AAAAH IMETOSHA BOSSππ N0 68...69ππ
Ni nani jina la huyo mwanamke aliyejifungua?! Nilimuuliza eve aliniambia jina lake ni lia Stanley.... lia lia lia...... kwanini huachi ndoa yangu ikawa na amani nikufanyie nini ewe mwanamke ili uweze kukaa mbali na mme wangu?! Kwanini hukomi.... natakiwa kufanya nini ili kumkomesha huyu binti kama ni matusi tushatukanana sana....kama ni kupigana tushapigana niliwahi kumng'ata hadi kwenye makalio yake sababu ni hiyohiyo kumganda mme wangu lakini mbona haachi..... nimtumie vibaka wampoteze?! Au nimtumie mtu wa karibu yake amtilie hata sumu kwenye chakula ale afeππ au nimtumie nurse eve nitamlipa ili amchome lia sindano yenye sumu ili aweze kupoteza maisha....siwezi kumuacha mme wangu siko tyr kuanzisha mahusiano mapya......nitadiri naww lia na nitakufunza namna ya kuheshimu ndoa za watu....hivi ni kweli nimedhamiria kutaka kumuuaπ€π€ duh vipi kama mzimu wake ukiwa unanitokea na kunisumbua si nitaishi kwa wasiwasi sanaπ€¨π€¨ ila nahisi kinachomchanganya lia ni mapenzi.... upendo alionao kwa mme wangu ndo kitu kinachomfanya ashindwe kabisa kumove on..... nitamsaidieje sasa ili aweze kutambua kuwa paschal ni mme wangu na haipo siku ambayo yeye atakuwa wake......
Kiukweli niliwaza sana siku ile..... nilifikia uamuzi wa kwamba nijiandae niende kule hospital waliko niende nikawaone niliwaza kumuua lia apotee kabisa kwenye uso wa dunia lakini niliona hiyo siyo njia sahihi..... nilijiandaa nikaandaa na chakula baada ya hapo niliondoka kuelekea kule hospitalini....nilimkuta eve aliniongoza hadi sehemu aliko mme wangu.... maskini mme wangu alikuwa kachoka sana alikuwa tu amekaa kwenye viti vya wagonjwa na alipitiwa na usingizi pale nilivyofika pale karibu yake nilimuonea huruma sana ananificha ili kuilinda ndoa yetu nahisi hiyo ndiyo sababu pekee inayomfanya yeye apambane na haya peke yake bila kunihusisha...... nilimsogelea karibu pale nikaketi kwenye kiti cha pembeni yake nilimgusa began zaidi ya mara tatu lakini hakushtuka nilimuacha alale kwanza niliomba kwenda kumuona lia nurse eve alinipeleka kule alikolazwa lia hakuwa katika hali nzuri tangu alipofanyiwa operation alikuwa hajapata fahamu......
Nilimtizama alipokuwa kalala usingizi mzito sana wala hata alikuwa hajitambui.... kiukweli nilimuonea huruma sana nilifunga macho yangu pale nikamgusa lia mkono wake nilimfanyia maombi nilimuomba mwenyezi mungu amuamshe pale akiwa mzima ili aweze kumuona mtoto wake na kumlea..... niliombaaaa....... nakuomba...... nilimsihi mungu ampe pumzi yule mwanadada lia.... baada ya kumaliza kuomba niliyafuta machozi yangu yani niliomba kwa hisia hadi machozi yakawa yananitirilika ..... mimi ni mama niliyezaa nina watoto nilimuwazia zaidi yule mtoto kichanga aliyemzaa lia niliwaza vile wanangu wanavyokuwa huru kwangu nikamuwazia na yule mtoto mdogo wa lia anahitaji zaidi uwepo wa mama yake...... nilimuomba mwenyezi mungu ampe uzima lia......baada ya kuyafuta machozi yangu niligeuka nyuma nilishangaa kuona paschal akiwa amesimama pale mlangoni na alikuwa anabubujikwa na machozi mengi sana baada ya mimi kumgeukia paschal alipiga magoti chini huku akiwa analia aliniambia naomba unisamehe sana mke wangu kwa kukuficha juu ya hili..... sikutaka kuendelea kuwa pasua kichwa kwa mme wangu pale alipokuwa alikuwa na stress nyingi sana sikutaka kumuongezea stress zingine na hata hivyo nilishaamua kuwa wife material kwake.... nilimfuata nikamuinua pale chini nilimpangusa machozi yake na baada ya hapo nilimkumbatia nikamwambia Acha kulia..... naelewa kila kitu lakini kunificha haikuwa njia sahihi uliyoamua kuichagua..... aliniomba radhi aliniambia jana jioni kipindi nataka kutoka ofsini......
Alinifuata baba yake lia aliniambia kuwa binti yake yuko hospital anapambania uhai wake na wa mtoto aliniomba niambatane naye kwa sababu lia ameomba sana niende nikamuone hospital nilishindwa kukataa niliongozana na baba yake lia hadi huku hospital nilimkuta lia akiwa na hali mbaya sana alikuwa analia na kuniambia kuwa yeye atakufa alitaka tu mimi nije ili aniombe nimulee vyema mtoto atakayemzaa.... kuzaa kwa njia ya kawaida ilishindikana ikabidi afanyiwe operation jana usiku na tangu alipofanyiwa operation hajaweza kuamka hadi mda huu..... ucjali hatokufa ataamka.... nilimtia moyo paschal nilimshikilia mkono hadi nje kule kwenye gari nilimpatia chakula akala hakula chochote tangu jana usiku alikuwa na njaa sana alimaliza kula akanishukuru then kwa pamoja tuliendelea kusubilia majibu ya madactari kuhusiana na hali ya mgonjwa ..... nilipelekwa nikamuona yule mtoto wa lia..... mtoto alikuwa sawa hakuwa na tatizo lolote lile kiafya..... ni wa kiume alifanana sana na paschal π£π£ Kiroho lazima kiume buana duh yani unawaza kabisa hili bao lilipenya lotelote ina maana hawa watu walikulana nyama kwa nyamaπͺπͺ lakini yule ni mtoto huwezi kumhukumu..... paschal hakuacha kuomba radhi kila sekunde nilimuondoa shaka.....
Ilifika hadi jioni lia akiwa hajazinduka kutoka usingizini.... tuliruhusiwa kumchukua yule mtoto tukaondoka naye kwa kuwa yeye hakuwa na shida yoyote..... nilimchukua nikaenda kumhudumia nyumbani kwangu lia katika maisha yake kalelewa na baba tu hapakuwepo na mtu katika familia yao ambaye angemchukua yule mtoto na kwenda kukaa naye.... uzuri ni kwamba kipindi hicho tayari paschal alikuwaga kaishanifungulia ofisi yangu na mimi ndo niliyekuwa boss hiyo ilinifanya nipate muda wa kumhudumia yule mtoto mimi mwenyewe kwa mikono yangu kwa sababu sikuwa na zile heka heka za kuwaza mambo ya kazini kwa sababu nilikuwa nimejiajiri mwenyewe..... usiku mida ya saa nane tulipatiwa taarifa kuwa lia ameamka...... zilikuwa ni taarifa njema kesho yake asubuhi tuliamkia hospital tukampeleka na mtoto ili aweze kupata maziwa ya mama....lia hakuwa katika hali nzuri bado alikuwa hajaweza kuongea kitu chochote kile na hata kupumua alikuwa anapumua kwa mbali sana hali yake ilikuwa inatisha sana..... tiliendelea kuwa tunamtembelea hospital tulikuwa tunampeleka na mtoto kwa ajiri ya kwenda kupata maziwa ya mama.....
Zilipita kama 2 weeks hali ya lia ilianza kutengamaa kwa kiasi Fulani alianza hata kuongea japo kwa tabu sana....aliniomba radhi kwa ubaya aliowahi kunitendea hapo nyuma....asante kwa kunilelea mtoto wangu pendo nakuomba unisamehe kwa ubaya wote niliowahi kukutendea hapo nyuma..... kila siku nilikuwa ni mtu wa kumfuata fuata mmeo japo kila siku alikuwa akinikumbusha kuwa yeye ni mme wa mtu na moyo wake tayari ulishakupenda wewe mke wake sikutaka kukubaliana na uamuzi wake niendelea kumshawishi na kumtega sana tu hadi nikafanikiwa kufanya naye mapenzi nilikuwa natamani akuache ili anioe mimi lakini hiko kitu kilikuwa kigumu sana kwake...... siku niliyoamini kuwa paschal siyo wangu na hawezi kuwa wangu ni ile siku uliyotufumania kule nyumbani kwako paschal alinifukuza mimi na wewe ulibakia..... siku ile ndo niliamini kweli cha mtu huwezi kukimiliki..... sikukata tamaa baada ya siku kupita nilipoanza kuona mabadiriko ya mwili wangu nilikwenda hospital kupima ndipo nilipogundulika kuwa mimi ni mjamzito......
Nilikuwa nikimtafuta paschal bila matumaini simu zangu alikuwaga hapokei kabisa na hata msg zangu alikuwa hajibu....siku niliyokata tamaa juu ya paschal ni ile siku aliyonionya kuhusu kuwa nampigia pigia simu kila muda alithubutu kunipatia namba yako ili nikiwa na shida nikutafute wewe na siyo yeye kiukweli nilijichukia sana mimi nilijua nikiibeba mimba yake inaweza ikamshawishi yeye akanipenda mimi lakini kumbe nilikuwaga najidanganya tu.....mimi nakuomba tu unisamehe najua mimi ndo niliyekuwa sababu ya mvurugano usio kwisha kwenye ndoa yenu..... mmeo anakupenda na mimi nimeliamini hilo....sitaki tena kuwa sababu ya uvunjifu wa amani kwenye ndoa yenu kiukweli natamani kuwaona mkiwa mnaishi kwa furaha..... hali yangu ni kama hivi unavyoniona sijui kama nitapona ila hata nikifa basi nitaenda kwa amani kwa sababu angalau nimeweza kukuomba wewe msamaha kwa usumbufu niliokuwa nikikupatia nawaomba mnilelee mtoto wangu nakuomba unisamehe pendo......
Itaendeleaaaa......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni