DEMU MLA MADEMU
Kwl Story Killer
Sufuria la ubwabwa lilibiduliwa kwenye sinia kubwa. Baada ya kubiduliwa, ukafuatia mchuzi wa nyama na vipande kadhaa vilivyo katwa kwa madirio sana. Ile mchuzi kuishia…
Mikono ikaonekana pande zote za sinia ikikishambulia kile chakula bila hata kukumbuka sala, ama kusubiriana.
Naam, kile chakula kilifanyiwa uvamizi na madada poa, walio ificha hiyo kazi yao halisi kwenye kivuli cha uhudumu baa. Baa iitwayo MBAKA ASUBUHI maalufu na ilijizolea jina kubwa ndani ya mtaa huo wa MOLONI.
Ukubwa wa njaa yao ulijionesha kwa namna walivyo kuwa wanakipiga kile chakula. Maana ni fasta, kama abilia wanao taka kuwahi basi ambalo tayari limesha anza kuondoka.
"Shogaa! Kama msinge jiongeza kupika walahi mngenipoteza, maana nilikuwa nina njaa, hadi nikahisi tumbo linataka kukutana na mgongo."
Kauli hii ilitoka kwa Zena, mmoja wa wale wadada..
Kwa namna ilivyo, ilionesha kuwa wawili walibaki getoni kwa siku hiyo. Wale watatu ndio walikuwa mtaani, kule kwenye baa wanayo fanyia kazi.
"Mimi je, hapa hali tete! Na kile kibwana nilicho kipata leo sasa..
Shoo zake sio zakitoto. Kimeni minya-minya vibaya, mbaka nimejambia mbele. Badala ya kujambia kwenye ile njia ya maji taka.
Elfu sabini kiliyo nipa nimeona ni halali yangu kabisaa, wala sikuona hata haja ya kutoa shukrani. Yaani nimetoka nimenuna bila hata kuaga, nikatamani hata nikitukane!
Nikikumbuka niliye jipeleka ni mimi mwenyewe. Basi nikaishia kusonya tu."
Hilo aliongea Husna, akaelezea hali yake, na nusu kipande cha stori ya yaliyo mkuta huko geto kwa muhuni aliye muopoa siku hiyo.
"Kwahiyo leo tumejua kulipika?"
Aliuliza Deborah, huyu ni mmoja wa wale wawili walio baki nyumbani, na ndio walio andaa lile bweche.
"Sanaa!"
Sentensi hiyo ilijibiwa na Zena, kitoto fulani kibichi ambacho ndio kilianzisha lile zogo.
Lakini Rustina, mwenzao kati ya wale watatu alikuwa na maoni tofauti.
"Kupika mmepatia. Nawapa maua yenu kwa hilo, ila hapa kuna kitu kimemisi. Kama kingekuwepo basi mambo yangekuwa mia-mia bila dosari."
Ndicho alicho ongea yule mdada..
"Kitu gani kimemisi wee nae?"
Hilo swali lilitoka kwa Betha, ambaye ni mwenzake na Deborah walio baki wote magetoni wakikipika kile chakula. Kama ujuavyo watoto wa kike mambo ya kuoneana wivu..
Na Betha tayari aliisha onesha dalili za kupaniki, kutokana na ile hali ya Rustina kutaka kumkosoa.
Juu ya kope za macho yake kuka vamiwa na pingili za ndita, kama migongo ya bati za nyumba.
"Shoga nawe huambiwi?
Hivi unadhani nataka nikuchambe…
Uzuri leo sijaamuka hiyo mudi. Nilichotaka niseme si cha shali wala hakihusiani sana na nyie, kilicho misi hapa ni kachumbari fulani hivi yenye kamchuzi ka-kwenda."
Aliongea Rustina, ni kweli bwana alipo gusa ndipo. Maana sasa wote watano walitulia baada ya kusikia alicho sema, hata wale walio na chakula mdomoni waliacha kutafuta…
Watulia sababu waliambiwa kitu ambacho wote walikipenda. Sasa Betha aliamua kuzifanya zile tamaa zao kuwa kweli. Akaingiza mkono ule wa kushoto kwenye kifua chake, pale kwenye sidilia. Mkono ulipo toka, ulikuwa umebana noti ya shiringi elfu mbili.
"Husna katukimbizie fasta nyanya, karoti na vitunguu. Hapo jirani, kwenye duka la mama Uledi. Tena wakati naingia nimeviona, na nyanya zipo mbichi mbichi zenyewe."
Aliongea Betha. Ajabu Husna aliitazama noti ile kama vile hajaiona…
"Mmh! Jamani, nasikia uvivuu!"
Sentensi hii ya Husna ndio iliyo mwinua Deborah kutoka pale chini kwenye mkeka walipokuwa wanakula. Akaenda kuikwapua ile noti mikononi mwa Betha.
"Tunabaki tunajishauri, wakati wote tunauhitaji wa kachumbari. Kununua tu ndio shidaa. Mnabaki mme yapigilia makalio yenu kwenye sakafu."
Aliongea Deborah, akainuka na kujifunga vizuri kitenge chake. Maana siku hiyo alishinda nyumbani tu. Na…
Alikuwa amevaa kitenge.
Lazima niseme ukweli kuwa bajeti ya nyama kwenye uumbwaji wa mwili wa huyu dada ilikuwa ni kubwa. Hasa hipsini mwake, ndio maana bodi ilijitingisha wakati wa kuinuka kwake. Alitoka kama anapepesuka fulani.
Wenzake hawakumjibu, zaidi ya kumwangalia, kisha wakatazamana sura huku wamebidua midomo. Kisha wakaendelea kulisakata lile ngenge.
***
Hata hatua tano hazi-zidi, ni karibu! Na milango ilikuwa inatazamana. Maana ni kwenye kona ya nyumba. Wakati Deborah yule dada poa anatoka kwenye chumba chake, macho yaligongana na mwenyeji wa chumba kinacho fuata baada ya chao, kutoka kwenye ile kona.
"Za asubuhi dada!"
Deborah alisalimu, huku akigeuka haraka na kuanza kujivesha vindala vyake alivyo viacha kwenye kibalaza cha mlango wao.
Ajabu sasa, mbaka Deborah anamaliza kuvaa ndala na kugeuka, bado yule mdada alikuwa hajafungua kinywa na kuijibu ile salamu yake.
Deborah alipo geuka mara ya pili, macho yake yeye na ya yule mdada yaligongana. Baada ya kugongana yule mdada aliachia tabasamu la kujihami.
"Dada nimekusalimia!"
Deborah alijaribu kum-kumbusha, wakati huo aliisha anza kuinua hatua za miguu yake, tayari kwa kutoka nje.
"Nashangaa…
Salamu ya asubuhi napewa sahizi!"
Aliongea yule mdada, bado anatabasamu. Mkono mmoja alikuwa ameshika kitana. Na ule mwingine kioo kidogo, anajichana nywele zake ndefu za asili. Ambazo zimeipamba sura yake ndefu na nyeusi ya kushuka. Iliyo nakshiwa na jicho lake la kuita, pua fulani hivi, na mdomo wenye lipsi pana kiasi. Ambazo mwishoni, kwenye kingo zake zina kimstari chemba-mba kama vile ni wa kuchorwa.
"Hata sikujua, si muda wote leo nilikuwa nimejifungia."
Aliongea Deborah huku anainua sura yake na kulitazama jua, hata mwenyewe alipo tazama, akakubali kuwa alikosea salamu. Huenda ilikuwa saa sita kasoro ama saa saba.
"Nisamehe mwenzangu."
"Haya bwana…
Safari ya wapi hiyo sasa?"
Aliuliza tena yule mdada, ambaye ni jirani wa wale kina dada poa. Deborah alishtuka moyoni. Maana ni kama siku hii ya leo mdada yule alionesha hali kutaka kumzowea sana. Kinyume na ilivyokuwa mwanzo. Lakini aliamua kumjibu ili kuiepusha shali…
"Kwa mama Uledi hapo. Naenda kufuata nyanya za kachumbari."
Jibu la Deborah likamfanya yule dada kuamua kuacha kujichana, akakiacha kitana kiki ning'inia kichwani kwenye nywele. Mikono akaibana nisha makwapani mwake. Macho yake ya wastani, yaliyo jifinya kama yanahofia mwanga wa lile jua, yalikuwa yamekaza kwa Deborah.
"Ungesemaga mpenzi…nyanya ninazo za kutosha."
Aliongea yule dada. Kauli iliyo mfanya Deborah kuhisi kwamba kuna dalili ya kupona kwa ile buku mbili aliyo tumwa.
"Mweee! Nitashukuru jilani!"
Aliongea Deborah kwa lugha ya kujipendekeza.
"Njoo huku ndani…"
Aliongea yule mdada. Akimtaka Deborah aingie ndani kwake.
"Usiwaze karibu tu. Uchague zikazo kufaa, na za kukutosha."
Ndivyo aliongea. Haraka Deborah alitembeza kwato na kukaribia pale mlangoni. Ambapo yule mdada muda wote alikuwa amemfungulia pazia. Anamtazama kwa makadirio…
Hakulirudisha pazia mbaka Deborah alipo pita. Tena, alipo kuwa anampita alipeleka mkono wake na kumshika makalioni. Kidogo hilo liliweka viulizo moyoni kwa Deborah, ila aliamua kupotezea.
Mule ndani…
Baada ya kuingia, Deborah ilimtoka mimacho ya ushamba. Kulikuwa na kila kitu kizuri cha lazima na cha muhimu kinacho faa kuwepo nyumbani. Tena ni sebule kubwa, yenye chumba kimoja cha kulala chenye choo na bafu kwa ndani. Pia palikuwa na jiko, na sehemu ya kulia chakula.
'Hana mume, lakini ana kila kitu ndani. Jamani mwanamke mwenzetu huyu hela ana zitafutia wapi?
Ooh, ama..
Ndio ana madanga, yale yanayo jiweza? Lakini huwa ana danga saa ngapi? Muda wote yuko bize. Kama sio mtaani, basi ni nyumbani kajifungia ndani.'
Hayo yalipita moyoni kwa Deborah.
"Isikushangaze hali ya huku, kuanzia leo na kuendelea utapazowea. Maana siwezi kuwanyima kuingia kwa shida yoyote itayokuwa imewaleta."
Aliongea yule mdada huku anamshika mkono Deborah, Deborah alishtuka! Maana alikuwa amezama kwenye lile dimbwi la mawazo.
Baada ya kushikwa mkono, yule mdada alimwongoza mahali lilipo jiko.
Ama!
Iilikuwa ni jiko lenye hadhi yake. Lenye kuyapendeza macho ya mtu yoyote anaye penda vitu vizuri.
Kwa pembeni kuna kuna fliji, pia kabati lenye kila kitu. Humo kulikuwa na nyanya za kutosha. Lakini pia kulikuwepo na kachumbari ambayo tayari imesha katwa, hiyo ilikuwa juu, pembeni ya lile jiko la umeme.
"Mwanamke una pambana wewe!"
Deborah alishindwa kujizuwia na kuamua kutoa hizo sifa kwa mwanamke mwenzake.
"Wee! Umeonaje mbaka useme hivyo?"
Aliuliza yule mdada, akijifanya kuwa hajui kile kinacho mfanya Deborah atake kumpa sifa.
"Naona umejikamilisha. Ama shemeji yetu ndio anaghalamia?"
"Hapana, sijafika huko bado kipenzi. Najipambania mwenyewe."
Mwenyewe!
Hiyo ilimshtua Deborah. Kwa haraka akampiga jicho yule mdada. Akimshusha na kumpandisha. Ni mzuri!
Ijapo naye ni mzuri, ila alikili wazi yule mdada kamzidi.
'Hawezi kuwa singo huyu! Naijuwa hiyo.'
Hayo aliwaza, maana hakutaka kuamini kwamba mdada mzuri kama yule, eti akakosa bwana.
"Ipi siri ya mafanikio sasa? Maana si wengine tumeuza bia wee, mbaka tukageuka kuwa walevi. Lakini hakuna kilicho badilika. Zaidi ya kuishia kununua vipodozi na nguo."
Aliuliza Deborah.
"Aah, kawaida. Cha muhimu ni kuweka juhudi na nia."
Aliongea yule mwenyeji wa chumba kile. Akamshika mkono wake na kumvuta. Hali hiyo ilimfanya Deborah awe mbele ya yule mdada. Kabati lenye nyanya na ile kachumbali iliyo kwenye hotipoti lililo juu ya jiko, vilikuwa mbele yao wao wana vitazama.
"Sasa nisikuweke mpenzi, chagua mwenyewe nyanya za kukutosha ama kachumbari hiyo ambayo nimeikata tayari wala sina shida nayo."
Aliongea yule mdada. Ukaribu ulio kuwepo kati yao, haukuweza kuzuwia wao kuto gusana. Kila mtu akalihisi umbile la mwenzie namna lilivyo.
Bado ni Deborah!
Akiwa kwenye hali hiyo ya kutojua vipi ni vipi, mara akahisi vidole vya yule mwanamke mwenzake vikitembea kwenye nyonga, mara akashikwa! Taratibu vidole vile vilianza kum-balizi. Kutokana na utalamu wake kwenye michezo hiyo. Akili ya Deborah iliweza kutafsiri kitendo hicho, akajua vile vidole vilikuwa vikiikagua aina ya nguo yake ya ndani aliyo vaa.
Mwendelezo kipande kinacho fuata>>>
Kusema yote 1000 karibu WhatsApp no 0627790647.