πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 9 ENDELEA...... "Poleee " Philips na Bryant Kobe waliongea kipamoja
"Pole ? ni heri niibiwe lakini si kuanguka. Kampuni kubwa kama hili ni aibu kuwa na visiki " Tasha aliongea kisha akaichomoa mikono yake kwa Wanaume hawa kisha akasimama vizuri.
"Karibu, bila shaka uko hapa kurudisha majibu ya ujumbe uliotumiwa " Bryant Kobe aliongea akionesha tabasamu.
"Kapatwa na nini leo hata anioneshe uso wa tabasamu " Tasha alijiuliza ndani ya moyo wake huku akisita kupiga hatua.
"Nifuate ofisini " Bryant Kobe aliongea kisha akaongoza njia.
Ile Tasha anataka kupiga hatua Philips Kobe alimdaka mkono
"Samahani "
"Bila samahani "
"Nimevutiwa na wewe, naomba unipatie namba yako " Philips Kobe aliongea kwa sauti ya kunong'ona.
Tasha hakuwa na choyo, alizama kwenye pochi yake akampatia business card.
"Kwaheri " Alizungumza kisha akamuwahi Bryant Kobe.
Kwa pamoja walipanda lifti, vile kulikuwa na kioo sasa Tasha hakujizuia kujitazama.
Lifti ilicheza kidogo wakajipata wameegemeana.
"Samahani...." Tasha alijiwahi.
"Samahani?....kwani wewe ndio umeitikisa lifti "
Tasha hakujua hata asemeje kwa jibu kavu alilopatiwa.
Basi kwa pamoja waliingia ofisini baada lifti kufunguka.
"Nipatie mkataba nadhani kesho nitaingia studio kutengeneza tangazo" Tasha aliongea huku akiachia tabasamu.
Mkataba uliletwa mezani, aliupitia chapu chapu kama robot hivi.
"Naomba kuongezewa pesa kwa sababu nina uhakika pindi tangazo langu litakapo ingia sokoni maji ya kunywa aina ya Volvic yatauzika sana "
"Una uhakika wa asilimia ngapi katika hili kwanini tusiongezeke pesa baada ya kazi kuanza kuzaa matunda!"
"Najiamini kupita kiasi na ndio maana na zungumza hivi" Tasha aliongea akiwa kamkazia macho Bryant Kobe.
Mmmmmmh ghafla tu walijikuta wametazamana, hakuna aliyekuwa tayari kuona aibu. Hivyo waliendelea kuangaliana.
"Ngoja nione kama utaendelea kunitazama hivi " Tasha aliongea kisha akalegeza macho yake, yalikuwa ni yale macho ya kichokozi.
Bado Bryant Kobe aliendelea kushikiria msimamo wake wa kukaza macho.
"Nitakukomoa " Tasha alijisemea ndani ya moyo kisha akaweka macho ya makengeza, lilikuwa ni kengeza la kutisha asikuambie mtu.
"Achaaaaa wee mchawi nini " Bryant Kobe aliongea akionekana kuogopa.
π π π Ilikuwa ni burudani kwa Tasha...
Secretary Annie aliingia akiwa kabeba chupa ya chai pamoja na vitafuno.
Si alijitia hatishwi na uzuri wa Tasha basi acha avute mdomo hata asitoe salamu.
"Karibu chai CEO....." Aliongea kwa sauti ya kuremba.
Bryant Kobe alishindwa kuelewa kulikoni kuhusu sauti inayotoka kwa Secretary wake.
"Ongeza kikombe cha pili pamoja na vitafuno tuna Mgeni, tena ni yule uliyesema anafaa kuwa modo kwenye tangazo la maji ya Volvic" Bryant Kobe aliongea.
"Sawa " Annie aliachia tabasamu na makasiriko hapo hapo.
"Nipo kwenye mfungo sihitaji chai...kama umeridhia ombi langu naomba nidondoshe saini yangu nisepe " Tasha aliongea.
Bryant Kobe hakuwa na noma alimpatia mkataba.
"Sijaja na gari naomba kusaidiwa usafiri β" Tasha aliomba.
"Secretary Annie mmpeleke Mgeni wetu...." Bryant Kobe alitoa amri.
Ile Tasha anataka kuondoka alidakwa mkono.
"Nipatie namba yako, kuanzia sasa na kuendelea tutakuwa tuna wasiliana"
Basi Tasha alizama kwenye pochi yake akatoa business card. Waliagana kisha akaendelea na safari yake.
Kwa jinsi Secretary Annie alivyo fungua mlango wa gari kwa hasira ilimfanya Tasha atetemeke.
"Hebu kaendelee tu na kazi yako nitapanda bajaji "
"Ahsante kwa kujiongeza mfundisha pumba Tiktok " Secretary Annie alijikuta akimchukia ghafla tu.
"Vipi una hofia Bryant Kobe ataosha vyombo na kupiga deki pindi atakapo jaribu kunipenda au unahisi wivu usioeleweka kisa na maana nimechaguliwa kuwa promota wa bidhaa ya Kampuni lenu ?....acha wivu haupendezei kabisa Mwanamke " Tasha aliongea kisha akaondoka.
Wakati yote yanaendelea, Bryant Kobe alikiwa dirishani akimfuatilia kwa ukaribu.
Moyo wake ulizidi kuridhia kuwa Binti huyu ni mrembo kuliko Wanawake wote aliowahi kuwaona π tamaa ya kumpata ilimuijia.
Baada ya masaa ya kazi naomba tupate dinner " Ujumbe kutoka kwa Bryant Kobe uliingia kwenye simu ya Tasha.
Hajakaa sawa ujumbe kutoka kwa Philips Kobe uliingia.
Naomba tupate dinner baada ya masaa ya kazi.
"Mb.. wa hawa. itanilazimu nipike chakula waje kula nyumbani kwetu" Tasha alijisemea kisha akaingia kwenye bajaji.
Upande mwingine baada ya masaa ya kazi kuisha, Zara aliwakalisha watoto wake sebuleni.
"Naomba mvae kupendeza tumealikwa kupata chakula cha usiku nyumbani kwao Tasha.... narudia kusema naomba wote mpendeze hasa hasa wewe Philips Kobe itanilazimu niingie chumbani kwako ni kuchagulie nguo " Zara aliongea.
Bryant Kobe na Philips Kobe walishindwa kuelewa kwanini Tasha kafanya hivi.
ITAENDELEA......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi