Story.......................THE KING'S SON (MTOTO WA MFALME) Sehemu......ya.......02 ILIPOISHIA........ Bahati mbaya ilikuwa kwake kwani alishangaa kumuona Prince Yoramu
ENDELEA NAYO...
"Huwezi kuondoka kirahisi hivyo Yoashi, nilijua lazima Princess Miriamu akushauri wewe kutoroka......Prince Yoramu aliendelea kuongea......kitu usichokijua ni kuwa hisitoria yako yote naifahamu ndiyo mana sitaki kuona ukienda mbali na ufalme huu" Prince Yoramu aliongea maneno yaliyomfanya Yoashi mwenyewe ashangae na kumsogelea.
Zilikuwa ni tarifa mpya kwake kwani ata yeye alikuwa hajui hisitoria ya maisha yake.
"Nini unachoongea Prince...!?, naomba uniambie vizuri mimi ni nani na wazazi wangu wako wapi..!?" Yoashi alimuuliza lakini Prince Yoramu aliwageukia walinzi wake.
"Mpelekeni ndani na muwe makini nae, hakikisheni hapati nafasi ya kutoroka kwenda sehemu yoyote ile " Walinzi walifata amri kwa kumkamata Yoashi na kumrudisha ndani huku akiwa na maswali mengi yakutamani kujua kiundani zaidi maneno yaliyo zungumzwa na Prince Yoramu.
Princess Miriamu alishangaa kumuona Yoashi ndani ya ngome ya kifalme mana alitegemea mida hiyo angekuwa ameshaondoka na amefika mbali. alienda kumuuliza Yoashi sababu za yeye kurudi ndani ya ngome ya kifalme naye aliamua kumwelezea kila kitu Princess Miriamu.
Princess Miriamu alimfata kaka yake ajue ni kitu gani alichopanga kumfanyia Yoashi,
"Kaka una matatizo gani..!?. umepanga kumfanyia nini Yoashi mpaka umzuie yeye kuondoka...!?" Princess Miriamu aliongea na alioneshwa kuchukizwa na kile alichokifanya kaka yake.
Prince Yoramu hakutaka kumjibu Princess Miriamu badala yake aliamua kuondoka na kumuacha akimtazama.
Prince Yoramu baada ya kuachana na Princess Miriamu aliitwa na Malikia Rebeka,
"umepanga kufanya nini kwenye siku yako mhimu mwanangu...!?" Malikia Rebeka aliongea nakutaka kufahamu kitu alichokuwa akifikilia mwanae.
"Mama, hakuna cha maana nitakachofanya zaidi ya kumfanya Yoashi aishi kwenye ngome hii ya kifalme maisha yake yote. Pia uliniambie nisije kumpa nafasi Yoashi ya kuwa huru na nimfanye awe mtumwa wangu mpaka kufa kwake" Prince Yoramu aliongea na Malikia Rebeka alimsifu kwa kile alichopanga kufanya.
Malikia Rebeka alimwambia anatakiwa awe makini zaidi kwani siku Yoashi akija kujua kuwa Mfalme Balaki aliiangamiza familia yake basi naye atawapoteza wazazi wake.
Huo ndio ulikuwa wasiwasi wa Malikia Rebeka na aliendelea kumhimiza mwanae azingatie maneno yake. Prince Yoramu alimwahidi Mama yake ata hakikisha Yoashi hatokuja kuleta madhala kwenye familia yao.
Wageni mbali mbali walialikwa na walianza kuwasili kwenye ufalme wa Mfalme Balaki kwa ajili ya kushuhudia sherehe ya Prince Yoramu na moja ya wageni waliokuja siku hiyo ni Mfalme Efroni aliye ongozana na binti yake aliyefahamika kwa jina la Princess Herodia.
Mfalme Efroni na binti yake walikaribishwa vizuri ndani ya ngome hiyo ya kifalme, huku wakiongozana na walinzi baadhi waliotoka nao kwenye ufalme wao na baadhi ya walinzi waliokuja nao walikuwa na lengo la kumuua Mfalme Efroni pasipo yeye mwenyewe kujua.
Upande wa Yoashi akiwa ndani ya jumba la kifalme huku nyuma akiwa na ulinzi wa kutosha aliowekewa na Prince Yoramu kwa ajili ya yeye kutokutoroka, Princess Miriamu alifika na kushika mkono wa Yoashi,
"una mpeleka wapi..!?" mlinzi mmoja alimuuliza lakini Princess Miriamu aliona kama dharau kwa swali aliloulizwa na mlinzi.
Alimsogelea na kumpiga kibao,
"Umetoa wapi nguvu ya kuniuliza..!? umesahau kama mimi ni mtoto wa Mfalme...!?".
"Nisamehe Binti Mfalme sitarudia tena kukuuliza swali kama hilo" mlinzi aliongea lakini Princess Miriamu hakutaka kuongea zaidi alimuchukua Yoashi nakuondoka nae huku wakiwaacha walinzi wakiwatazama na mlinzi mmoja alikimbia kwenda kumpa tarifa Prince Yoramu.
Yoashi baada ya kupata msaada wa kuchukuliwa na Princess Miriamu, kuna kitu alichotamani kumuuliza Princess Miriamu,
"Princess kwanini unanijali kiasi hiki...!!?"
"unataka kujua kwanini nakujali Yoashi...!?" Princess Miriamu nae alimuuliza swali Yoashi badala ya kujibu kile alichoulizwa.
"Ndio Princess, mana toka tukiwa wadogo umekuwa upande wangu siku zote bira kujali kuwa mimi ni mtumwa ndani ya ufalme wenu"
"Sababu kubwa ya mimi kukujali nikuona siku moja ukiwa ni mwenye furaha, nachukizwa na jinsi kaka yangu anavyokutesa.....Princess Miriamu aliongea kwa huzuni na maneno yake aliyaelewa vyema Yoashi..... Princess aliendelea kuongea..... Kwakuwa kaka hataki wewe uondoke basi leo unatakiwa uwe karibu yangu mda wote kwa ajili ya usalama wako zaidi mana nahisi kaka kuna kitu alichopanga kufanya zidi yako".
Yoashi hukuwa nacha kupinga alikubali kuongozana na Princess Miriamu popote pale atakapokuwa akienda mana ndiyo msaada pekee aliokuwa nao kwa wakati huo.
Prince Yoramu aliletewa tarifa za Princess Miriamu kumchukua kinguvu Yoashi kutoka kwa walinzi wake ila aliwaambia wahakikishe Yoashi hatoki ndani ya ngome ya kifalme.
Wageni mbalimbali waliendelea kuwasili kwenye sherehe hiyo huku Mfalme Balaki akiwapokea wageni wake nakuwatembeza sehemu mbalimbali.
Mfalme Efroni akiwa na binti yake nao waliendelea kuzunguka ndani ya ufalme huo pasipo kujua kama baadhi ya walinzi waliokuja nao wanampango wa kumuua Mfalme Efroni. walifika sehemu na Princess Herodia hakutaka kuongozana na baba yake mana aliona kama ananyimwa uhuru wa kutembea, aliondoka pasipo kumtarifu Mfalme Efroni.
Baadhi ya walinzi waliokuwa na lengo baya kwa Mfalme Efroni walifurahi baada ya kuona Princess Herodia kaondoka. Mmoja wao aliwaambia walinzi waliokuwa nje ya mipango yao wamfatilie Princess Herodia kwa ajili ya usalama wao, nao pasipo kujua waliondoka na kumuacha Mfalme Efroni.
Walinzi waliokuwa na mipango ya kumuua Mfalme walifurahi baada ya kubaki wenyewe na walichokuwa wakisubiri Mfalme afike sehemu nzuri ili waweze kufanya kile walichopanga kufanya.
Princess Herodia aliendelea kutembea na alijihisi ni mwenye furaha kwa kile alichokuwa akikiona ndani ya ufalme huo kwa mbali aliweza kumuona Princess Miriamu akiwa na Yoashi wakija upande wake, walikutana na kupishana huku kila mtu akiendelea na safari yake.
Princess Miriamu alifika sehemu na kumgeukia Yoashi,
"Naomba unisubiri hapa nakuja mda sio mrefu" Princess Miriamu aliongea nakuondoka akimuacha Yoashi sehemu aliyomwambia amsubiri na hakukuwa na mtu mwingine zaidi yake. Yoashi aliamua kumsubiri Princess Miriamu lakini akiwa pale aliweza kufika Mfalme Efroni akiwa na walinzi wake wenye mipango mibaya zidi yake.
Mfalme Efroni alianza kumwongelesha Yoashi aliyetoa heshima mbele yake huku walinzi wakiwatazama. Mlinzi mmoja alifikilia nakuona hiyo ndiyo nafasi ya wao kumuua Mfalme Efroni mbele ya Yoashi aliyekuwa na mwonekano wa kitumwa ndani ya ufalme huo.
Upande wa Princess Herodia baada ya kuchoka kutembea aliamua kurudi sehemu aliyotoka ili akaonane na baba yake au Mfalme Efroni.
Mfalme Efroni alikuwa bado akimwongelesha Yoashi na alivutiwa zaidi na unyenyekevu aliokuwa nao Yoashi lakini wakiwa kwenye maongezi, Mlinzi mmoja alichukua upanga wake na kumchoma Mfalme Efroni.
Yoashi alibaki kwenye mshangao baada ya kushuhudia kwa macho yake Mfalme Efroni akichomwa upanga na moja ya walinzi wake. Baada ya Mfalme Efroni kuchomwa upanga pale pale alianguka chini huku upanga ukiwa kwenye tumbo lake na mda wote Yoashi alikuwa bado kwenye mshituko kwa kushuhudia tukio lile.
Mlinzi mwingine alianza kumsogelea Yoashi ili amumalize lakini mwenzake alimshika mkono nakumzuia na kumpa ishala kuwa kuna mtu anakuja.
Alimwonyesha mtu aliyekuwa nyuma yao akija huku akikimbia kuwafata wao walipo, hakuwa mwingine bali alikuwa Princess Herodia aliyefika pale, nakuanza kumtikisa baba yake lakini alikuwa ameshachelewa kwani tayari Mfalme Efroni alikuwa ameshafariki.
Moja ya mlinzi aliandaa upanga wake ili amuue Princess Herodia lakini mwenzake alimpa ishara ya kutokujaribu kufanya kitu kama hicho kwani kuna kitu alikifikilia.
Mlinzi aliyemzuia mwenzake asimuue Princess Herodia alimutazama Yoashi aliyekuwa akiwaangalia kwa hasira na kabra hajatoboa siri yao mbele ya Princess Herodia mmoja wao aliamua kuongea,
"kwanini umemuua Mfalme wetu...!?" aliongea huku akipeleka lawama kwa Yoashi na wenzake walianza kuongea kama mwenzao wakimulaumu Yoashi.
"Umemuua Mfalme wetu" mwingine nae aliongea.
"Mnanisingizia nyie ndiyo mliomuua Mfalme wenu wenyewe" Yoashi aliamua kujitetea hakutaka kupewa kesi isiyo kuwa yake.
Kutokana na uwingi wao walimwaminisha Princess Herodia kuwa Yoashi ndiye kamuua Mfalme wao na Princess Herodia pasipo kufikilia aliyaamini maneno yao nakuamua kumfata Yoashi alipokuwa amesimama.......ITAENDELEA.
Yoashi ataongea nini mbele ya Princess Herodia ili amwamini kuwa hausiki na kifo cha Mfalme Efroni..?. sehemu ya 3 ina majibu zaidi.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi