FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 4
Nikashuka kwenda kuchukua maji wakati nageuka kuondoka nikakutana uso kwa uso na yule kijana sasa, Moyo paah aibuu yaani nimekuwa naona aibu muda wotee kama nimejinyea jamani daah
Akanipita kama hanijui nikajisemea sijui kanisahau.? Ila sio kirahisi hivyo weweee yaani awe amenisahau mmh
Nikajikaza huyooo, nikamgeukia mana alikuwa ashanipita yupo dukani nikapiga hatua kadhaa nikarudi mpaka alipo "kaka asante .. lakini pia naomba unisamehe kwa ile changamoto pale naomba sana unisamehe"
Akageukaa !! Akanikazia macho halafu akacheka kwa kupindisha tu mdomo pembeni "usijali sister kuwa na amani, Mitaa yetu haina wizi kabisa vijana wote wanajishughulisha kwahiyo unakaribishwa sana" nikashusha na pumzi maana kaniongelesha vizuri kweli sio kama mara ya kwanza ..
"Asante!!..."
Nikaachia tabasam dogo tu la aibu, wakati natembea kwenda kwenye gari nilihisi bado ananitazama ila sikuthubutuu kugeuka .
Nikaingia kwenye gari kwanza nikashusha pumzi nzito huku nimeshika kifua, Nikafungua maji nikapiga funda tatu za faster faster nikafunika nikaeka pembeni kabla sijawasha gari nikageuza shingo kumtazama yule kijana nikamuona anaenda kwenye Honda moja kubwa ilikuwa imepaki pembeni akaiwasha baada ya kupanda ilikuwa kubwa nae alivyopanda ilimpendeza hatari ....
Nikachukua simu nikapigia Shoga angu Tinner
"Si nimemuona yule kakaa.... hahaha yaani sijui kwanini namuogopa jamani aah .... hahah Tinner bwana ile li zuriii .... hahaha acha ujinga na D wangu jee akhaaa ....aaaaah siwezi hamna bwan huyu kaka unajua sijui yupoje ana muonekano wa pekee sana nimempenda ila sio kimapenzi we mjinga....... hahaha acha ujinga bwana weeee baadae mie ngoja niende nyumbani bwana we baki na wahuni wako mwenzangu nyumba za bure hahah poleeee.... kwaheri bwanaaa."
Nilikata simu maana Tinner alikuwa ananiletea mada zingine et aniunganishie huyo kaka anaona nimesha fall kwenye penzi mmh aah wapiii nimempenda tu mwonekano wake una vutia ila sio kama mpenzi hapanaaa ... Nikawaesha gari nikasepa zanguuu kwanguu ...
Nilipo fika nyumbani nikawa bize kuandaa andaa mazingira kwa ajili ya kesho kazini huwa napenda sana kuandaa nguo zangu mapemaaa kila kitu kiwe sawa ...
Mpaka usiku sikuwa hata nimemtafuta Tinner, nikainuka nikaenda kuoga. Maji ya moto yakashuka juu ya mabega, nikavuta pumzi ndefu. Aibu ile ya asubuhi mdada kama mie kushushuliwa vile ilianza kupungua, nafasi yake ikachukuliwa na mwonekano wa yule kaka jinsi alivyo mzuri ana muonekano mzuri afu anavuta ma bangi vile mmh,
Haya bwana nilipo toka kuoga nikajitupa kwenye kochi, Ndio nikashika Simu, kufungua nikakutana na ujumbe wa Tinner.
βUmefika salama? Au bado uko njiani unamfikiria βkaka Hondaβ?β
Nikacheka peke yangu
βAcha ujinga wewe. Nimfikirie wa nini sasa"
"Hayaa jibu, umefika salama "
"Ndio bwana, nilikuwa bize bizee mwaya ndo mana sikukutafuta haya mie nalala unajua kesho naingia asubuhi"
"Hayaa usiku mwemaaa " ..
Nikaingia zangu kulala, Hiyo siku ilikuwa ndefu kwangu na matukio ambayo sikuwi kuwaza ipo siku nitapitia, ile siku ikapita hivyoo ...
Asubuhi niliamka nimeshasahau yote ya jana nikaanza siku mpyaa yaani habar za wale vijana wajinga wote kwangu zilifutika, nikaingia kazini ...
Sasa tangu ile siku niende kwa Tinner ilikuwa imepita kama wiki hivi maana w/end moja tu ndio ilipita .
Boyfriend wangu mimi Alikuwa amesafiri karibu mwezi ulikuwa umepita ni mtu ambae yupo bize sanaaa yaani bize huwa anatumia muda mchache sana na mie mchache mnoo ni mtu wa kusafiri sana nje ya nchi , Asubuh akanipigia simu akanambia amekuja yupo home, Waooo nilifurahi sanaaaa sikuwa na sehemu ya kwenda nikaona acha W/end yangu leo ikaishie kwa babyyy , wakati najiandaa akanipigia simu akanambia
"Babyy.... Samahani mpenzi wangu gari yangu moja imepata shida hapa.ndio nataka kuelekea huko nipo na kijana wangu ambae ana iendesha amefika hapa sasa hivi ndo kanipa hizi taarifa "
"Shida gani??" Nikamuuliza huku nimeishiwa hamu mana nilijiandaa kumpa mauono feni Hatari
'"Wamezuia mzigo wangu ngoja nikafatilie ila napita hapo kukupa zawadi zako, Nikimaliza tu mambo yangu utakuja"
Nikasema sawa...
Nikatulia nyumbani kusubiri zawadi, huwa ana magari makubwa haya yanasafirisha mizingo nje ya nchi ana magari mengii makubwa haya malori mengi hata sijui mangap ila ni mtu wa business sanaa nayeye ndio kila kitu kwangu ...
Basi bwana kama saa moja hivi likapita nikasikia piki piki nje ya geti, kabla sijainuka simu yangu ikaita honey ndio anapiga , nikapokea chap akanambia njoo nje mana siwezi kuingia niko na mtu hapa, nikasema sawa nikainuka mbio mbio, na vile nilikuwa nimem_miss nilijipanga nikifika namkumbatia nampiga ma busu kama yoteee ...
Ile nafungua geti nilikutana na bonge wa Surprise aiseee mpaka miguu ikawa mizito gafla kuvuka geti lile tabasam lote likapotea ..
D alikuwa yupo pamoja na yule kaka mvuta bangi aah weee sijui kwanini nikajikuta yaani ile kujiamini kunaisha koteee ..
Nikajikuta nagongana macho na yule kaka nikakwepa haraka nikawa naangalia taili la Honda yake alikuwa na ile ile Honda inampendeza hatari na hivi limakaka li refuu ila wakaka warefuuu aisee mpo romantic sanaaa sema tu hamjijui hata wafupi jamani msije kunipopoa mawe n nyie mnanafasi yenuu So mwaah ila leo nitaongelea hawa warefuu maana ndio walio nikunaaa haswaa hahaha ...
Basi D akaja akanivuta mweeh akanishika kiuno akanibana kiunoni kwake
"Mrembo wangu ... nilikukumbuka sana ujuee" mie nacheka chekaa kama mwehu naona aibuuu naiba iba kumtazama yule kaka hana hata habari na sie anatazama ki vyakeee
Itaendelea....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
