*MKAKA KAUZU HUYU JAMANI* 🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺🥺 *6-10* *__________________________________________* *SEHEMU YA SITA* Frank alikuwa na wasiwasi usio wa kawaida
"Anaya, usille sasa si unaona watu wamejaa mlangoni hapo jamani"
Alizungumza frank akiwa na wasiwasi sana, akiangalia na mazingira ya ofisi yalivyokuwa ndio kabisa, Yaani ofisi ilikuwa vuluvułu kwaajili ya mechi yetu ya kipuuzi.
"Vas Bası"
Alizungumza frank uku akinisaidia kuvaa baada ya yeye kumaliza kuvaa.
Baada ya kila kitu Kuwa Sawa na frank kupulizia air freshener polepole Frank akafungua mlango. na wafanyakazi pamoja na baba frank na flora wakaingia wakiwa na wasiwasi sana,
"Kuna nini?"
Flora aliuliza akiwa na wasiwasi sana, si unajua Tena mambo ya bff, Yaani huyu dada alitokea kunipenda sana na Mimi nilimpenda pia.
"Anaya amepata miscarriage alikuwa anajiweka Sawa ili nimuwaishe hospital"
Alizungumza frank Tena alidanganya uongo ambao ata Mimi ulinishtua sana kwakweli miscarriage ya gani Tena jamani wakati mtu Ametoka kuvunja kuta Tena Wala hakuwa amenionea huruma Mtoto wa mwenzie.
Kila mtu alijikuta akinionea huruma sana na kunipa pole za kila aina, kwa haraka flora na frank wakasaidizana kwaajili ya kunipeleka hospital kwaajili ya kwenda kusafishwa.
Nilipelekwa kwenye hospital ambayo flora na frank walionekana kujulikana sana na aswaah aswaah frank, Sijui Frank alishawasiliana na mtu maana nilipokelewa na kupelekwa kwenye chumba cha emergency.
"Mimi siumwi dokta"
Niliamua kujitetea maana kwa muda huo ni Mimi tu na dokta ndio tulikuwepo umo
"Najua usijali, frank ameniambia kila kitu, so usijali tutakaa kwa muda wa Lisaa moja tu kisha nakupeleka kwenye Wodi ya mapumziko na baadae nitakuruhusu kwenda Nyumbani"
Nilijikuta nikimkodolea macho huyo dokta uku Nilijiuliza amelipwa kiasi gani mpaka kufanya kazi kubwa kiasi hiki? Frank alifanya yote haya
ili kumuaminisha kila mtu Kuwa nimepata miscarriage na watu wasiweze kujua ni kitu gani kilitokea.
Baada ya muda nikatolewa kwenye chumba cha emergency na kupelekwa kwenye wodi ya kawaida.
"Unaendeleaje?"
Frank aliniuliza baada ya kubaki Mimi na yeye kwenye chumba cha hospital.
"Umeniumiza sana, naumia mpaka muda huu"
Nilizungumza kwa kudeka nikiamini Kuwa Frank atanionea huruma na Kuwa Mpole mbele yangu, lakini ilikuwa tofauti sana kwani Frank akaanza kunifokea.
"Uliyataka Mwenyewe lakini, hivi Anaya hivi wewe ndio hauna akili kiasi hiko? Yaani kukushika kidogo tu ukaamua kujiachia Mwenyewe Kama uko na mwanaume wako si ndio? Anaya Mimi ni mwanaume nikipata mwanamke ajiheshimu Kama wewe Basi
ninachokifanya ni kupita tu, yaaani shwwaaah, Kwahiyo wewe kwangu umekuwa Kama Mbuzi tu aliyefia kwa muuza Supu"
Nyieeeeh nilijikuta nikijisikia vibaya sana, Yaani
Sawa nilishadhalilika kwa vitendo lakini bado Frank ameamua kuniambia kabisa kwa kinywa chake, nilibaki nikimuangalia tu frank uku machozi yakinitililika.
"Naomba niende Nyumbani tu
Nilizungumza uku nikitaka kunyanyuka kutoka kitandani..
"Acha ujinga wako wewe, unajua flora ameendal kukuchukulia uji upate kunywa "
Nilimuangalia frank kisha kwa hasira nikajibu.
"Kama uliweza kudanganya mwanzo na kila mtu aka kuamini, sizani Kama utashindwa kudanganya kwa wakati huu"
Nilimyanyuka zangu kisha huyo nikaondoka zangu nikiwa na maumivu ya mwili lakini pia na maumivu ya moyo baada ya kupewa maneno makali sana na frank
Nilitoka nje na pasi na kupoteza muda nikatafuta usafiri na kuondoka zangu.
KWa upande wa kazini kila mtu aliamini uongo ambao aliutoa frank hivyo boss wangu akanipatia mwezi mzima wa kujiangalizia Nyumbani, naweza nikasema Kuwa ilikuwa ni
kitu kizuri sana kwa upande wangu kwaajili ya kuweka akili yangu Sawa lakini pia kuepuka aibu kubwa ya Kuwa Karibu na frank.
Hatimaye likizo yangu iliisha lakini bado nilijikuta nikiwa na wasiwasi sana wa kwenda kazini, Yaani nilijikuta nikitaka tu kuacha kazi kabisa.
"Anaya Mdogo wangu, yaliyotokea yameshatokea na uwezi kupingana na ukweli, wewe kuacha kazi sio solution kabisa Sawa?
Unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kufocus na kazi yako, huyo frank Sijui Nani Nani Wala asikutibue akili yako na hayo maneno yake ya kipuuzi Sawa Mdogo wangu ?"
Alizungumza dada yangu ambaye kwangu alikuwa ndio kila kitu na mambo Mengi. Nimekuwa nikimshirikisha pasi na kumficha ata kitu kimoja.
Hatimaye siku ambayo niliitajika kwenda kazini, niliamua kusikiliza ushauri wa dada yangu na pasi na kuona aibu nikarudi zangu kazini nikiwa ni mtu Mpya kabisa..
Sio kwamba niliacha kumpenda frank hapana lakini niliona Kuwa ni mtu ambaye anifai na kilchotokea ilikuwa ni ujinga wangu tu
Aaah kitu ambacho sikuwaambia ni kwamba, kipindi ambacho nilikuwa likizo, frank amekuwa akinipigia simu na kunitumia sms lakini sikuwa Nikijibu Wala kupokea simu zake.
KWa upande wa wazazi wangu niliwadanganya Kuwa mwezi huo ofisi yetu ilikuwa na shidal hivyo kazi tunafanyia Nyumbania.
Flora alifurahi sana kuniona ofisini kwa Mara nyingine Tena, wafanyakazi wenzangu pia walifurahi sana, moja kwa moja nikanyoosha njia na kwenda ofisini kwangu ambapo. nilikutana na frank akiendelea na kazi,
Ule msemo wa ukistaajabu ya musa utayaona ya filauni ndio huu sasa, Yaani Frank kitendo cha kuniona tu alijikuta akifurahi sana na kwa bashasha akanyanyuka na kunikumbatia kWa nguvu sana nika.....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni