πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 14 ENDELEA. "Ni swali gani hili? mbona nashindwa kuelewa " Bryant Kobe
"Acha bhangi ni kama umeanza kuwa mizizi ya bhangi na hata unajisahau "
"Nieleweshe, kwanini umenitoa nilipokuwa nimekaa na ukaamua kunileta hapa "
"Ni kweli hujui kwanini umeletwa hapa"
"Ningekuwa najua sababu iliyonifanya niwe hapa hata nisinge kuuliza maswali yasiyo na majibu "
Tasha alimsogelea taratibu Bryant Kobe kisha akamuweka denda la maana.
Walijikuta wakibadilishana mate, si unajua tena kipepo cha uzinzi kinavyo kuwaga na nguvu.
Bryant Kobe ndio kushtuka baada ya kuona anashikwa shikwa kwenye nyeti zake.
"Kuanzia sasa na kuendelea hatuta fanya hivi tena wala kushikana shikana ...." Bryant Kobe aliongea kisha akaondoka.
Tasha aliishia kushika moyo wake, hakuelewa ni kitu gani Mwanaume huyu kamaanisha, ile anataka kumkimbilia alidakwa mkono wake kwa kutulizwa kifuani na Philips Kobe.
"Hayupo sawa, akikaa sawa nadhani mtazungumza "
"Siku nyingine naomba usirudie kuingilia mambo yasiyo kuhusu..... kitendo cha kunishika mkono umenipunguzia mwendo, niache nimfuate mpaka kieleweke " Tasha aliongea kisha akamfuata Bryant Kobe.
Alimuangaza kwa macho huku na kule lakini hakumuona, namba yake ya simu si anayo bhana aliamua kumpigia. Simu iliita na kuita tena lakini haikupokelewa kabisa, mwisho kabisa iliacha kupatikana.
Bryant Kobe alikuwa zake chumbani kwake akiachambua nguo, alihitaji kusafiri kimya kimya. Kitu pekee kilichokuwa kina mzuia kusafiri ni Kampuni la Danone.
Kwa sasa halimpi mashaka kwa sababu ameshaambiwa amkabidhi Philips Kobe.
Anaamua kupitia geti la nyuma, aliiwahi ndege iliyokuwa inaondoka saa mbili za usiku.
Hatimaye sherehe ya birthday ya Zara ilikamikika, watu walianza kutawanyika mmoja baada ya mwingine.
Philips Kobe anaingia chumbani kwa Kaka yake, kwa jinsi mazingira yalivyokaa tu aligundua Bryant Kobe kaondoka.
Alishika simu akaanza kumpigia lakini hakupatikana.
Alikumbuka kutumia namba ya siri aliyowahi kumpatia
"Mb....wa wewe umeelekea wapi usiku huu "
"Nahitaji kubadilisha mazingira kwa muda, hakikisha Kampuni linakaa katika hali nzuri....na kubwa kuliko yote usimfanyie kiburi Mama yako " Bryant Kobe aliongea kisha akakata simu.
Anaamua kuingia Tiktok aone kuna jipya gani.
Alikuwa na kama siku nne hivi bila kuingia mtandaoni.
"Mwanaume ule kwa jasho Mwanamke uzae kwa uchungu hii inajulikana kwa kila mtu, ila cha ajabu siku hizi Mwanamke ndio ana kula kwa jasho na kuzaa kwa uchungu unadhani tuta waheshimu nyie Wanaume na huku mmeyakimbia majukumu yenu " Bryant alijikuta akiachia sonyo kwa mafundisho ya Tasha.
Kulivyo pambazuka asubuhi Zara aliingia chumbani kwa Philips Kobe bila hodi, alimfuma akimalizia kupiga nyeto.
"Kimbwa wewe fanya haraka kuoga uende ofisini.... Kaka yako kaamua kupumzika, ni muda wa wewe kutamba sasa " Zara aliongea kisha akaondoka.
Philips Kobe hakujibu chochote, alijitahidi kadri ya uwezo kumalizia kazi yake kisha akaingia bafuni kuoga.
Baada ya kumaliza alivaa suti akaelekea ofisini, minong'ono ya hapa na pale ilisikika.
Hakujali zaidi ya kunyanyua kichwa chake juu.
Anaingia ofisini kwa kujiamini, anashangaa baada ya kumuona Tasha.
"Yupo hapa kuonana na wewe" Secretary Annie aliongea akihisi ni Bryant Kobe, anashtuka baada ya kujua ni Philips Kobe.
"Bryant Kobe kasafiri sijui atarudi lakini atarudi, kama una shida yoyote zungumza kwangu" Philips Kobe alimuambia Tasha kisha akakaa kwenye kiti.
Acha Tasha akodoe macho kama ameambiwa mambo ya msiba.
ITAENDELEA.......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi