MAMBO YA KUFANYA PALE AMBAPO MWENZA WAKO ANAPOKUNUNIA /MWENZA WAKO ANAPOKAA KIMYA TU BILA SABABU ZOZOTE ZA MSINGI
Mwanamke huwa kiumbe ambaye anakuwa na mabadiliko ya hisia ghafla (mood swings) Kwa maana dakika moja anakupenda sana kisha dakika inayofuata anakuchukia hataki hata kukuona.
Lakini hivi sasa wapo wanaume wenye kuonyesha tabia hizo za kununa, kususa, kugoma kulala, kulala mzungu wa nne,kukaa na hasira kupitiliza kwa muda mrefu bila sababu zozote za msingi.
Kwa wanaume wenye mood swings ukifanya uchunguzi utakuta wengi wamekulia familia ambazo hakuna mwanaume imara ambaye ni mfano bora wa kuigwa hivyo wao hujikuta wanaiga hulka ya kununa, kususa,kukunja sura kwa ghadhabu,kuwa na gubu pamoja na kisirani kutoka kwa mama zao na dada zao.
Hivyo leo tuangalie muhtasari wa namna ya kukabiliana na tabia ya gubu, kisirani,kununa, kususa, kugoma kutoa unyumba,kugoma kulala pamoja,kulala mzungu wa nne ambapo tabia hizo mwenza wako akiwa nazo zinaweza kukusumbua.
Je imekuwa kawaida kuona tabia zifuatazo kwa mwenza wako?
-Anakata mawasiliano ghafla bila sababu zozote za msingi na endapo ukiuliza kuhusu mabadiliko ya tabia zake atakugeuzia kibao kisha unazuka ugomvi mkubwa sana.
-Atakuomba fedha nyingi sana kuliko uwezo wako kisha ukisema hauna fedha ananuna, anaanza kulalamika,anadai haumpendi,anatishia muachane,anakutangaza vibaya.
-(mwanamke),anagoma kupika, kufua, kufanya usafi wa nyumba, kutandika kitanda,kuandaa watoto kwenda shule,anatoroka kwenda nyumbani kwao kusingizia ananyanyaswa,anabamiza mlango kwa ghadhabu,au anapopika anaunguza chakula,au akinyosha nguo zako anaunguza kwa makusudi kisha anasingizia bahati mbaya .
-Mwenza wako anakuwa na hasira kupitiliza, huzuni, majonzi, upweke kupitiliza,kila juhudi za kumfurahisha zinazidisha hasira zake.
-Mara kwa mara mnakuwa kwenye majibizano, kutukanana, kudharauliana, kushutumiana, kufokeana,kupeana vitisho, kutishia kujiua, kutishia kukudhuru,kutishia kukupokonya zawadi zake alikununulia.
-Imekuwa mara kwa mara unapiga magoti,unaomba msamaha mara kwa mara, kumbembeleza,kumpa ushauri, kumkumbusha wema ambao umemfanyia,kuanza kulia ili kumshawishi mwenza wako abadili tabia..
Kwanini watu hupenda kuwanunia wenza wao ?
FAHAMU SABABU ZENYE KUCHOCHEA WENZA KUNUNIANA.
Zifuatazo ni sababu zenye kufanya watu kuwanunia wenza wao.
1.Kushindwa kufikia muafaka.
Kama mwanaume na mwanamke wameshindwa kufikia muafaka labda kuhusu kuzaa,kusomesha watoto, matumizi ya uzazi wa mpango,malezi ya watoto, matumizi ya fedha,kutoka pamoja "Out",kukatazwa kwenda nyumbani kusalimia wazazi (mwanamke) husababisha mwanamke au mwanaume kuamua kununa, kususa, kugoma kutoa unyumba, kugoma kulala pamoja,kulala mzungu wa nne,kukaa kimya kama bubu muda wote,kujitenga kila wakati mmoja wao anapotaka kujenga ukaribu.
2.Safari kuahirishwa,au kunyimwa fedha ,au kukataliwa kitu chochote kwa mfano mwanaume anataka mwanamke amchukulie mkopo kwa kuweka dhamana kazi au mali zake ambazo mwanaume hajachangia hata senti tano kisha mwanamke amekataa,au mwanamke anataka kusomeshwa lakini mwanaume amekataa,au mwanamke anataka anunuliwe gari,au apewe mtaji lakini mwanaume amekataa hivyo husababisha hisia za chuki,wivu,kinyongo,kuitana majina ya wanyama kama mbwa na nguruwe kama kisasi cha maumivu ya kukataliwa.
3.Kukaa kimya kama shinikizo la mabadiliko ya tabia.Kwa mfano mwanaume anataka mapenzi kinyume na maumbile kisha mwanamke amekataa hivyo mwanaume anaweza kuhama nyumba,au kuongea na michepuko mbele ya mke wake,au anasusia chakula,kugoma kulipa ada za watoto,kugoma kuhudumia familia kama njia ya kulipiza kisasi.Lengo la yote hayo ni kumshinikiza binti akubali kuingiliwa kinyume na maumbile.
4.Kujilinda kihisia.
Kuna watu ambao tangu utotoni walijifunza kukaa kimya kama silaha ya kujilinda dhidi ya mateso kutoka kwa wazazi.kwa mfano mtoto anafokewa, kutukanwa, kujibiwa vibaya, kupelekeshwa,kutishiwa kuuawa hivyo kama anajua akiongea atakuwa kwenye matatizo ikiwemo kipigo,kunyimwa chakula,kulazwa nje huamua kujilinda dhidi ya kipigo cha mzazi kwa kukaa kimya kwa sababu anajua baba au mama ni mtuwa hasira kupitiliza hivyo kujibu matusi ya mzazi kunaweza kumletea matatizo zaidi.
Wengine walijifunza kukaa kimya utotoni kama njia ya kushinikiza kupewa mahitaji yao kutoka kwa wazazi wao.
5.Kukaa kimya ili kuepuka ugomvi.Baadhi ya watu wanajijua wapo na hasira kupitiliza vilevile huwa na desturi ya kuropoka hovyo hivyo huamua kukaa kimya ili kuepuka kuongea kitu kibaya kisha baadaye aingie kwenye mikono ya sheria.Mtu mwengine anajua akiongea tu ghafla majibizano, kutukanana, kudharauliana, kushutumiana, kufokeana, kupeana vitisho,kupeana kashfa,kuvujisha siri za faragha kunaweza kujitokeza.
6.Kukaa kimya kama adhabu kwa mwenza au mtoto Baadhi ya watu tangu utotoni walijifunza kukaa kimya kama adhabu kwa wakosaji wao.Kwa mfano mzazi anakaa kimya haongei na mtoto kwa sababu mtoto amefeli masomo, mwengine anakaa kimya kama njia ya kuepuka usije kuomba fedha za matumizi,mwengine anakaa kimya ili kupunguza ukaribu na wewe,mwengine anakaa kimya tu ili umuombe msamaha,uanze kulia,upige magoti,umnyenyekee.
7.Kukaa kimya kama njia ya kutafuta kisingizio cha kuvunja mahusiano.Mtu mwengine anakuacha ghafla kimyakimya haongei chochote anafanya "Ghosting) kwa maana anapotea ghafla,simu hapokei, ukituma sms hajibu, usipomtafuta hakutafuti,ukikaa kimya anakaa kimya hata miezi sita (6) huyu anafanya hivyo ili ukate tamaa muachane lakini baadaye atarudi kusingizia shetani alimpitia hivyo anataka mrudiane lakini anakuwa na "Target " zake umpe faraja na msaada wa kifedha tu ili aondoke zake kwenda kwa mwenza wa HADHI yake.
MADHARA YA KUNUNIANA/KUKALIANA KIMYA
UNapoamua kununa, kususa, kugoma kutoa unyumba, kugoma kulala pamoja, kulala mzungu wa nne, kukaa kimya kama bubu muda wote bila sababu zozote za msingi jiandae kwa matoleo yafuatayo
1.MAELEWANO KUKOSEKANA
Wewe au mwenza wako mmoja atakuwa na hasira kupitiliza,hisia za kisasi, chuki, kinyongo,upweke kupitiliza, kupoteza hisia za mapenzi, kupoteza hamu ya kula au kula sana bila mpangilio, kukonda,kushindwa kufanya kazi.
2.UPWEKE KUONGEZEKA
Mmoja au nyote wawili,upweke kupitiliza utajitokeza.
Unaweza kuelemewa na majukumu pale ambapo mwenza wako hakupi ushirikiano wowote.Kwa mfano mwanamke akigoma kupika, kufua, kufanya usafi wa nyumba, kutandika kitanda, kuandaa watoto kwenda shule huku anakaa kimya tu haongei chochote ,au yupo busy kuchati tu,au anatoroka kwenda nyumbani kwao kusingizia ananyanyaswa mara kwa mara husababisha hisia za upweke kupitiliza.
3.UGOMVI KUONGEZEKA
Pale ambapo mnakaa kimya bila kuongea chochote,sio kila mtu ni mvumilivu.
Mmoja anaweza kuanza kuporomosha matusi ya nguoni,kisha mtaaanza kutukanana, kudharauliana, kushutumiana, kufokeana, kupeana vitisho, kutishia usalama wa kila mmoja,tishio la kuachana,mmoja ataonekana mbishi,mbabe,mtemi, mjuaji, hashauriki, haambiliki,mtu wa misimamo mikali sana.
4.Manyanyaso kuongezeka.
Mwanaume au mwanamke mwenye wivu wa mapenzi kupindukia ataamua kumtawala mwenzake kimabavu kwa kumpokonya simu, kumnyang'anya ATM card,kumpangia marafiki,kumtangaza vibaya mwenzake,kumlaza nje,kumlaza chooni,kumnyima chakula,kumnyima huduma za matibabu, kumpokonya hati miliki, kumchafua,kuhamasisha mwenza wake kutengwa na jamii.
Ufumbuzi wake
Kuna nja nne (4) za ufumbuzi wake.Kwa muhtasari
1.Pata utulivu wa akili-Epuka kutegemea faraja ya mwenza wako,epuka kupiga simu mfululizo, kutuma sms mfululizo, kujitumisha zawadi na fedha,epuka kuanza kulia,epuka kumbembeleza.Ishinde hofu ya mahusiano kuvunjika.
2.Mpe mwenza wako nafasi
Kama mwenza wako akianzisha mahusiano mapya kipindi umempa nafasi ya kupata utulivu wa kiakili basi achana naye.Uguza kidonda chako anza upya.
3.Tumia lugha fasaha yenye kueleweka na heshima,eleza unataka nini na hautaki nini.Kama ukifanya makosa omba msamaha,kama mwenza wako hataki kusamehe basi muachane kwa amani.
4.Weka mipaka.Tambua tabia gani unaweza kuvumilia na tabia gani hauwezi kuvumilia.
haya yapo ndani ya kitabu cha JINSI YA KUPONA MAUMIVU MAKALI SANA MOYONI.
#Spirit_Warrior
#Wounded_Healer
????????
Kama tatizo lako ni kubwa zaidi tunaweza kuwasiliana kwa ajili ya Counselling session na ufafanuzi wa kilichoandikwa hapo juu na utaona mabadiliko na kujisikia nafuu ndani ya muda mfupi baada ya mazungumzo.(Counseling kwa njia ya simu gharama Tshs 30000 , kuonana uso kwa uso Tshs 40000
Kwa wapenzi wa kusoma vitabu unaweza kupata nakala zangu orodha ipo chini ????
Kupata kitabu cha
1.JINSI YA KUPONA MAUMIVU MAKALI SANA MOYONI - (Softcopy Tsh 30000)
2.UTULIVU WA AKILI KIPINDI KIGUMU (Softcopy)
3.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
4.TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (by & Softcopy)
5.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
6.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)
7.MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)
8.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO
BEI Kitabu kimoja softcopy 5000 isipokuwa kitabu namba 1 bei yake ni Tsh 30000, hardcopy moja 10000
Mawasiliano
+255766862579
+255622414991
Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam.