πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π SEHEMU YA 17 ENDELEA...... "Mama yako alimuua Mama yake Bryant Kobe
"Una uhakika na maneno unayo zungumza?"
"Siwezi kuongea uongo, yaani kwa umri wangu huu siwezi kuzungumza vitu vya uongo....." Dada wa kazi mstaafu aliongea.
"Ahsante kwa kuniambia ukweli, shika hii itakusaidia kukuwekea Ulinzi " Philips Kobe alimuachia bastola Dada wa kazi mstaafu kisha akaondoka.
Mara nyingi akiwa mpweke huwa anapenda kunywa pombe.
Aliingia katika Casino moja matata akaagiza pombe, muonekano wake wa kitajiri uliwavuta wadada warembo, walimzunguka kama Kuku na vifaranga wake.
Ulikuwa ni mwendo wa kulewa tu, anakuja kushtuka asubuhi akiwa kalala kitandani na mabinti watatu ......kichwa chake kilikuwa kinamuuma sababu ya pombe.
"Hello CEO, unaweza kufika ofisini haraka kuna changamoto" Secretary Annie alimpigia simu.
"Mpigie Bryant Kobe, kichwa changu hakipo sawa" Philips Kobe aliongea kisha akazima simu kabisa siyo kukata.
"Mji...nga huyu " Secretary Annie aliongea pekee yake baada ya kupiga simu mara ya pili akaambiwa haipatikani.
Akiwa katika kuchanganyikiwa mlango ulifunguliwa, aliachia tabasamu pana baada ya kumuona Bryant Kobe.
"Kuna nini mbona Wafanyakazi wengi wamesimama nje badala ya kuendelea na kazi"
"Taarifa ya miezi sita niliyompatia Philips Kobe kuhusu Wafanyakazi wote aliikosoa sana na hata akaona wanastahili kukatwa asilimia 7 kwenye mishahara yao... kitu hiki kimewakwaza sana ndio maana wapo hapo nje "
"Wapatie taarifa hakutakuwa na maamuzi mengine tofauti na hayo yaliyotolewa, mtu yoyote asiye ridhia haya maamuzi aandike barua ya kuacha kazi na hata hivyo kutakuwa na mabadiliko mengi kuanzia sasa" Bryant Kobe aliongea kisha akakaa kwenye kiti.
Alifanya majukumu yake kama kawaida baada ya kuhakikisha amefikia malengo aliingia kwenye gari lake akaenda kumfuata Philips Kobe. Japo hakuwa amempatia taarifa wapi yupo lakini alikuwa na uhakika wa kumpata.
Warembo wakiwa bize kuchezea kifua cha Philips Kobe walishtuka baada ya kumuona Bryant Kobe.
"Naomba muondoke hapa haraka iwezekanavyo " Aliwafokea.
"Hatuwezi kuondoka bila kulipwa pesa, kwa usiku mzima tumempa company hapa " Mmoja wa warembo alizungumza.
Bryant Kobe hakutaka kusumbuana nao, alijishika mfukoni kisha akapatia dola.
"Ni kama unatukomoa hivi, hizi dola tunaenda kubadilisha wapi " Mrembo mwingine alifoka.
Bryant Kobe hakutaka kusumbuka nao, alifungua mlango kisha akawatoa nje.... wengine hawakuwa hata wamevaa vizuri, aliwarushia chupi zao pamoja na vinguo vyao.
"Nadhani mara ya mwisho tulikumbushana hamna kuelewa hovyo..... vipi kama hawa wahuni wamekurekodi namna mlivyo kuwa mnakula bata si utatia aibu huko mtandaoni " Bryant Kobe aliongea.
Acha Philips Kobe aangue kilio, moyo wake ulikuwa na uchungu sana imgawa hakuweza kusema chochote lakini alihuzunika.
"Sitakuuliza shida ni nini, naomba twende nyumbani" Bryant Kobe aliongea kisha akambeba mdogo wake....
Alimuingiza kwenye gari kisha safari ya kwenda nyumbani ilianza.
Zara akiwa ana mwagilia bustani alishangaa baada ya kuwaona Vijana wake wawili.
"Kitu gani kinaendelea " Alijisemea kisha akamsogelea Philips Kobe, alimnusa pua zake akagundua amelewa.
"Nipo na kazi zangu hapa, mnaweza kuingia ndani tutazungumza baadae ..." Zara aliongea akijitia hajaona chochote cha maajabu.
Kitendo cha watoto wake kuingia ndani, alifunga bomba.
"Bila shaka Dada wa kazi mstaafu atakuwa amezungumza na Philips Kobe....nina uhakika kuna kitu atakuwa kamuambia " Zara alijisemea kisha akaelekea chumbani kwake alihitaji kuonana naye.
Baada ya kuhakikisha amemaliza kuvaa, alichukua bastola akaweka ndani ya mkoba wake.
Upande mwingine Tasha akiwa ana safisha chumba chake alidondoka sababu ya kizungu zungu kisichojulikana kimesababishwa na nini.
ITAENDELEA......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi