WATOTO MAPACHA,
kipande Cha 13
Wazazi wa Stefano pamoja na Celina walikaa pale hospital mpaka mama Celina akazinduka ,na alipozinduka alitulia japo alikuwa anaweweseka kulingana na ukichaa wake huku yale mambo yalipita akiyasahau ,wakajua ni kichaa kilimpanda , wakaruhusiwa kumchukua na kurudi nae nyumbani , walimpakia kwenye gar na kurudi nae mpaka pale nyumbani kwa kina Stefano hawakutaka kumrudisha kule majalalani Kwan waliamua kumsaidia mama Celina pamoja na Celina mwenyewe ,
Mama Stefano alijua kama Celina atakuwa hapo nyumban basi kuna uwezekano mkubwa yule Celena akaja sasa akija lazima wakutane hapo ndio atajua ukweli ,
Walifika nakupaki gari ,wakatelemka na kumtelemsha Celina kichaa,yaani mama Celina ,lakini walipomtelemsha tu mama Celina akataka kukimbia wakamdaka na ikawa vurugu ya vuta nikuvute ,
Mala wakafanikiwa kumkamata na kumfunga miguu kwa kutumia kanga ,
Mama Celina akatulia,
Wakamletea chakula akakataa kula kabisa ,yaani nikama kichaa kilirudi upya ,
Aliongea maneno huku akirusharusha mateke,
Celina alimjulia mama yake akasema hiko chakula kiwekeni kwenye mfuko mchafu mchafu halafu kiwekeni nje mi nikija nikichukue,
Mama Stefano alifanya kama alivyoambiwa na kweli Celina akatoka na kukichukua na kumletea mama yake,
"Usimfungue atakimbia ujue ,,"
Mama stefano alimwambia Celina maana Celina alikuwa anamfungua mama yake ile kanga ,
"Hawezi kukimbia mi nikiwa nae,,""
Celina alijibu ,
Na kweli Celina akamfungua mama yake wakaanza kucheza ,na chakula kilipokuja Celina alimtengea mama yake halafu wakaanza kushindana kula ,yaani ilikuwa ni kama mchezo tu ,walishindana kula mtu na mtoto wake na mama mtu akashinda ,Celina akajifanya kununa ,na mama yake akampakata akaanza kum bembeleza ,
Celina akawakonyeza wazazi wa Stefano ,wakajikuta wanacheka tu ,
Shuleni kwa kina Celena , Celena akajikuta anapata hamu ya kumuona Stefano pamoja na wazazi wa Stefano ,alikumbuka siku ile walicheza pamoja na Stefano mpaka akachelewa kwenda kwao akajikuta analala huko huko ,
" Nikitoka tu naenda "
Aliwaza Celena ,
Na kweli kengele ilivyolia tu akachomoka hakusubili hata gari ya kwao kuja kumchukua , akanyoosha na njia kwenda kwa kina Stefano,
Kwa bahati mbaya Baroz baba yake na Celena alikuwa anapita njia hiyo hiyo anaelekea nyumbani akamuona Celena mwanae anakata mitaa , akajiuliza huyu mtoto anaenda wapi tena , na mbona hajapanda gari la shule ,?
"Ngoja leo nisimstue nijue anakoelekea "
Aliwaza Baroz huyo wa serikali,
Wakati Celena anakaribia kwa kina Stefano gafra mama yake Celina yaani yule kichaa akamuona , nae akajua kuwa ni Celina amekuja kutoka shule , akaanza kumchekea chekea huku akimkimbiza , celena nae kutokana na ule woga akakimbia na kujificha ili yule kichaa aondoke ,celena alikuwa hajui Kama mama huyo ndio mama wa Celina ,ikabidi ajifiche kwanza sehemu,
Na wakati huo baba yake na Celena Baroz alisimamisha gari baada ya kumuona mwanae ameingia uchochoron, sasa pale aliposimamisha gari ndipo alipo mama Celina kichaa ,
" Haa huyu si mke wangu huyu ,"
Aliwaza Baroz huku akimkazia macho mama Celena , na mama Celena nae baada ya kuliona lile gari nikama alikumbuka akalisogelea na kulishika akisema " hii gari ya mume wanguu jiiiimmmmh piipiii ,,!
"Celinaaaa nenda kamtoe mama yako kwenye gari ya watuu Mungu wangu akivunja kioo sijui itakuwaje,"
Aliongea baba Stefano na wote wakatoka nje wakawa wanamshangaa mama Celena jinsi alivyokuwa anafanya kwenye ile gar ,
Sasa walipotoka nje tu barozi akashangaa kumuona mwanae Celena yupo katikati ya ile familia halafu kabadilisha nguo kavaa nguo za nyumbani ,
"Haa huyu kabadirisha nguo saa ngapi na si aliingia kwenye kile kichochoro,"
Aliwaza Baroz huku akimkazia macho Celina akizani ni Celena mwanae ,
" Celinaaa njoo uone gari ya baba yakoo ,,ona ilivyonzuriii aaammmmh pipiii ,"
Bado mama Celina alifanya vituko pale kwenye ile gari , bahati nzuri ile gari ilikuwa na tintedi nyeusi yaan mtu wa ndani anamuona wa nje lakini wa nje hamuon mtu wa ndani,
Kwa hiyo Barozi alikuwa anawaona wote lakin yeye hawamuoni,
"Sasa huyu Celena kamjuaje mke wangu na wale ni wakina nani ,"?
Bado alijiuliza Baroz huku bado akiwashangaa wakina mama Stefano pamoja na Celina ,alichokishangaa zaidi ni jinsi yule mama alivyofanana na Celena , yaan Kama mtu na mtoto wake kabisa , Mr Benson au barozi yeye alibaki kushangaa tu huku akimwangalia Celina alizani ni mtoto wake Celena,
Sasa kule alikojificha Celena akachungulia akaliona gari ya baba yake imepaki akaangalia pembeni akawaona mama Stefano,baba Stefano ,Celina na Stefano tena wanamshangaa yule mama kichaa ,
Akaona ngoja ajifiche kwanza maana akitoka tu baba yake anaweza kumgombeza na kumwambia kwanini uko huku unazurura , ikabidi atulie tu huku akichungulia , Nia yake ni kumsubilia baba yake aondoke Kisha aende pale kwa kina Stefano akaonane na Celina ,
Sasa Mr Benson barozi akaamua atelemke kwenye gari ili awasalimie wale watu waliokuwa na mtoto wake Celena yeye alizani ni Celena kumbe ni Celina , Sasa aliposhuka tu , yule kichaa mama yake na Celena akamuona , yaani ikawa Kama muvi wakabaki wameangaliana kwa sekunde chache , gafra tu yule mama kichaa akatamka "MUME WANGU ,"
tena alisema huku machozi yanamtoka ,barozi nae akajibu ," MKE WANGU ,"
Ilikuwa ni Kama dakika tu za kuhesabu kila mtu alishangaa , maana yule kichaa katamka neno ambalo ni sahihi na Mr Benson nae akajibu inamaana Yule mama kichaa amekumbuka kuwa yule aliesimama pale ni mumewe ,
Celena alitaka kwenda kumshika mama mama yake akazuiwa kwanza na mama yake Stefano ili waone kitakachotokea maana walishangazwa na ile kauli ya wote wawili ,
,Sasa Mr Benson akamsogelea yule mama kichaa ili amkumbatie , yule mama kichaa akasogea nyuma Kisha akaokota jiwe ,
" Tokaaa mbele yanguuu ,," aliongea yule mama kichaa huku akimtishia Kama anataka kulirusha lile jiwe ,
" MKE WANGU nisikilize basi kwanza "
Aliongea Mr Benson huku watu wakishangaa maana tayari watu walishaanza kujaa ,
" Hee mbona anasema ni mkewe , "?
Baba Stefano alimuuliza mama Stefano ,
" Yaani jinsi unavyoshangaa na Mimi ndo nashangaa hivyo hivyo ,"
Mama Stefano alimjibu mumewe ,
Sasa Mr Benson akamsogelea tena yule kichaa lakini gafra yule mama kichaa akarusha jiwe na likapasua kioo Cha nyuma chagari , pwaaaaa ,,!!!!
" Nimekwambia ondokaaaa ,,, umeniacha Mimi ukaoa mfanyakazi mshenzi weeeeee ,,, " aliongea yule mama kichaa huku analia , Sasa ili kuepusha usumbufu , Mr Benson akapanda kwenye gari huku anamuita Celina alizani ni mwanawe Celena ,
" Celena twende nyumbani ,"
Celena akawa anamshangaa tu maana hata yeye hamjui , " we celenaaa twennde nyumbani ," alijalibu kuita tena lakini ndio kwanza Celina akamfuata mama yake yule kichaa na kumkumbatia huku alimtoa eneo lile ili asije akarusha jiwe lingine ,
" Huyu mtoto vipi mbona anajifanya hanijui , ? Aliwaza Mr Benson huku akiondoka eneo Hilo ,
Sasa kumbe Celena kule alikojificha alisikia kila kitu na hata gari ya baba yake ilipopasuliwa kioo aliona na akaamua kuondoka upesi eneo Hilo Sasa ile anafika nyumbani tu na baba yake ndio anaingia , kwanza baba yake akasimamisha gari akawa anamshangaa ," huyu mtoto vipi jamani amefikaje hapa na nilimwachia kule ,"
Aliwaza Mr Benson huku bado akimshangaa Celena ,
" Shikamoo baba ,"
Celena alimsalimia baba yake lakin baba yake badala ya kuitikia akawa anamshangaa tu , yaani Celena na Celina hawajapishana kitu ,alimkagua Kama ataona kasoro yoyote lakin hajaona ,
"Mmh haya maajabu ya Dunia ,"
Aliwaza Mr Benson,
KUMBUKA story hii utaipata yote mwanzo mwisho kwa elfu moja tu,0655772653 njoo whtsap,
Itaendelea.