Story.......................THE KING'S SON (MTOTO WA MFALME) Sehemu......ya.......03 "Kwanini umemuua baba yangu..!!?"
ILIPOISHIA.........
Princess Herodia pasipo kufikilia aliyaamini maneno yao nakuamua kumfata Yoashi alipokuwa amesimama........
ENDELEA NAYO...
"Kwanini umemuua baba yangu..!!?" Princess Herodia aliongea akiwa amemkaba Yoashi.
"Mimi sijamuua Baba yako wao ndio waliomuua, naomba uamini maneno yangu"
"siwezi kuamini maneno yako, hawa ni walinzi waliokuwa wakimlinda Baba yangu hawawezi kumuua Mfalme wao" Princess Herodia hukutaka kumwamini Yoashi naukizingatia ni mtu asiye mfahamu, aliamini ni mhusika wa mauaji ya baba yake.
Mda huo huo aliweza kufika Princess Miriamu nakushuhudia taharuki iliyokuwepo ya Yoashi kuhusika na mauaji kitu alichokipinga Princess Miriamu.
Tarifa zilimfikia karibu kila mtu za Mfalme Efroni kuuliwa na hofu ilikuwa kwa Mfalme Balaki mana kifo cha Mfalme mwenzake kimetokea ndani ya ufalme wake tena kwenye kasili lake la kifalme.
Upande wa Prince Yoramu alifurahi baada ya kusikia kuwa Yoashi ndiye mhusika wa kifo cha Mfalme Efroni haraka alituma walinzi wakamkamate Yoashi.
Walifika na kumkuta akiendelea kujitetea mbele ya Princess Herodia.
Walinzi walifika nakumchukua huku Princess Miriamu akijaribu kuwazuia na kitendo kile kilimkera Princess Herodia,
"Baba yangu amefia kwenye ufalme wenu na mtu aliyehusika na mauaji amekamatwa lakini wewe unamtetea..!?" Princess Herodia aliongea.
"Mimi namjua vizuri Yoashi hajahusika na mauaji ya baba yako" Princess Miriamu alimjibu. Walinzi waliomuua Mfalme Efroni walikuwa bado wapo maeneo hayo waliamua wamchukue Princess Herodia nakumtoa pale ili asiendelee kuongea na Princess Miriamu kwani kulikuwa na kila dalili ya siri yao kuwa hadhalani kwa jinsi alivyokuwa akiongea Princess Miriamu.
Princess Herodia alichukuliwa huku mwili wa Mfalme Efroni ukibebwa nakwenda kuhifadhiwa.
Upande wa Mfalme Balaki aliamua kusitisha sherehe iliyotakiwa kuanza mda mchache ujao na baadhi ya wageni walisikitika kwa kile kilichotokea huku wengine wakihisi huenda ni mpango wa Mfalme Balaki wa kumuua Mfalme Efroni.
Prince Yoramu alikuwa ni mwenye hasira baada ya siku yake kuharibika, na sehemu sahihi aliyoona inafaa ya kumalizia hasira zake ni kwa Yoashi aliondoka na kumfata Mfalme Balaki,
"Baba haina haja ya uchuguzi kufanyika Yoashi ndiye mhusika wa mauaji ya Mfalme Efroni kama inavyosemekana, hivyo inatakiwa utoe ruhusa ahukumiwe mbele ya familia ya Mfalme Efroni ili tusitengeneze uadui nao" Prince Yoramu aliongea lakini mda huo huo aliingia Malikia Rebeka na aliyasikia mazungumzo yao yote.
"Ni kweli Mfalme, Yoramu alichokiongea ndicho tunachotakiwa kukifanya" Malikia Rebeka aliunga mkono maneno yaliyozumzwa na mwanae.
Mfalme aliona ni sahihi kile kilichozungumzwa na mkewe pamoja na mwanae. Alitoa amri Yoashi aletwe na Princess Herodia aliitwa akiwa kwenye majonzi ya kumpoteza Baba yake huku akisindikizwa na walinzi, ata wale waliohusika na mauaji nao walikuwepo.
Mfalme alitoa maagizo kitanzi kiandaliwe kwa ajili ya Yoashi kunyongwa kwa kukutwa na hatia ya kumuua Mfalme Efroni.
Yoashi alisogezwa kwenye kitanzi kwa ajili ya kunyongwa.
Upande wa pili Princess Miriamu alipata tarifa za Yoashi kunyongwa haraka alikuja kwenye eneo la tukio, alifika na kukuta wakijiandaa kumtundika Yoashi kwenye kitanzi, alikimbia na alipofika alianza kuwazuia kitendo kilichomkera karibu kila mtu aliyekuwa pale.
"Una kichaa wewe..!!?, unaweza kupinga maamuzi yangu tena mbele ya wageni wangu..!?" Mfalme Balaki aliongea.
"Baba hichi mnachotaka kukifanya mnakosea Yoashi hajamuua Mfalme Efroni, naombeni mmwamini" Princess Miriamu aliongea lakini maneno yake hakuna mtu aliyeyaamini.
Mfalme Balaki alitoa amri Princess Miriamu achukuliwe na atolewe ili zoezi liweze kuendelea.
Walinzi walifanya kama walivyo ambiwa kwa kumtoa Princess Miriamu.
Walimshika na kuanza kumtoa maeneo yale huku akiendelea kupiga kelele kuwa Yoashi hausiki na chochote.
Mfalme alitoa amri zoezi liendelee la Yoashi kunyongwa lakini Princess Herodia alifikilia nakuona mtu aliyehusika na kifo cha Baba yake hatakiwi kufa mapema ivyo,
"Mwacheni msimnyonge" Princess Herodia aliongea na kuwafanya wote washangae hasa Mfalme Balaki.
"Kwanini hutaki tumuadhibu mtu aliyemuua baba yako..!?" Mfalme Balaki alimuuliza.
"Nahitaji kwenda nae kwenye ufalme wetu nikampe mateso na anieleze kwanini aliamua kumua Baba yangu" Princess Herodia aliongea na Mfalme hakuweza kumpinga.
Amri ilitolewa ya Yoashi kutolewa kwenye kitanzi na alichukuliwa na walinzi wa Princess Herodia.
Hawakutaka kukaa tena kwenye ufalme wa AZENI, walichukua mwili wa Mfalme Efroni na kuondoka.
Safari ilianza huku Yoashi akifungwa kamba na Farasi alianza kumvuta yani ilikuwa akizembea kidogo tu basi mwili wake unavulutwa na Farasi ilimlazimu awe anakimbia ili asivulutwe na Farasi.
Princess Herodia na walinzi wake hawakujali kuhusu tabu aliyokuwa akipitia Yoashi wao waliendelea na safari.
Upande wa Princess Miriamu aliamini tayari Yoashi ameshanyongwa ila aliletewa tarifa na mtumishi wa jumba la kifalme zilizomfanya ajiulizie kipi kilichomfanya Princess Herodia abadilishe maamuzi na amue kuondoka na Yoashi.
Prince Yoramu nae alishikwa na hofu baada ya Yoashi kuchukuliwa na Princess Herodia alimfata Malikia Rebeka,
"Mama nashikwa na mashaka huenda Yoashi akarudi siku moja kuja kutuzulu, nilitaka afe kabisa" Prince Yoramu aliongea.
"Sio wewe tu ata mimi pia ila yote haya kaya sababisha baba yako mana niliwahi kumwambia lakini alipuuzia, inatakiwa ufanye jambo ili Yoashi asije kuleta matatizo kwenye familia yetu"
"Jambo gani ninalotakiwa kufanya ikiwa tayari ameshaondoka na Princess Herodia..!?", Prince Yoramu alihoji na kutamani kujua Malikia atamshauri kitu gani.
"Inatakiwa utengeneze ukaribu na Princess Herodia, kwakuwa Yoashi yupo kwenye mikono yake basi ukiwa karibu na Princess Herodia utakuwa karibu na Yoashi na utafahamu kila kitu kitakacho kuwa kikiendelea kwa upande wake" Malikia Rebeka aliongea na Prince Yoramu alikubaliana na maneno ya mama yake kilichokuwa kimebaki ni namna ya kutengeneza ukaribu na Princess Herodia kama mama yake alivyomwambia.
**********************************
Prncess Herodia aliweza kufika akiwa na walinzi wake ndani ya jumba lao la kifalme,
Malikia wa ufalme huo aliyefahamika kwa jina la Malikia Ruth alipatiwa tarifa za ujio wao, haraka alitoka na lengo lake likiwa ni kumpokea Mfalme Efroni kama ilivyo kawaida bira kujua tayari hayupo kwenye dunia hii.
Alifika na kukutana na mazingira tatanishi kidogo kwani alishuhudia maiti ya Mfalme Efroni nakuyafanya macho yake yasiamini kile alichoweza kukiona, alimsogelea binti yake ili amuulize vizuri,
"Niambie mwanangu, sitaki kuamini kama aliyefariki ni Mfalme" Malikia Ruth aliongea nakumfanya binti yake awe na kazi ya kumuelezea.
"Ni yeye mama ni mwili wa baba huo" Princess Herodia alimjibu.
Malikia Ruth aliusogelea mwili wa mmewe na kuanza kuangua kilio.
Yoashi alikuwa mtazamaji kwa kile kilichokuwa kikiendelea. Princess Herodia alimsogelea mama yake na kumuonesha Yoashi waliyekuja nae kwenye ufalme wao kuwa ndiye mtu aliyehusika na kifo cha Mfalme Efroni.
Baada ya kupewa tarifa zile Malikia Ruth alifuta machozi yake na kumsogelea Yoashi hakutaka kumuuliza pale pale alianza kumshushia kipigo kwa kumpiga ngumi na makofi licha ya kuwa ni mwanamke ila maumivu Yoashi alikuwa akiyapata kutokana na kipigo alichokuwa akipigwa.
"Nendeni mkamfungie huko tukimaliza mazishi nitadili nae mwenyewe" Malikia Ruth aliongea na kuwafanya walinzi wafanye kile walichoambiwa na Malikia wao.
Msiba ulikuwa mkubwa ndani ya ufalme huo, raia wa kawaida walihuzunika kumpoteza Mfalme wao mana alikuwa akiwajali ila wengi wao walipatwa na hasira baada ya kusikia mtu aliyehusika na mauaji ya Mfalme Efroni amekamatwa na kaletwa kwenye ufalme wao wengi walitamani auliwe mda huo huo.
Malikia Ruth aliunga mkono maneno ya raia wake ila Princess Herodia alikuwa kinyume nao kwani alitaka kuona Yoashi akiteseka kwanza ndiyo afe.
Malikia Ruth kwa upendo aliokuwa nao kwa binti yake aliamua kuyakubali mawazo yake, alisubiri kuona ni kitu gani Princess Herodia alichopanga kufanya.
Baada ya msiba kuisha kwenye ufalme huo wa GALA taratibu zingine ziliendelea za Yoashi kuathibiwa.
Princess Herodia kitu cha kwanza alichopanga kufanya kwa Yoashi ni kutoa amri kwa walinzi wake kwenda kumfungia katikati ya mji na raia wote waliitwa,
"Huyu ndiye mtu aliyehusika na mauaji ya Mfalme wetu, hatutaki afe kwa sasa ila tunataka ateseke kwanza..... Princess Herodia aliendelea kuongea.....kila siku mtu atakayejisikia kutoa adhabu kwa mtu huyu basi atakuwa anakuja nakumpiga kibao kimoja na kumtemea mate....hiyo ni adhabu ndogo kwake baada ya hapo itafata adhabu kubwa itakayomfanya yeye apoteza maisha" Princess Herodia alimaliza kuongea na baadhi yao walikubaliana na maneno yake huku wengine wakidai ni adhabu ndogo aliyopatiwa kwani walitaka afe hapo hapo.
Siku iliyofata asikari wa jumba la kifalme walifanya kama Princess Herodia alivyoagiza, Yoashi alienda kufungwa katikati ya mji huku asikari wakilinda ili watu wasije kumuua moja kwa moja, haikupita mda watu walianza kuja kila mtu alifika na kumpiga kibao na kukusanya fundo la mate mdomoni na kumtemea Yoashi...........ITAENDELEA.
Mimi mwenyewe natamani kujua kitatokea nini kuhusi Yoashi karibu kwenye sehemu ya 4
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi