Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

πŸ”ž Onyo: Hadithi hii ina maudhui ya watu wazima, vurugu za kifamilia, na hisia nzito. Inafaa kwa wasomaji waliotimia miaka 18+. Tafadhali soma kwa tahadhari. πŸ”ž Hadithi ya Watu Wazima : Zawadi Sehemu ya 7

31st Jul, 2025 Views 57


Simulizi za john
0789 824 178 ,
1000
Nikasema, β€œMama, hakuna chochote, baba alikuwa anaangalia vidonda tu.” Akasema, β€œUnasemaje? Baba? Baba gani? Babako yule? Unamudu ili unibadilishe uishi kwenye ghorofa hii, si ndiyo? Unaona ninafaidi, unataka kuwa mke mwenza, si ndiyo? Ulimuonyesha nini huko chini?” Nikasema, β€œMama, mbona unaniambia maneno ambayo sielewi? Unanionea!” Akasema, β€œNani anakunea?” Alinishika, akanibamiza ukutani, akasema, β€œNitakuua!” Nilipasuka kichwani kisogoni, damu zikamwagika. Mama hakustuka, akaendelea kunipiga, kisha akasema, β€œToka kwangu, toka!” Akanisukuma nje huku navuja damu, nalia, bila kusema nisameheβ€”nilishaamua kuondoka, bora nikafie mbali.
Nikimkumbuka mama na bibi yangu, nilitamani kurudi, lakini baba yangu ni mkatili, ataniua. Nje ya nyumba kuna kibaraza chenye ngazi, akanisukuma, nikabiringika kama mzigo, nikatua chini. Masai aliona, akaja akikimbia, lakini mama aliniokota, akaanza kunipiga tena, akisema, β€œOndoka kwangu, mshenzi!” Nikaskia sauti, β€œMama Zawadi, mshenzi wewe, mwache mtoto wa watu!” Alikuwa Baba Zawadi. Masai alinishika, nikiwa navuja damu puani na mdomoni, bila nguvu. Baba akasema, β€œMasai, kampakie kwenye gari haraka! Na wewe, mwanamke mkatili, nikirudi nisikukuteβ€”una roho mbaya kama paka!”
Masai alinibeba, nikatolewa nje ya geti kwenye gari la baba. Baba alipanda, akasema, β€œMasai, hakikisha nikirudi simkuti yule mwanamke, nitamuua!” Aliwasha gari. Nakohoa damu, baba akaogopa, akasema, β€œZawadi, nakupeleka hospitali, sawa?” Sikuweza kusema. Alipita kwa polisi, akachukua karatasi, tukafika hospitali. Alinibeba, akipiga kelele, β€œNesi, daktari, nisaidieni mtoto huyu!” Walinipokea, nikawekwa kwenye kitanda cha emergensi. Nilitibiwa, lakini sikusikia maumivu, kama sielewi kinachoendelea. Nilipopewa dawa, nikapitiwa na usingizi.
Niliamka niko kitandani, bila nguo, nimefunikwa shuka. Nikajiona niko hospitali, chumbani chenye vitanda vinne, lakini hakuna mtu. Nilianza kukumbuka yaliyonipata, machozi yakanitoka. Nesi akaja, akasema, β€œMuda wa dawa, binti mzuri, umeamka?” Nikasema, β€œNdiyo.” Akasema, β€œUnajisikiaje?” Nikasema, β€œNafuu.” Akasema, β€œKakako anakuja, yupo njiani.” Nikashangaa, β€œKakangu gani?” Nikauliza, β€œKaka?” Akasema, β€œYule aliyekuleta, kwani sio kakako? Si babako, bado mdogo.” Nikajua ni Baba Zawadi. Nikakaa kimya. Alinipa dawa, nikanywa, drip liliisha, akaweka lingine, akatoka.
Nikiwa na mawazo, β€œMama akirudi, itakuwaje? Bora nitoroke.” Nilitamani kumtafuta Neema, lakini sikuwa na mawasiliano naye. Nikapanga kutoroka nikipata nafasi. Nikiwa nimelala, Baba Zawadi akaniita, β€œZawadi!” Nikaitika, β€œAbee,” nikafumbua macho. Akasema, β€œUnajisikiaje?” Nikasema, β€œNaendelea vizuri.” Akasema, β€œPole sana.” Nikasema, β€œAsante, baba.” Akasema, β€œNimekuletea nguo uvae, ile ilichafuka, ilitupwa.” Nikasema, β€œBaba, asante, lakini nitaifua.” Niliongea nalia.
Baba alinishika, akasema, β€œZawadi, naomba unisamehe kwa yaliokufanyia mke wangu. Alikufanyia kitu cha kinyama. Nitafanya kila kitu kwa ajili yako, nitakupa chochote unachotaka. Nina watoto, nawaza kama sipo, wataishije? Nisamehe, nitakulea kama mwanangu.” Nikasema, β€œBaba, naogopa, siwezi kurudi, yule mama ataniua.” Akasema, β€œHayupo, hatorudi kabisa kwangu. Uwe na amani, nitakusaidia, nitatafuta msichana wa kazi, sawa? Naomba unipe muda.” Nikasema, β€œMmmh, nifanyaje? Nimepigwa hadi nakohoa damu, safari hii ataniua. Je, ni kweli hatorudi?” Nikawaza, β€œNikubali au iwaje?” Itaendelea.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

πŸ”ž Onyo: Hadithi hii ina maudhui ya watu wazima, vurugu za kifamilia, na hisia nzito. Inafaa kwa wasomaji waliotimia miaka 18+. Tafadhali soma kwa tahadhari. πŸ”ž Hadithi ya Watu Wazima : Zawadi Sehemu ya 7  >>> https://gonga94.com/semajambo/onyo-hadithi-hii-ina-maudhui-ya-watu-wazima-vurugu-za-kifamilia-na-hisia-nzito-inafaa-kwa-wasomaji-w
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest