Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
23 Sep 2025
30 views
VYOTE NDANI GONGA94
BABY MAMA VS WIFE Episode 2 Kemjei alikaa nnje ya nyumba ya Tafon, akisubiri arudi nyumbani ili ampe mahitaji ya shule ya mtoto wao. Ndani ya nyumba, mke
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
wake Natasha alikuwa hawezi kukaa sawa, moyo wake ukichemka kwa hasira.
“Akiingia tu,” alijiambia, “nitaona kama kweli atanitimiza ahadi ya kunirudisha shule au atatumia pesa zote kwa mtoto wa huyo mwanamke.”
Tayari hali ilikuwa ngumu sana kwa Tafon. Hakuwa na pesa za kutosheleza pande zote mbili. Alimpenda sana mke wake na alitamani amani katika ndoa yake. Lakini pia alimpenda mwanawe mdogo mtoto aliyezaliwa kabla hajaoana na Natasha. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba mke wake hajawahi kupata ujauzito tangu wao kuoana, na wote walikuwa wakiomba na kutumaini kupata mtoto.
Bila kujua kinachoendelea, jioni ile Tafon alitembea kimya kuelekea nyumbani. Hakujua kabisa kwamba mama wa mtoto wake tayari alikuwa amekaa nnje ya nyumba yake, akiwa na mwanae pembeni, huku mkewe naye akisubiri majibu ndani.
Mara alipofika tu, Kemjei alinyanyuka haraka.
“Asante Mungu, hatimaye umefika,” alisema kwa ukali.
Tafon akashangaa. “Kemjei! Wewe unafanya nini hapa?” Sauti yake ikatikisika kwenye kuta zote nnje ya nyumba.
Mama wa mtoto wake hakupoteza muda. “Mtoto wetu lazima aanze shule mwaka huu. Nimekuja kuchukua hela za ada na mahitaji yake.”
“Tafadhali nenda nyumbani,” Tafon akamnong’oneza kwa wasiwasi. “Nitakuja kukuona baadaye.”
“Niko hapa sitoki,” Kemjei akajibu kwa msisitizo. “Umekuwa hupokei simu zangu. Shule inaanza baada ya siku chache. Watoto wengine wataenda darasani na mtoto wangu abaki nyumbani? Kama bado unataka Fanka ajulikane kama mwanao, basi tatua mambo yake sasa hivi.”
“Hii siyo sehemu wala muda sahihi,” Tafon akaomba, macho yake yakielekea mlangoni.
Kemjei akatabasamu kwa dharau. “Unaogopa tu mke wako akinisikia. Hebu nikwambie, tayari aliniona.”
“Nimekuwa na ndoa naye miaka miwili sasa,” Tafon akajibu kwa kujitetea.
Kemjei akatikisa kichwa. “Lakini mimi nilikuwa nawe miaka minne iliyopita. Wakati wa kuoa uliniacha na ukaenda kumuoa yeye. Yeye bado hana mtoto, lakini unadhani ni bora kuliko mimi?”
Moyo wa Tafon ukaanza kudunda kwa kasi. “Lakini uliwahi kuniambia huwezi kuolewa na mwanaume masikini kama mimi. Nilitegemeaje kukutunza wakati huo?”
“Ulinidanganya,” Kemjei akamrushia maneno. “Ulinifanya niamini wewe ni mfanyabiashara mwenye mafanikio, kumbe ulikuwa unanichezea tu. Sasa shughulika na matokeo ya matendo yako. Mwanangu lazima aanze shule Jumatatu kama watoto wengine.”
Wakati maneno yake yanaendelea kama moto, ghafla Natasha akatokea nje. Alisimama mlangoni, akiwatazama kwa macho makali.
“Mume wangu,” alisema kwa sauti thabiti, “kama kweli bado unajali ndoa yetu, muache huyo mwanamke na uje kwangu, kwa mke wako.”
Lakini Tafon hakusogea. Kabla hajajibu, mama wa mtoto wake akamvuta shati kwa hasira.
“Wewe hutoki hapa mpaka umetoa pesa za shule ya mwanao,” alitangaza.
Uwanja wote ukawa kimya, utulivu mzito ukatawala, isipokuwa macho ya yule mtoto mdogo yaliyokuwa yakimwangalia baba yake kwa upole. Akiwa katikati ya wanawake hao wawili aliowapenda kwa namna tofauti na kwa kipindi tofauti, moyo wa Tafon ulizama zaidi kwenye machafuko.
Itaendelea...
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
FROM BANGI TO BABY 💞💘 SEHEMU YA 5
Basi akanivuta kwa mkono mmoja akanibana kwenye kiuno chake baada ya salamu hapo kanipiga ma busu kama yotee halafu nje...
BABY MAMA VS WIFE Episode 2 Kemjei alikaa nnje ya nyumba ya Tafon, akisubiri arudi nyumbani ili ampe mahitaji ya shule ya mtoto wao. Ndani ya nyumba, mke
wake Natasha alikuwa hawezi kukaa sawa, moyo wake ukichemka kwa hasira.
“Akiingia tu,” alijiambia, “nitaona kama kweli atanitimiza ahadi ya kunirudisha shule au atatumia pesa zote kwa mtoto wa huyo mwanamke.”
Tayari hali ilikuwa ngumu sana kwa Tafon. Hakuwa na pesa za kutosheleza pande zote mbili. Alimpenda sana mke wake na alitamani amani katika ndoa yake. Lakini pia alimpenda mwanawe mdogo mtoto aliyezaliwa kabla hajaoana na Natasha. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba mke wake hajawahi kupata ujauzito tangu wao kuoana, na wote walikuwa wakiomba na kutumaini kupata mtoto.
Bila kujua kinachoendelea, jioni ile Tafon alitembea kimya kuelekea nyumbani. Hakujua kabisa kwamba mama...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/baby-mama-vs-wife-episode-2-kemjei-alikaa-nnje-ya-nyumba-ya-tafon-akisubiri-arudi-nyumbani-ili-ampe-