TIPWA TIPWA NA MR MARVEL. SEHEMU YA 12
🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋🦋
Mr. Marvel akaendelea “Niliendelea kufanya kazi na wakati mwingine nilikuwa nambeba Salmon na kwenda naye kazini. Kwa sababu hiyo, nilipoteza baadhi ya kazi kwa sababu haikuruhusiwa kufanya kazi na mtoto. Nilipokuwa napambana na maisha nilisikia mke wangu ameolewa na mwanaume mwingine tajiri, maarufu na mwenye nguvu. Iliniuma, lakini nilisema sawa tu. Niliendelea kufanya kazi mchana na usiku mpaka nikakutana na rafiki yangu wa zamani………… Huyu rafiki Tulikuwa karibu sana lakini mambo yakatufanya tutengane. Yeye alikuwa ana maisha mazuri, alikuwa na biashara kubwa. Alijua mimi ni engineer mzuri, lakini sikuwahi kupata nafasi ndipo Akaamua kunipa kazi kwenye kampuni yake. Kuanzia hapo maisha yakaanza kubadilika. Niliweza kupanga nyumba nzuri, nikaajiri mtu wa kumwangalia Salmon nikiwa kazini. Niliweza kumudu milo mitatu kwa siku hata sita kwa siku pia niliweza. Maisha yakawa mazuri na sikutaka tena kufikiria mapenzi. Nilijikita kwenye kazi na kumlea Salmon tu.
So Miaka mitano ikapita Nikaanzisha kampuni yangu na sasa imekuwa kubwa”
Noela akauliza “Na mke wako?”
“Now ni zamu yake kuteseka. Yule mwanaume aliyemuoa alimwacha na hakupata mwanaume mwingine tena. Aliposikia nipo vizuri Alitaka kurudi kwangu lakini sikumkubali”
“Kwaiyo Sasa yuko wapi?” 🤔
“Yuko Mwanza anaishi kwa ndugu zake. Sijui anafanya nini sasa na sijali sana kuhusu yeye”
“Salmon anamkumbuka mama yake?”
“Yes! Licha ya yote aliyofanya, bado ni mama yake. Wakati mwingine anaenda kumtembelea na kukaa naye siku chache”
“Unadhani Salmon anataka mrudiane na mama yake?”
“Mhhhhh! Ndiyo! zamani alikuwa ananisihi nimsamehe mama yake na mimi nikamsamehe. But kurudiana ilikua ni ngumu sana”
Noela akauliza “Kwa nini?”
“Kwa sababu ya yote aliyonifanyia ni ngumu kumuamini tena! Also kwa sasa moyo wangu unadunda kwa mwanamke mwingine. Nategemea siku moja atanipa nafasi nimuonyeshe ananichanganya kiasi gani” aka tabasamu😍
Noela akabaki kimya, akaona aibu kwa sababu alijua mwanamke anayezungumziwa ni yeye.
Mr. Marvel akauliza “Una swali lingine?”
“Ndiyo. Uliwezaje kukaa peke yako muda wote huo?”
“Kwa kweli ilikuwa ngumu. Nililala na wanawake wachache mpaka siku ile nilipokutana na wewe hotelini. Na mimi pia nataka nikuulize, ulikuwa unafanya nini pale?”🤔
“Kabla sijakujibu, Kwanza si uliona jinsi chumba kilivyopambwa?”
“Yes”
“Ilikuwa kwa ajili ya Salmon. Nilimuandalia kila kitu, lakini hakuja. Ilipaswa kuwa usiku wetu wa kwanza”
“Samahani kwa kuharibu usiku wako”
“Nafurahi ulifanya hivyo. Ni Bora nimpoteza usichana wangu kwa mtu mzuri kama wewe na sio Salmon. Unajua aliniambia eti hakuja hotelini kwa sababu baba yake alipata ajali?”
Mr. Marvel akashangaa, “Nini? Mimi? Ajali? No!”😳
“Ivyo ndivyo mwanao alivyo nidanganya! Lakini yaliyopita, yamepita”
“Ningependa kuomba msamaha kwa niaba ya mwanangu! Ni kijana mzuri and i love him ila ni
Ujana tu unamsumbua!”😊
“Usijali kuhusu ilo ila Wewe ni tofauti sana na yeye”
“KiVipi?”
“Wewe unajali, ni mpole, mnyenyekevu na pia mkorofi. Si rahisi uumize mtu kwa sababu wewe uliwahi kupitia maumivu kama hayo”
“Vizuri sana. Umenisoma vizuri”😊
Noela akatabasamu kisha Wakakaa kimya kidogo ndipo wakaamua waingie ndani maana giza lilikwisha ingia.
Kwa muda wote Noela alipokuwa kwenye ile nyumba, alizidi kuwa karibu sana na Mr. Marvel. Walikuwa wanapiga stori, wanapika pamoja, wanaangalia movies na kutoka mara kadhaa.
Ilikuwa ni wiki mbili tu, lakini ilionekana kama wamejuana muda mrefu. Na kwa sababu ya Mr. Marvel, Noela aliacha kufikiria kuhusu Salmon na Iris.
Basi Usiku mmoja walipokuwa sebuleni, Noela akamwambia Mr Marvel kuwa anataka kurudi chuo.
Mr. Marvel akauliza “Una uhakika?”
Noela akasema “Ndiyo”
“Utakaa chumba kimoja na Iris?”
“Sitaki Na sijui nitaishi wapi”🥺
“Kama ndo ivyo… Endelea kukaa hapa”
Noela akauliza “Na chuo je?”
“Usijali, Nitakupa gari na dereva. Atakuwa anakufikisha chuo kila siku, na baada ya masomo atakurudisha nyumbani salama. Apo Vipi?”
Noela akashangaa “Utanifanyia hivyo?”😳
“Ndiyo! kama utakua tayari”
“Mimi nipo tayari” Noela Alifurahi sana kwa sababu hatalazimika kukutana na Iris au Salmon mara kwa mara🥳
Kwa upande mwingine, Salmon alikuwa anamtafuta Noela lakini hakumpata. Hakujua aende wapi kumtafuta kwa sababu Noela hakuwa na marafiki wengi.
Pia simu yake ilikuwa imezimwa. Noela Aliwasha simu tu alipotaka kuwasiliana na familia yake kisha anazima ndo maana ilikuwa ngumu sana kwa Salmon kumpata.
Hali hiyo ilimkera sana Iris. Alikasirika kwa maana Salmon bado alikuwa anamtafuta Noela badala ya kumpa yeye attention🤣.
“Wakati mwingine nahisi ulikuwa unanitumia tu”
Iris alilalamika
Salmon akauliza “Unamaanisha nini?”
“Noela hayupo badala iwe nafasi yetu kufurahia mapenzi yetu lakini wewe kila wakati unamtafuta, unampigia simu, hunipi attention ninayo stahili. Tayari Nimewaambia watu wote kuwa tuna date, ila ni ngumu wao kuniamini coz huonyeshi mapenzi kwangu”
“Iris, nitakuonyesha mapenzi baada ya kumpata Noela. Hata huogopi au kuwa na wasiwasi labda kuna kitu kimemtokea? Tangu atufumanie siku ile hajawai pokea simu zangu wala kuja chuo”😳
“Mimi najali kuhusu wewe tu Salmon! Achana na ilo tipwa tipwa lako”😒
“Iris, Noela alikuwa rafiki yako. Angalau uwe na huruma kwa anachopitia”
“Kheeee! Ni kosa langu kwamba humpendi? Ni kosa langu kwamba hukuwa mwaminifu kwake? Hili si tatizo langu. Please usilitaje tena jina la yule nguruwe”
“Unajua nini?? Acha nirudi nyumbani coz mood imeisha”
“Hutalala hapa? Nilidhani umekuja kukaa na mimi”🥺
“Siwezi kulala hostel. Vipi kama Noela akirudi akatukuta tena hapa?”
“Sawa, basi twende wote huko kwako!”😊
“Uwende wapi?? Wewe kaa hapa, subiri kama Noela atarudi au laaah! Kama Akirudi nipigie simu”
Salmon akaondoka akimuacha Iris akiwa na hasira. Iris Hakujua afanye nini ili moyo wa Salmon uwe wake kabisa, kwa sababu kila kitu alichofanya hakikufanikiwa.
Sasa Asubuhi ya siku iliyofuata, Iris akiwa amelala, akasikia mtu akiingia chumbani. Alidhani ni Salmon, lakini alipomuona Noela, akaogopa kidogo kisha akajifanya hajali kuhusu ule ujio wake.
kwa dharau akauliza “kheee ndo umerudi?”😒
Noela akajibu “Ndiyo”
“Sikiliza Noela, sijali kama umerudi au la. Hilo ni jambo lako. Ninachotaka ni ukae mbali na mwanaume wangu, Salmon. Tunapendana, sitaki na drama zako”
Noela akatabasamu akisema “Sawa” kisha Akaanza kufunga makabati akitoa nguo zake na kupaki kwenye mabegi kimya kimya🤐.
Hili jambo lilimshangaza Iris kwa sababu alidhani Noela angegombana naye lakini hakufanya hivyo.
Baada ya kumaliza kupaki mizigo yake, dereva wa Mr. Marvel akamsaidia Noela kubeba mabegi yake na kuyapakia yote kwenye gari. Walipomaliza waliondoka zao.
Iris kuona vile akachanganyikiwa zaidi. Noela amehama hostel na tena amekuja kuchukuliwa na gari la gharama, na dereva juu!😭
“Ina maana Noela kapata mwanaume tajiri? Ndiyo maana haumi sana kuniona na Salmon? Kwa lile gari, lazima huyo mwanaume ni tajiri. Ina maana yeye kapata mwanaume tajiri, mimi nateseka na Salmon ambaye hajawahi hata kuninunulia kijiko. Lazima nichunguze nijue huyo mwanaume ni nani, ikiwezekana nimpitie. Noela hawezi kunizidi mimi. Mimi ni mzuri kuliko yeye tipwa tipwa kama ngiri”
Je Nini kitaendelea?
Nakuja…
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni