MIMI SIKUACHI🥰 SEHEMU YA 58
Wakati nawaza pale akaja yule muuzaji na baadhi ya sampo ya vitu vya kike vya gharama kweli dah mfukoni pesa ya kufosi na uhakika wa kupokelewa zawadi sina ila fresh ngoja nijaribu tu 😄 hata hivo wanaume si tumeumbiwa mateso wacha nijitese tu nilitoa pesa mfukoni nikanunua nguo za ndani vinguo fulani hivi hatari sana Princess akivivaa vile mamae atawaka hatari muhuni nanunua akamvalie mwanaume wake dah lakini kwa vile najipendekeza ili niwe karibu na watoto wangu hakuna namna itabidi nifanye tu basi nilichukua braa za rangi kadhaa pale na vichupi chupi fulani hivi vya kisasa nikafungashiwa nikaondoka zangu mpaka home nimefika tu ndani nikapiga simu kwa mama la mama nimwambie kuhusu mizigo ili akiniruhusu hata mida hiyohiyo niende nikaipeleke..
Nilipiga simu kinoma haipokelewi dah nikaona fresh nikaiacha nikaenda kwanza kuoga nimemaliza kuoga ile natoka tu bafuni nakuta simu inaita Princess huyo anapiga nikaipokea fasta kabla haijakata ikikata naweza nikanuniwa mwaka mzima na watoto nisiwaone🤣🤣🤣🤣🤣kichaa sana yule mwanamke hello naam vipi akasonya vipi ya nini mbona unapiga piga sana simu una shida gani..ah samahani nilitaka tu kuwajulia hali hahahahaaa kutujulia hali hiyo vipi sitaki uzoee zoee kunipigia simu koma kabisa nimekwambia😣😣
Sawa mama nisikilize basi nilichotaka kukwambia ongea haraka niko bize unanipotezea muda.. haya mama nimewachukulia vitu naomba unielekeze mnapokaa nije nivilete..vitu gani na nani kakuomba?? Princess jamani watoto kuna vitu waliomba niwanunulie nimeshavinunua naomba niwaletee..
Uwaletee wapi hivi janaume zima et naomba niwaletee uwaletee kwa nani?? We unajua kodi ya nyumba sh ngapi au unalegeza tu lisauti lako libaya lione ka jinga akakata simu dah nikajicheka kwanza😂😂😂😂sasa hizi chupi nitavaa mimi au🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣nilijiona msenge kinoma ila fresh
Siku ikapita kimya siku ya pili kimya mmmhhh siku ya tatu nikaamua kujipigisha simu hola hapokei ikakata kama wiki bila mawasiliano siku moja usiku akanitafuta akaniuliza ni vitu gani ulitaka kuleta? Nikamtajia tu vile vya watoto akasonya akaniambia kwahiyo hao watoto walijileta wenyewe duniani nikacheka kimoyomoyo kumbe kweli yule mwenye duka aliongea ukweli.eh
Kwamba nikipeleka zawadi za watoto peke yao mama yao atanuna bora hata nilikubali kununua na zawadi za mamtu..ila sikumwambia nilitulia akachamba we badae akaniambia kesho zilete ila usije mpe tu mtu alete na kama ni mavitu ya ovyo atarudi nayo..
Naomba nije mimi pleas nikaongea kiume kwa sauti Fulani hivi mpaka bibie akashindwa kutoa jibu la haraka akakata simu😅😅😅badae akatuma msg subiri nijifikirie dah haya bwana nikatulia huku naomba Mungu nikubaliwe tu kweli..
Hiyo siku akanitafuta akaniambia wako sehemu niende bahati nzuri nilikuwa nyumbani sikutaka kupoteza muda maana nilipewa dakika chache nikichelewa wanaondoka... nilibeba vile vitu nikapakia kwenye gari fasta nikaifuata ile location kwa mbali nikawaona aiseee nilitoa hadi machozi sikuamini..
Nilienda hadi sehemu walipo watoto wakanikimbilia wakanikumbatia kwa furaha sana nikaanza kuwagawia zawadi zao mama yao akawa pembeni tu anaangalia anabenua midomo nakwambia hatari..
Nilicheza na wanangu pale wakahitaji na baadhi ya vitu pale nikawanunulia ilikuwa raha sana haikupita muda mrefu mama yao akaniambia muda umeisha tunatakiwa kuondoka akawakusanya watoto wakawa wananililia dah..
Basi ikabidi nimuombe niwarudishe mimi nyumbani lakini mamtu hataki hata kusikia kanikazia muda huo hata zawadi sijampatia bwana ziko kwenye gari naogopa kinoma maana anaweza akazikataa nikaaibika😅😅😂😂😂
Nilivoona amekaza kuondoka nikawaza mmhh acha tu nimpatie zawadi zake akikataa basi kweli nilienda kwenye gari nikazichukua alafu watoto nikawaambia nendeni kwenye gari tukabaki wawili mimi na mama yao..
Nikajikaza kisenge yani nikamwambia hizi hapa nimekuletea heee hakuamini akajidai kukataa nikambembeleza mpaka akachukua akaanza kuziangalia nani kakwambia uniletee zawadi za hivi kwa sauti Fulani hivi ya kudeka hahahaaaa nikajua hapa fresh twende basi nikupeleke nyumbani lamama🥰🥰🥰🥰
Akakubali ile sitaki nataka tukaenda kwenye gari mzee baba moyoni nachekelea tu nikimwangalia mtoto Princess anazidi tu kuiva kanawili huyo basi alinielekeza wanapokaa nikawapeleka hadi nyumbani na juice nikapewa😂😂😂😂unajua kilichofuata ni nini???
Penzi likarudi tena la moto kinyama siku hiyo napigiwa simu usiku mtoto hajisikii vizuri nipeleke dawa nafika huko nakuta mamtu ndo hajisikii vizuri anautaka hahahaaaaaaaaaaa sikutaka kupoteza muda mzee nikatumia fursa vizuri nikaanza kufanya maandalizi ya nguvu🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Itaendeleaaaa
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni