SIMULIZI : KISURA WA DAMPO????????
(nilizaliwa na kichaa, nikazaa na ceo)
Sehemu ya 4
Basi hatukukaa sana sero tukatolewa ila wenzangu walipiogwa ila mimi niliachwa na nikamsikia mmoja wa maafande wa kike akisema, “ msimpige huyo ana mimba, ila watu wengine hata kujionea huruma hawajionei, yaan yeye mwenyewe hana hata pa kukaa ila anapanua tu…
Sikuwaelewa, ila tukatoka, ila wakati tunatoka kuna kijana alikuwa ni mtangazaji kwenye radio moja, ambae alikuwa anapambana sana kutetea haki za wasiojiweza, anaitwa nuhu suleyman, unaweza kumtafuta istagram ukampata, ni kijana ambae anapambana sana kutetea haki za watu, na alikuwa ni mtangazaji flani hivi bomba sana, alishawah kuwaahidi wenzangu kumbe siku moja atakuja kuwahoji na kulifikisha jambo letu dunian na huenda tukapata msaada ambao tulikuwa tunauhitaji……..
Akatuchukua na kutununulia mikate na juice, tulifurahi sana, maana ni mara chache sana tunakula vyakula visafi, kisha akakaa na sisi kisha akaanza kutuhoji, kuna mmoja wa kike ambae hakuwa ananipenda hjata kidogo maana alikuwa analalamika kuwa bwana ake alikuwa ananitaka bila hata kumjua huyo bwana ake ni nani, akaanza kusema…
“ najua watu wengi wanatuona sisi watoto wa mtaan kama hatuna maadili au hatuna adabu na kila siku mnatutuhumu kwa makosa ambayo mengine sio hata sisi ambayo tumeyafanya, ila naomba niwaambie watanzania kuwa, wengine tulizaliwa kwenye familia nzuri tu, ila siku zote wanaume tunawaomba muwekeze kwa wake zenu, maana siku moja mkija kutangulia mbele ya haki n I ndugu zenu wa chache sana ambao watamsaidia mke na watoto wako, hata kama wewe ukiwa umewasomesha na hizo kazi ambazo wanafanya umewatafutia wewe…
“ tulizaliwa wawili mimi pamoja na mdogo wangu, akasema Yule bint kisha akamuita yule mdogo wake na akaja mpaka walipo kisha akasema “ huyu hapa, na baba yangu alikuwa anafanya kazi bank mpoja hivi, ila nilipokuwa nina miaka saba na mdogo wangu akiwa na miaka minne, baba yangu alipata ajali, tena kwenye gari lake mwenyewe, aligongwa na lorry na kufariki hapo hapo, na hapo ndio maisha yetu yalibadilika, maana nilikuwa nasoma pale green valley na wakati huo nilikuwa darasa la pili, ila baada ya baba kufariki nikaacha kabisa shule, na ile miradi ambayp baba yangu aliifungua alifungua kwa majina ya ndugu zake, na hakuwa anamuamin kabisa mke wake, na hata nyumba ambayo tulikuwa tunaishi ilikuwa ina majina ya mdogo wake wa mwisho hivyo tukafukuzwa kama mbwa na mama yangu akawa anatulea, na kwa kuwa hakuwa na elimu, wala na ujuzi wowote ule wa biashara, akaamua kujiuza ambapo alipata ukimwi mimi nikiwa na miaka kumi na alipojua kuwa anaukimwi alikata tamaa na kukataa kutumia dawa mpaka alipofariki, na hapo ndio safari yetu ya kuwa watoto wa mitaani ikaanza….
Ingawa sikuwa nampenda huyu bint, ambae alikuwa anatoa historia yake, na alikuwa anaitwa Semeni ila nililia sana, maana kweli watoto wengi wa mtaan sio kama wanataka yale maisha ila hawana namna tu ya kuishi…
Yule mtangazaji alipoona nalia sana, akaniita na kutaka na mimi nije kutoa ushuhuda wangu, noilishindwa kuongea kwa karibu dakika kumi na tano nikawa nalia tu, maana kila nikikumbuka nimeuuza usichana wangu nikujua nitamsaidia mama yangu ila mwisho wa siku amefariki, na kila nikiwaza ile story ya semeni ndio kabisa machozi yalikataa kukauka kwenye macho yangu….
NAKUJA…..
MREMBO WA DAMPO 5
(nilizaliwa na kichaa, nikazaa na ceo)
WHATSAPP 0755090082
Basi Yule kijana mtangazaji akanisubiri nilie mpaka uchungu wangu uishe kisha nikaanza kusimulia na mimi kuwa “ kiukweli mimi simjui baba yangu, ila mama yangu alibakwa sijui na nani, maana alikuwa kichaa, yaan Yule kichaa kabisa wa kuokota makopo, na sikuwah hata kumsikia akiongea zaidi ya kucheka cheka tu, kwa hio kuanzia nazaliwa nilijikuta ni mtoto wa mtaani, nililelewa na mama yangu kichaa, na alikuwa mkali huyo balaa, yaan mtu akinigusa anaweza kumlenga na mawe mpaka akashangaa, hivyo alinilea mwenyewe tu, mpaka nakuwa bint ambae mnaniona hivi sasa, ila nilizaliwa mpwapwa na sio arusha, nikaendelea kusimulia…
“ ilikuwaje mpaka ukafika arusha kutoka mpwapwa ? akaniuliza Yule mtangazaji….
“ siku moja nikiwa nimelala na mama yangu na siku hio kulikuwa na mvua, akaja mwanaume mmoja ambae sikuwa namfahamu na hakuwa chokoraa mwenzangu, maana alikuwa amevaa vizuri na alikuwa ananukia akataka kuniingilia, ndio mama yangu akampiga ili aniachie na watu wake wakampiga mama yangu mpaka akapoteza fahamu, nikawa kama nimechanganyikiwa, nikawa natafuta msaada wa mama yangu, nimekuja kurudi namkuta mama yangu anatoa wadudu na manispaa wakamchukua kwaajili ya kwenda kumzika, na sikuwa nataka kuendelea kukaa tena pale ndio nikapandishwa kwenye lorry na wenzangu kisha nikajikuta nipo mpanda, nikasema na Yule kijana akawa anaonekana kutuonea huruma sana yaan…
Basi akamuohoji kila mmoja na kumbe maisha yetu yalirushwa kwenye moja ya page ya mtu ila haikwenda sana na haikuonekana sana ila kumbe Yule bwana kaka ambae ni mackmill aliona na kumbe alikuwa ananitafuta kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote yale, na hapo nilikuwa nimeshajigundua kuwa nilikuwa na mimba, maana mtoto alishaanza kucheza tumbon na tumbo lilikuwa limeshakuwa kubwa tayar, na mtu yoyote Yule laiti akiniona ni dhahiri atajua kuwa nilikuwa ni mjamzito tena bila kujificha kabisa yaan…
Kumbe siku ile baada ya kutupa ile card ya benk, yule dada akaichukua, na haikuwa na million tano kama ambavyo niliambiwa, ilikuwa na zaidi ya million thelathin na Yule dada akaichukua ile card na alikuwa anaijua namba ya siri ya mackmill hivyo hakuteseka kutoa pesa na kutumia na akahama kabisa na sehemu, sasa kama tunavyojua pesa ikitolewa muhusika anatumiwa kiwango cha pesa kilichotolewa, hivyo akawa anatumia sms mara imetolewa million mbili, mara imetolewa million tano, mara imetolewa million tatu na mambo kama hayo……….
Sasa mackmill akajua kuwa nimechukua ile card na kwa matumizi ambayo nilikuwa nafanya akajua kuwa naishi maisha mazuri sana, kumbe ndio hivyo nilikuwa naishi maisha ya kuunga unga tu yaan, hayana mbele wala nyuma, ila akaja akaona ile interview, ingawa haikuwa na watu wengi ambao waliitazama, ila ni kama mungu tu alitaka mackmill aione , a;lishtuka sana kuniona na mimba, tena nmilikuwa kama chokoraa na wakati alinipa card yenye pesa nyingi sana….
Akaanza kusema kuwa anataka nitafutwe na anataka aelee mimba yake mwenyewe, hata hata mimi sina ninachoelewa kama natafutwa au laa, siku moja kulikuwa na mvua, na hata kama wale migambo walikuwa wanatujua ila walikuwa wanataka zile pesa zetu kidogo ambazo tulizipata baada ya kufanya kazi za kubeba mizigo na kusaidia watu mchana hivyo wakaanza kushika watu hovyo, na wakati huo nilikuwa naweka pesa ili angalau mwanangu apate nguo, ,maana sikuwa na pesa za kueleweka , wala sikuwa na uhakika wa kupata pesa za moja kwa moja…..
.Je nini KITAENDELEAAA!! "
ofaaa simulizi hi ipo mpk mwisho ni .