AIBU YA KUCHELEWA KUOLEWA ILINIFANYA NIKAOLEWA NA JINI ????????
Sehemu ya Nne ( 4 )
*************
@Kila Mtu
????????????????????????????????????????????????
..Kinyonge nilifuta machozi na kuinuka nikitaka kwenda chumbani ila msichana wangu wa kazi alikuja na kusimama mbele yangu huku akiwa na glas ya maji. Nilimuangalia na kumtaka anipishe nipite akanambia " samahani dada naweza kuongea na wewe?" "Hapana Zubeda sio sasa, kama kuna lolote unalo hitaji tumia pesa yako nitakurudishia kesho na usinihesabie chakula" "Sihitaji pesa ila nataka kuongea na wewe kuhusu wewe mwenyewe "Kauli yake ilinishtua nikamuuliza "kuhusu mimi ukimaanisha nini?" "Kama hutojali naomba ukae samahani lakini" Nilimuangalia bila kusema kitu nikakaa kumsikiliza,binti alishusha pumzi na kunyosha mkono kunipatia maji. "Sijakuomba haya ongea nimechoka nataka nikapumzike " niliongea huku nikiwa nimekunja uso, Zubeda aliweka glass pembeni na kusema. "Aaam! dada nilitaka kuongea na wewe kuhusu swala la ndoa , najua hutaki kusikia hili ilafamilia yako iko sahihi wewe sasa ni mtu mzima unapaswa kuwa na kwako." "Napaswa kuwa na kwangu hapa ni kwa kwako?" "Hapana sina maana hiyo maana yangu ni kuwa unatakiwa kuolewa uwe na mume na watoto, maana umri wako umeenda sana. Hivi unajua dada yangu ambae umelingana nae sasaiv anawatoto wa tatu, ukiachana na huyo anaemfuata nae ameshaolewa na anamtoto mmoja na hivi karibuni atapata mtoto wa pili.Na wote hao wamesoma na wanakazi zao japo sio nzuri kama yako ila walichukua uamzi sahihi na mapema " Zubeda alivyo ongea hivyo nilimuangalia kwa sekunde kadhaa Kisha nikamwambia " Inaonekana uhuru ulionao unakuzuzua sana, hivi unapata wapi nguvu ya kuacha kazi zako na kuja kunikalisha hapa kwa mambo ya kipuuzi namna hii?. Mimi kuolewa au kuto olewe we kunakuhusu nini ?" "Samahani sana dada ila nimeona nikwambie ukweli lakini kama nimekukwaza nisamehe "Niliinuka nikapiga hatua kadhaa nikasimama na kumwambia "hii iwe mwanzo na mwisho kuongea na mimi kuhusu hiki kitu. Fanya kazi zako ukichoka kalale nasio kuongea yasiyo kuhusu" Niliongea na kuingia chumbani kwangu , nilifika na kukaa kitandani huku macho yakiwa kwenye picha ya Adam iliyokuwa ukutani. Niliangalia kwa mda mrefu na kukumbuka mambo mengi tuliyokuwa tukifanya pamoja , uongo dhambi nimekuwa kwenye mahusiano lakini hakuna mahusiano yalikuwa moto kama hili .Tulipendana na niliiona ndoa hii hapa ,lakini kama yalivyokufa mengine nalo limekufa . Kinyonge niliamka na kuchukua sm yangu nikaanza kuangalia picha za harusi za rafiki zangu, nakukumbuka story ya mahusiano ya kila mtu. Kwa sauti iliyojaa uchungu nikasema " Mungu nimefanya nini kibaya kiasi cha kunifanya kila mahusiano ninayoingia kuishia njiani. Kwanini naachwa mimi kila siku, je me nimbaya? Au sifai kuwa mke wa mtu? Mbona sina tabia chafu,wala sijawahi kumuumiza mtu labda tuseme ndio maana napitia haya.Miaka 30 sina mahusiano ya kueweka, kila mtu anaekuja kwangu hadumu bali huja na kunitumia kisha anapotea bila hata sababu ya msingi. Na mbona nimekuomba sana au maombi yangu hayana nguvu kiasi ambacho hutaki kunijibu, kama ni hivyo tafadhali angalia kiu yangu na uniokoe. Nakama kuna kitu nilichofanya ambacho ndio sababu ya mimi upitia haya tafadhali nioneshe nitatubu hata ikibidii kuadhibiwa niko tayari ila tu nivushwe hapa."Niliongea kwa uchungu huku machozi yakinitoka, mwisho nikapanda kitandani na kujikunja kama kifaranga alienyeshewa na mvua. Taratibu mda ulienda usingizi nao ukashika nafasi yake nililala na kesho yake asubuhi niliamka na kuchoma vitu vyote vya Adam . Na baada ya kuhakikisha nimeondoa kila kitu nilioga na kutulia chumbani huku nikiendelea kuufariji moyo wangu. Mara simu yangu iliita kuangalia mpigaji ni rafiki yangu Wema , niliiangalia kwa mda kidogo huku nikijifikilia kupokea .Lakini mood yangu ilinigomea ,sikuwa nikijisikia kuongea au kufanya lolote zaidi ya kuwa mwenyewe. Mda ulienda jioni ilipofika Wema aliamua kuja naona ni baada ya kuona sipokei sm zake , basi baada ya kufika ilinilazimu kutoka chumbani na kukaa nae seblen. "Elena! Kuna shida gani mbona ulikuwa hupokei sm zangu?" Aliongea Wema baada ya salamu, kwa sauti ya chini nikamjibu. "Nisamehe bure nilikuwa nimelala ,mh ulikuwa unasemaje kuna mpya?""Aaah kwahiyo me kukupigia hadi niwe na mpya?" "Hapana ila nimeuliza tu huenda zikawepo" Wema alikaa kimya kidogo na kusema " nahisi zipo , Elena kuna kitu nimeona na nashindwa kuelewa nini kinaendelea " "Kitu gani tena mbona unanitisha " "Umeachana na Adam?" Swali lake lilinifanya nikashusha pumzi na kumjibu. "Yeah ""Acha masiala tena ? Ndugu yangu kwani imekuwaje ?" "Imekuwa hivyo hivyo basi" "Imekuwaje hivyo hivyo , kwani nini kimetokea hadi mkaachana na mmeachana lini?" "Kabla sijakujibu umejuaje kama tumeachana?" "Umeanza ,we jibu ilikuwaje na nilini " "Okay ,ilikuwa siku moja kabla ya ndoa mdogo wako , na kuhusu kilichotokea ni......" nilishindwa kuongea nikabaki kimya .Wema alinikazia macho na kuniuliza " ulimcheat? Au ulimjibu vibaya maana akili zako unazijuaga mwenyewe" Nilitabasamu na kumwambia " unanijua nikiingia kwenye mahusiano huwa sitaki kuwa na makando kando so swala la kucheat kwangu halipo" "Okay huku cheat sasa imekuwaje mkaachana maana mlikuwa vizuri " "Mmh! Ukweli nikwamba hatuku gombana na ila ilitokea tu akaamua kuvunja kila kitu""Bwanae unazunguka sana ,yaani alianzaje anzaje hadi mkafikia hatua ya kukatisha kila kitu " Kabla ya kumjibu Wema nilimuangalia kwa sekunde kadhaa Kisha nikamwambia . "Aam siku moja kabla ya kuachana tulitoka out kama kawaida yetu ,tukala na kuongea vitu vingi sana na mda wa kurudi nyumbani ulipofika tukarudi na kulala . Sasa asubuhi niliamka nikiwa nawaza sana kuhusu hatma ya mahusiano yetu, nilifikilia ni mwaka wa pili toka tuanze mahusiano lakini hakuna siku ambayo Adam aliongea kuhusu ndoa.Wala si kuongea tu hata zile ishara zakuwa anampango hazikuonekana so nikaona si mbaya kama nikimuuliza ili nijue anafikilia nini. Kumuuliza akanambia hana mpango, na kama unavyonijua kuambiwa vile nikaanza kuuliza mwaswali na katika maswali hayo nahisi nilimkera. Maana alichukia na kunambia niachane na hizo mada kwa bahati mbaya sikutaka kuelewa nikaendelea kutaka kujua muafaka wa mahusiano yetu.Ndo kwenye kujibizana pale akanambia hayuko na mimi kwasababu anataka kunioa no ila yupo kwasababu anataka kuenjoy maisha. Na akasema kama ninahitaji ndoa basi natakiwa kuwa mvumilivu hadi pale akili yake itakapo amua laa tuachane , kusikia hivyo mtoto wakike nikashuka. Kwa heshima zote nikamuomba samahani na kuandaa chai lakini aligoma akadai anaondoka , nami sikutaka kumkwaza nikamuacha akaondoka. Na baada ya kuondoka jioni akanitumia ujumbe kuwa anaona hawezi kuendelea anahitaji tuachane.Nililia na kumpigia sm lakini hakupokea, mwisho akatuma pesa na kusema nitumie kama fidia ya mda alionitumia" "Eeeh kwa hiyo kila kitu ndo kikaisha hivyo ?" "Yeah ,ameenda " "Na ulijaribu labda kumtafuta tena huenda aliongea au kufanya hivyo kwa hasira?" Nilitaka kumjibu ila kabla sijajibu nilikatishwa na sauti iliyokuwa ikitokea mlangoni, wote tuligeuka kuangalia ni nani alie ingiaA.......... ...???????? Nyieeeee....Mambo ni ya motooo.???? Kwani wewe auogopi Usipite bila kulike na kukomeniti fanya ku share kabisa ili sehemu inayofuata isikukose maana ndiyo sehemu balaaa????????????????????????????????
..ITAENDELEA...... Hii ni bonge la simulizi isikubali ikupite.
@wafuasi
#itaendelea_story_ni_kali_sana?
Mkiwa wavivu kucoment namimi nakuwa mvivu kupost hivyo comment kwa wingi jamani ili mnie mizuka
# PIA USISAHAU KUNI FOLLOW MIMI KULUTI MC ILI USIWE UNAPITWA NA STORY ZANGU FAIDA YA KUNI FOLLOW NI KUWA WA KWANZA KUPATA STORY KILA NINAPO POST
@everyone.