akapiga hatua kuelekea kwenye meza yake huku miguuni akiwa hana viatu. Romex alimuangalia huku akitingisha
kichwa chake.
Salsa alikaa kwenye kiti huku akipiga Mihayo moja kwa moja.
"Vipi una njaa?
Salsa aliitikia kwa kichwa akimaanisha ndio.
Anatamani kula nini? Natamani kula Salsa alifikiria kwanza kisha
akasema
"Natamani kula mihogo ya kukaanga lakini iwe na chachandu nyingi tena iwe na ndimi ya kutosha.
"Chachandu ni nini?
"Hujui chachandu?
Aliuliza kwa mshangao na Romex alimuangalia tu.
"Kweli huwezi kujua wewe ni wakishua. Usijali utapata unachotaka, sema na kingine
nini? Na pepsi big ya baridiiiii niweze kupooza hill koo
Sawa
Romex alipiga hatua kuelekea mlangoni lakini kabla hajafika mlangoni Salsa alimuita. "Boss.... Romex alisimama na kumgeukia. "Nilikuwa nataka big g na udongo.
"Mmmmh... Sawa.
Romex walitoka na kwenda kumtafuta mtu wa kumtuma hivyo vitu maana yeye hakuwa anajua ataipata wapi.
"Rose
"Abeee Boss.
Njooo.
Rose alienda mara moja. Unafahamu sehemu wanazouza mihogo na
changu?
Rose alicheka kidogo.
"Unamaanisha chachandu?
"Hiyo hiyo
"Ndio mbona kuna sehemu nyingi sana ila kwa mitaa ya hapa karibu hakuna mpaka kule
katikati.
Hakuna shida, nenda kaniletea mihogo chandu ya kutisha na ndimi, Big G na udongo.... "Udongo? Rose aliuliza kwa mshangao wa hali
ya juu, Romex akamkazia macho.
"Sawa nitakwenda, Rise alipokea hela.
"Nenda nje utaenda na dereva na pia hakikisha hanchelewi kurudi. "Sawa. Rose aliondoka akipofika mbele aligeuka
nyuma kumuangalia Romex. "Mmmh makubwa haya, huyu boss kapatwa na nini siku hizi au ana kusaidia mwanamke wake
ulezi wa mimba anajikuta anatamani kula vitu
vya wajawazito? Rise alijiuliza
Kwani pale kazini wengi walikuwa hawajui kuwa
salsa ni mjamzito mambo yote yaliishia ghorofa ya nne. Ila kuna baadhi ambao alikuwa karibu nae walikuwa wakihisi tu.
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni