Story.......................THE KING'S SON (MTOTO WA MFALME). Sehemu......ya.......04 Watu wa kila aina walikuja na kufanya kama wenzao walivyokuwa wakifanya
ILIPOISHIA.......
Haikupita mda watu walianza kuja kila mtu alifika na kumpiga kibao na kukusanya fundo la mate mdomoni na kumtemea Yoashi........
ENDELEA NAYO...
Watu wa kila aina walikuja na kufanya kama wenzao walivyokuwa wakifanya. Mashavu ya Yoashi yalivimba na alizimia kutokana na kupigwa makofi kwa mda mrefu huku mdomo wake ukitapakaa damu.
Walinzi walifanya kama walivyopewa maagizo na Princess Herodia, walienda kumchukua Yoashi kwa ajili ya kwenda kumfungia. walimfikisha na kumpatia chakula ili aendelee kuishi wapate kumtese vizuri. Yoashi alikataa kula kitu kilichowakasilisha Walinzi,
"Kula wewe mjinga" Mlinzi alimpa amri Yoashi na alikula bira kupenda huku chakula kikipita kwa tabu kutokana na mdomo wake kuchanika.
Upande wa Malikia Ruth akiwa na binti yake aliongea kitu kilichomshangaza Princess Herodia,
"Mwanangu sikutegemea kama Mfalme angekufa mapema kiasi hichi, hivyo kuna kitu lazima nikifanye"
"Kitu gani mama...!?"
"Nataka niolewa kwa mara nyingine tena" Malikia Ruth aliongea na kumfanya mwanae ashangae kwa kile alichokizungumza.
"Mama nini unachoongea..!?, wewe tayari ni Malikia na unaweza ukauendesha huu ufalme pasipo kuwa na uwepo wa Baba kwanini utake kuolewa kwa mara nyingine tena..!!?" Princess Herodia hakufurahishwa na kile kilichozungumzwa na Malikia Ruth na alipinga vikali.
"Umeshachelewa mwanangu tayari nimeshafanya maamuzi" Malikia Ruth aliongea na kuondoka akimuacha mwanae huku akimtazama.
Princess Herodia alitamani kujua ni nani anayetaka kumuoa mama yake tena gafra kiasi hicho.
**********************************
Kwenye ufalme wa AZENI. Princess Miriamu alikuwa ni mtu mwenye mawazo baada ya Yoashi kuwa mbali nae na mtumishi wake wa karibu alilitambua hilo, akiwa kama mfanyakazi aliamua kupeleka tarifa kwa Malikia Rebeka na alikuja mida hiyo kwa ajili ya kujua kipi kilichomfanya binti yake akose amani,
"Kipi kinachokusibu Miriamu mbona umebadilika gafra hivyo binti yangu...!?" Malikia Rebeka alimuuliza.
"Sina tatizo lolote lile mama" Princess Miriamu alimjibu na kujaribu kuonesha tabasamu.
"Anakudanganya huyo mama, anachokiongea sicho kilicho kwenye moyo wake" ilikuwa ni sauti ya Prince Yoramu aliyefika mida hiyo na alisikia mazungumzo yao.
"Unataka kusema nini Yoramu...!??" Malikia Rebeka ilibidi amhoji kijana wake.
"Mama huyo ana muwaza Yoashi, alizoea kuwa nae karibu toka tukiwa wadogo na leo yupo mbali nae...au nasema uongo Miriamu..!?" Prince Yoramu alimwambia mama yao huku akimuuliza swali Princess Miriamu.
Malikia Rebeka aligundua kuna kitu kilichojificha kwenye moyo wa binti yake kwa kile alichoambiwa na Prince Yoramu. alienda kwa Mfalme Balaki na kumshauri wamtafutie mwanaume atakaye muoa Princess Miriamu. Mfalme Balaki hakutegemea kupokea tarifa zile kutoka kwa Malikia Rebeka aliamua kukubali.
Mipango iliandaliwa ya Princess Miriamu kutafutiwa mwanaume wa kumuoa bira Princess Miriamu mwenyewe kupatiwa tarifa na huo ulikuwa mpango wa Malikia Rebeka kwani hakutaka binti yake ajue kuwa wanamtafutia mwanaume.
Baada ya siku kadhaa kupita walifanikiwa kumpata kijana aliyekuwa mtoto wa moja ya viongozi wakubwa ndani ya ufalme huo wa AZENI.
Princess Miriamu aliletewa tarifa za yeye kutafutiwa mwanaume kitu kilichomshangaza na aliamua kumfata Malikia Rebeka kwa ajili ya kwenda kusema kile alichokikusudia kukisema,
"Mama najua mimi ni mtoto wa Mfalme lakini hamuwezi kunichangulia mwanaume nisiyempenda" Princess Miriamu aliongea na alioneshwa kuchukizwa na tarifa za yeye kuolewa na mwanaume asiyemtaka.
"Huu ni utaratibu wa kifalme kazi yako nikujiandaa kwa ajili ya ndoa na sio kingine"
"Sitoweza kufunga ndoa, hii ni ahadi yako kwangu" Princess Miriamu alimjibu mama yake nakuondoka.
"Mtoto mjinga sana huyu nilichokuwa nakiwaza kumbe kilikuwa sahihi, itakuwa tayari alikuwa na mahusiano na Yoashi.... subiri nitamuonesha" Malikia Rebeka aliongea baada ya kubaki peke yake.
*********************************
Ndani ya ufalme wa GALA katika jumba la kifalme, Malikia Ruth siku hiyo akiwa amesimama akitafakari maelewano yaliyopo kati yake na binti yake Princess Herodia kupungua na hii ni baada ya kumtamkia kuwa ataolewa mda sio mrefu kitu kilichopingwa na Princess Herodia, kuna mtu alikuja kumkumbatia na kumfanya Malikia Ruth ageuke kumtazama mtu aliyemkumbatia,
"Ni wewe Boazi..!!" Malikia Ruth aliongea baada ya kumuona Boazi.
"Ni mimi Malikia wangu nimekuja kupata jibu langu la sisi wawili kufunga ndoa" Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Boazi aliongea.
"Siwezi kuvunja ahadi yangu kwako jiandae kesho tutafunga ndoa na haitakuwa na maandalizi mengi" Malikia Ruth aliongea na kumfanya Boazi azidi kumkumbatia zaidi bira kuogopa kama ni Malikia wa GALA.
Wakati yote yanafanyika kuna mfanyakazi aliyepewa kazi na Princess Herodia ya kumfatilia Malikia Ruth, alitoka na kwenda kumpatia tarifa,
"Princess nimegundua ni nani anayetaka kumuoa Malikia Ruth".
"Nahitaji kumjua ni nani huyo" Princess Herodia hakutaka kusikia maneno mengi kutoka kwa mtumishi wake alichokuwa akihitaji kusikia ni jina la mwanaume anayetaka amuoe mama yake.
"Princess, Boazi ndiye anayetaka amuoe Malikia".
"Nini unachokiongea wewe..!?"
"Ndio Princess, nimesikia Malikia akitaja siku ya ndoa ambayo ni siku ya kesho" mfanyakazi alizidi kuongea na maneno yake yalizidi kumkera zaidi Princess Herodia.
"Hiyo ndoa haitowezekana labda sio mimi, Boazi alikuwa rafiki wa karibu sana na baba pia alipatiwa cheo kikubwa iweje leo aje kumuoa mama yangu tena gafra ivi...!!" Princess aliongea na alipanga kufanya kitu ili azuie ndoa ya mama yake.
Upande wa Yoashi ndani ya ufalme huo bado alikuwa akiendelea kupokea adhabu yake kama ilivyo amuliwa na Princess Herodia, walienda kumfungia katikati ya mji ili watu waje wampe adhabu.
Siku hiyo ilikuwa tofauti kwani Alikuja raia na alipomaliza kumpiga kofi kama wenzake walivyokuwa wakifanya alisogea pembeni na kuchukua jiwe, alimponda Yoashi na kumpiga kichwani hali iliyoanza kuwaogopesha walinzi kwani Yoashi alinyamaza kimya,
"Mumwangieni maji huenda ata amka" moja ya Walinzi aliongea na wenzake walifanya kama alivyoongea lakini hakuweza kuamka.
"huyu itakuwa ameshakufa tayari, kwanza hali yake ni mbaya na ana vidonda karibu mwili mzima" Mlinzi mwingine aliongea na haraka tarifa zilipelekwa kwa Princess Herodia.
Princess Herodia siku hiyo alikuwa na mawazo ya kuzuia harusi ya mama yake, baada ya kupokea tarifa za Yoashi kushindwa kuamka alitoa amri wakammalizie kumuua Yoashi kama bado hajafa na maiti yake ikatupwe, walinzi walirudisha tarifa kwa wenzao.
Yoashi alifungulia na kuanguka chini kama mzingo huku akiwa hajitambui moja ya Walinzi alichukua mkuki wake na kumchoma nao tumboni ili afe kabisa.
"Huyu tayari kaisha kufa, kama umemchoma mpaka na mkuki lakini bado haongei wala hatoi sauti ya maumivu ina maanisha kuwa ameshakufa, inatakiwa tumbebe tukamtupe kwenye maporomoko ya maji".
Baada ya mwenzao kuongea wote walikubaliana na kile alichokisema walimbeba na kumpeleka kwenye maporomoko ya maji, na walipomfikisha walimurusha na kushuhudia kwa macho yao akipelekwa na maji yaliyokuwa yakielekea chini kwa kasi katika bonde hilo refu, waliamua kugeuka na kurudi kwenda kumpa tarifa Princess Herodia kuwa kazi imeshakamilika.
Yoashi baada ya kutupwa aliangukia mpaka chini na kudumbukia kwenye maji, maji yalimchukua na kuanza kumpeleka kule yalipokuwa yakielekea na haikujulikana kama ameshapoteza maisha au bado mzima.
Tarifa aliletewa Princess Herodia za Yoashi kufa na kutupwa kwenye maporomoko ya maji alifurahi kusikia mtu aliyemuua baba yake amepoteza maisha, ila bado alikuwa kwenye mawazo mazito juu ya ndoa ya mama yake inayotalajiwa kufungwa siku ya kesho, aliamua kumfata Malikia Ruth ili aongee nae kwa mara mwisho kabra hajafanya maamuzi.
Ujio wake ulimfanya Malikia Ruth atambue kuwa haukuwa wa amani,
"Bira shaka unataka kuniuliza kuhusu ndoa yangu nitakayoenda kufunga siku ya kesho...!?" Malikia Ruth aliamua kumuwahi Princess Herodia kabra hajaanza kumuongelesha yeye.
"Hujakosea mama ndicho kilichonifanya niwe hapa, natamani kujua kwanini umechukua maamuzi ya wewe kuolewa na Boazi tena ni siku kadhaa toka baba afariki..!!?" Princess Herodia alimhoji mama yake.
"Inatakiwa ukumbuke kuwa mimi ni mama yako na najua mengi kuliko wewe unayoyajua hivyo ata nikikujibu bado hautonielewa ni vyema ukaendelee na mambo yako, haya ya ndoa niachie mimi mwenyewe" Malikia Ruth aliongea na kumfanya Princess Herodia aondoke kwa hasira mana aliona mama yake kathamilia kufanya kile alichopanga kufanya.
Nje ya jumba hilo la kifalme Boazi alikuwa akiongea na vijana aliowapa kazi ya kwenda kumuua Mfalme Efroni.
"Mmefanya kazi kubwa sana na nimebakiza hatua chache niweze kukamilisha mpango wetu wa mimi kuwa Mfalme"
"Hongera mkuu" kila mtu alimpa pongezi lakini Kuna Mlinzi mmoja alifika na kumpatia tarifa,
"Mkuu Princess Herodia anapanga kuja kuzuia ndoa yenu siku ya kesho" Mlinzi huyo aliyepewa kazi ya kupeleleza kile kilichokuwa kikiendelea kwenye jumba la kifalme aliongea.
"Huyo Princess naona hanijui vizuri ngoja nimuoe mama yake alafu baada ya hapo nimuonyeshe kuwa mimi ni mtu wa aina gani" Boazi aliongea.......ITAENDELEA.
Boazi atamfanya nini Princess Herodia baada ya yeye kuwa Mfalme tukutane sehemu ijayo.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi