🔞 Onyo: Hadithi hii ina maudhui ya watu wazima, vurugu za kifamilia, na hisia nzito. Inafaa kwa wasomaji waliotimia miaka 18+. Tafadhali soma kwa tahadhari. 🔞 Hadithi ya Watu Wazima : Zawadi Sehemu ya 7
Simulizi za john
0789 824 178 ,
1000
Nikasema, “Mama, hakuna chochote, baba alikuwa anaangalia vidonda tu.” Akasema, “Unasemaje? Baba? Baba gani? Babako yule? Unamudu ili unibadilishe uishi kwenye ghorofa hii, si ndiyo? Unaona ninafaidi, unataka kuwa mke mwenza, si ndiyo? Ulimuonyesha nini huko chini?” Nikasema, “Mama, mbona unaniambia maneno ambayo sielewi? Unanionea!” Akasema, “Nani anakunea?” Alinishika, akanibamiza ukutani, akasema, “Nitakuua!” Nilipasuka kichwani kisogoni, damu zikamwagika. Mama hakustuka, akaendelea kunipiga, kisha akasema, “Toka kwangu, toka!” Akanisukuma nje huku navuja damu, nalia, bila kusema nisamehe—nilishaamua kuondoka, bora nikafie mbali.
Nikimkumbuka mama na bibi yangu, nilitamani kurudi, lakini baba yangu ni mkatili, ataniua. Nje ya nyumba kuna kibaraza chenye ngazi, akanisukuma, nikabiringika kama mzigo, nikatua chini. Masai aliona, akaja akikimbia, lakini mama aliniokota, akaanza kunipiga tena, akisema, “Ondoka kwangu, mshenzi!” Nikaskia sauti, “Mama Zawadi, mshenzi wewe, mwache mtoto wa watu!” Alikuwa Baba Zawadi. Masai alinishika, nikiwa navuja damu puani na mdomoni, bila nguvu. Baba akasema, “Masai, kampakie kwenye gari haraka! Na wewe, mwanamke mkatili, nikirudi nisikukute—una roho mbaya kama paka!”
Masai alinibeba, nikatolewa nje ya geti kwenye gari la baba. Baba alipanda, akasema, “Masai, hakikisha nikirudi simkuti yule mwanamke, nitamuua!” Aliwasha gari. Nakohoa damu, baba akaogopa, akasema, “Zawadi, nakupeleka hospitali, sawa?” Sikuweza kusema. Alipita kwa polisi, akachukua karatasi, tukafika hospitali. Alinibeba, akipiga kelele, “Nesi, daktari, nisaidieni mtoto huyu!” Walinipokea, nikawekwa kwenye kitanda cha emergensi. Nilitibiwa, lakini sikusikia maumivu, kama sielewi kinachoendelea. Nilipopewa dawa, nikapitiwa na usingizi.
Niliamka niko kitandani, bila nguo, nimefunikwa shuka. Nikajiona niko hospitali, chumbani chenye vitanda vinne, lakini hakuna mtu. Nilianza kukumbuka yaliyonipata, machozi yakanitoka. Nesi akaja, akasema, “Muda wa dawa, binti mzuri, umeamka?” Nikasema, “Ndiyo.” Akasema, “Unajisikiaje?” Nikasema, “Nafuu.” Akasema, “Kakako anakuja, yupo njiani.” Nikashangaa, “Kakangu gani?” Nikauliza, “Kaka?” Akasema, “Yule aliyekuleta, kwani sio kakako? Si babako, bado mdogo.” Nikajua ni Baba Zawadi. Nikakaa kimya. Alinipa dawa, nikanywa, drip liliisha, akaweka lingine, akatoka.
Nikiwa na mawazo, “Mama akirudi, itakuwaje? Bora nitoroke.” Nilitamani kumtafuta Neema, lakini sikuwa na mawasiliano naye. Nikapanga kutoroka nikipata nafasi. Nikiwa nimelala, Baba Zawadi akaniita, “Zawadi!” Nikaitika, “Abee,” nikafumbua macho. Akasema, “Unajisikiaje?” Nikasema, “Naendelea vizuri.” Akasema, “Pole sana.” Nikasema, “Asante, baba.” Akasema, “Nimekuletea nguo uvae, ile ilichafuka, ilitupwa.” Nikasema, “Baba, asante, lakini nitaifua.” Niliongea nalia.
Baba alinishika, akasema, “Zawadi, naomba unisamehe kwa yaliokufanyia mke wangu. Alikufanyia kitu cha kinyama. Nitafanya kila kitu kwa ajili yako, nitakupa chochote unachotaka. Nina watoto, nawaza kama sipo, wataishije? Nisamehe, nitakulea kama mwanangu.” Nikasema, “Baba, naogopa, siwezi kurudi, yule mama ataniua.” Akasema, “Hayupo, hatorudi kabisa kwangu. Uwe na amani, nitakusaidia, nitatafuta msichana wa kazi, sawa? Naomba unipe muda.” Nikasema, “Mmmh, nifanyaje? Nimepigwa hadi nakohoa damu, safari hii ataniua. Je, ni kweli hatorudi?” Nikawaza, “Nikubali au iwaje?” Itaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni