FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 12
Nilijitetea kwelii japo nilikwangua ka_akiba kangu ila niliona aibu sana kurudishiwa ile pesa aah nikasema acha nilipwe na Mungu tu ..
Akanibembeleza sanaa nikakataa wakati naondoka akaniomba namba ya simu nikawaachia namba yangu mie nikasepa zangu, yaani nipo hoi na kuuguza Tinner ananicheka tuu yaani duh.
Asubuhi nikaingia kazini kama kawaida bwana halafu sasa leo tena nilichelewa sanaa yaani nilichelewa mpaka basi, nikapishana na ile familia ndio inatoka muda huo mie niko hai haiii
Yule wa kiume akawa ananifata mbio ananiita "dadaa, Dadaa!!'" Nikageuka haraka
"Dadaa kaka anataka kukuona hatujaondoka tulikuwa tunakusubiri" Daah yaani nilikuwa nimechelewa mnoo
"Mdogo wangu mwambie kaka nimechelewa sana kwahiyo mpe salam zangu, Ipo siku tutaonana nae sawaa'" niliongea haraka haraka hata sikusubiri jibu lake mbio kwenda ku saini aisee naweza fukuzwa kazi hivi hiviii ..
Nikaingia kwenye majukumu yangu mpaka mchana yaani hata muda wa Lunch sikuwa nimeupata kabisaa, na siku enyewe kukawa na wagonjwa kibaoo mpaka jioni namaliza zamu jamani jamani jamani mgongoo inauma njaa yaani nipo hoii namwambia Tinner yaani pika chakula kingiiii nilikuwa na njaaa hatari afu hela ya kula sina nilikuwa nimefulia wee haha jua kali na hivi D ndo hatuuelewani akasitisha huduma kabisaaaa kwanza anavyonikera sasa hivi yaani hata kumuongelea nasikia hasiraaa ..
Basi jioni ile natoka nikapita pale ku_ sign out, Wakati nipo na Sign Nesi ananambia kuna watu wapo mapokezi tangu asubuhi wanakusubiri wewe wamekaa muda kweli yaani tumeshinda nao
Moyo ukafanya paaa!! Jamani asije kuwa yule mama na watoto wake jamani mie hadi nilikuwa nimesha wasahau nikamuuliza ni mmama akasema hamna mkaka tu hivi handsome handsome yupo na kivulana kile kilikuwa na mama yao humu anaumwa .
Hee!!! Mpaka nikashangaa kwahiyo huyo kaka amekaa anasubiri kunilipa pesa au kusema asante jamani, kwanza nikacheka nilivyosikia et handsome hahah ..
Ikabidi nielekee huko kuwaona hapo nawaza jinsi gani nitazikataa hizo pesa akinirudishia hahaha japo sina hela nimekaukiwa lakini inabidi tu nikatae si nimechagua thawabu bwanaaa hahaha hakia Mungu Uchamungu kaziiii hatari , Yaani nilikuwa natembea huku napanga maneno akisema dada hizi hapa pesa zako mmh nasema aah hapana kaka hapana afu nijichekeshe chekeshe hapo niondoke akiwa hajaja kunilipa kaja tu kunishukuru namwambia sawa kaka tupo pamoja bwana usijali huku nacheka cheka mmh mbona hatari...
wakati ndio nakaribia mapokezi nikavuta pumzi ndefuu, nikajikazaaa hatari nikaweka uso wa mbuzi kavu we ile natokeza tu nikasikia sauti ya mtoto yule wa kiume
"Kakaaa Doctor huyooo" mweeeeh kaka yake si ndio akageuka kutazama upande nina tokeaaa hamadii macho kwamacho na Veda, Aisee Dunia ndogo au ndo inazunguka kila mara ni huyu kaka tuuuu khaa..
Ni kitendo cha sec tu mwili wote ulitetemekaaa halafu ni muda mrefu sijamuona wala kusikia habari zake na nilikuwa nishaanza kumsahau japo kichwani picha yake iligoma kutoka ..
Ni kama wote tulipigwa na bumbuwazi, ni kama muda ulikuwa umesimama kupisha macho yetu yatazamane, Veda alibaki kasimama kama sanamu mkono mmoja aalikuwa ameshika soda hata yeye hakutegemea kukutana na mie kabisa
"Dadaa, kaka alitaka kukuona, ndo maana hatujaondoka"
Nikageuka chap kama umeme nikaanza kupiga hatua kuondoka haraka, kabla hata sijamaliza hatua ya tatu akaniita
"VEROOO....." OOOOOH hii ndio ilikuwa mara ya kwanza kusikia huyu kaka akiniita jina langu jamani ana sauti nzuriii, Nikashangaa mguu hauinuki kupiga hatua, nikabaki nimesimama moyo unaenda kasiii sauti ya Veda ilikuwa inarudia rudia kwenye maskio yangu inagonga mpaka kwenye ubongo jamani mweeee, Sauti ilinichoma mpaka kwenye moyoo nikasikia nimesisimkaaa, nikajikaza nikavuta pumzi ndefu, Ile nataka tu kuondoka akanivuta mkono nikajikuta nimegeuka bila kupenda halafu yupo hapa mbel yangu aloo mkaka mrefu yaani mpaka niinue uso kumtazama ..
"Ah, Vero...tunatakiwa kuongea tafadhari!!"
"Sina cha kuongea nawewe!!"
'"Please...tuache yote yaliyotokea tusahau tuongelee hili la mama yangu siwezi kujifanya sioni kitu wakati natakiwa hata kusema asante nikiwa nimepiga magoti..."
"Veda ... nilifanya as a doctor na sio vingine tafadhali usinielewe vibaya " nikauvuta mkono wangu
"Bonny embu kanisubiri kwenye piki piki..." akamtoa mdogo wake, Dogo akatoka yaani mwenyewe hata haelewi hivi
Sijui kwanini nilikuwa najisikia hasiraaaa yaani sielewi mana kuna upande namchukiaaaaa Veda lakini akitoka kwenye macho yangu namkumbukaaa afu najuta hata sijui kwanini ...
"Veda achana na mie tafadhali " sikutaka kabisaa kuongea nae, nae akawa ananifanya nyuma ananiimbisha nimsikilize kwakweli sikutaka hata kumpa nafasi..
Wakati natoka getini akanivuta kwa nje halafu akanibana ukutani yaani waswahili sijui wazungu huwa wanasema Zero distance, nikajikuta nameza mate kwa pupa nusu nipaliwe ananukia ki harufu kizuriiiiiii waoooh yaani Veda mweeh nikajikuta naona wivu hao wanawake zake wa kule Cassino jamani daah kwahiyo huwa wanalalia hili jifua la Veda nae huwa analala na wanawake wawili wawili aaaah haaaa nilijikuta et machozi yanatokaaa hapo hajaongea kitu tunahemeana tu...
Nikasikia "kuna nini hapo!!!??" Wee nilishtuka maana hii sauti sio ngeni kabisaaa
Itaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni