FROM BANGI TO BABY ππ SEHEMU YA 5
Basi akanivuta kwa mkono mmoja akanibana kwenye kiuno chake baada ya salamu hapo kanipiga ma busu kama yotee halafu njeee hapo sema mitaa nayoishi ushua mwingi sana ..
Akanambia "vero .. huyu Veda ni kijana wangu anasimamia gari zote namuamini sana lakini pia ni dereva wangu wa muda mrefu sanaa huyu ......Veda huyo shemeji yako Vero leo imekuwa kama bahati mmekutana hivi " mie nikacheka cheka tu, Huyo Veda kama hanijui babaa!! Alinitazama juu mpaka chini hata salamu hakunipa akatazama pembeni haya bwana sikupenda pia ..
D akanipa begi lilikuwa kuwa hilo akanambia humo kuna zawadi zangu yeye anawahi nikasema sawa kinyooonge yaani mood yoote iliisha baada ya kumuona hapo Veda nishajua jina lake anaitwa Veda, nimeingia ndani akili inaita Vedaa ..
Nikampigia shoga angu Tinner nikamuhadithia kumbe yule kaka mvuta bangi anajuana vizuri na D na ni msaidizi wakee eeh basi tukabaki tunashangaa wote hapo, mana hata kwangu ilikuwa surprise kubwa ndo mana watu wanasema usimdharau usie mjua aisee leo nimeamini basi bwana hicho kitu kilikuwa kigumu sana kutoka kichwani ...
Nikafungua zawadi zangu aloo heheh ngoja kwanza nicheke kupendwa si ndio huku bwana, mamaaa nilikuwa nimeletwa pochiii sio pochi za afu kumi kumi Tandika sijui ilala Nooo!!! Pochi expensive wazungu wanasema viatu mamaa sio vya wahaaa vya afu tano tano kariakoo Hapanaaa!!! Viatu high quality mamaa!! Hizo nywele za wazungu jamani vi nguo ki sister duh heheh nikamtambia shoga anguu hatari, Mungu kanipa mwanaume wa maana kabisa huyuuu ..
Nakumbuka mpaka Usiku D hakuwa amenitafuta kabisa ikabidi nimpigie simu, nikawa nasikia kelele kelee simu inakatwa nikamtext "kwani upo wapi jamani mbona hivyoo!??"
Akanijibu "nipo sehemu najipooza na machungu ya kazi vipi unataka kuja??" Khaa nilisikia hasiraa ila nikajikaza yaani kaona kujipoza na kazi ni bora sana kuliko miee, Nikasema "ndio"
Akasema " request hapo njoo mpaka The land ni kasino ipo Morocco " duh haya mambo ya kasino tena jamani mbona mapya kwangu ila kwakua nimemkumbuka sana D wangu na hapo hakawii kukuambia hata kesho kuwa anasafiri .
Ikabidi niite usafiri tu niende huko huko, nikafika mpaka nje hapo ya hilo cassino kubwaaa kama kwa wazungu, nikampigia simu hakupokea akanitumia ujumbe ushafika nikasema ndio akasema okay namtuma mtu Akufate, basi nikajitengeneza vizuri hapo nimependeza mama weee hatari nawakaa nimevaa viwalo vipyaaa mtoto wa kike na ka wigi kangu so mwaah yaani nimewaka ...
Akanipigia simu akanambia simama karibu na hilo bwawa hapo ili akuone nikasema sawa kweli nikasogea karibu na hilo bwawa la kuogelea nikachukua simu nachat na udugu wangu Tinner hapo nishapiga picha kama zote mie mitiko ya hivi hata sijawahi nakutana na D nyumbani kwake basi .
Nikashtuka mtu amenisogelea karibu kuinua macho sa ngap nisimuone huyo sijui ndo Veda eeeh huyu tenaaaa heee!!! Nikaishiwa pawa kwakweli kaa!! Akasema nifate sauti kavuuu nene nzitoo, duh mpaka miguu ikaanza kukongana anatembea harakaa jamani mie nakiatu kirefu sijui alitaka nianguke daah ..
Tukaingia humo ndani nikamkuta D amekaa kwenye meza imejaa Pombe kali machupa makubwa makubwa, wanawake humo jamani jamani jamani Kuna mtu anasema et wote tutachomwa moto sawa?? Hapana jamani moto unazidiana mie kweli nina dhambi ila nilivyokutana na hawa wanawake walio jaa laana humu ndani wooiii niliishiwa pawaa !! Uchafu unaofanyika kwenye makasino jamani loo mungu atulindie vizazi vinavyokuja maana ni hatari ..
Basi nikakaa pembeni ya D, Veda nae akakaa pembeni akachukua kipisi cha Bange , D akamwambia "Mzee ya ngapi hiyo?? Ipo siku utaamka akili unaziacha kitandani " Veda akacheka kidogo yaani kidogo kama tu hajachekaa mana alisogeza tu mdomo pembeni afu akaweka ki Bange chake akaanza kupuliz wanawake wapo matako nje njee wanakuja kuhudumia mie naona aibu kuna wengine wanacheza pale mbele wapo uch mweeh watu wana enjoy kuna wacheza kamali yaani kila aina ya michezo haramu ipo mule nilijikuta sina amani tena ya kukaa hapo nasema hapana jamani hii sio Tanzania yanguu jamani mbona sijawahi hata kusikia haya mamboo ...
D akanimiminia Pombe akanambia kunywa hii mamaa!, nikasema mie hapana hata sinywi akanilazimisha nionje hata kidogo hapana sijawahi nikakataa kata kata akanambia sasa umekubali kuja huku kufanyaje au we unahisi starehe ni moja tu kufanya mapenzi eeh??" Niliona aibuu nikamtazaa hivi ananitania au nikamkuta yupo serious
Akanambia "ukiwa mwanamke wangu lazima ujaribu vyote sawa haya jaribu hii mie si ndio mumeo Nakupa kunywa" akawa ananipa kwa lazima nikasema hapana mie situmii jamani, basi tukawa tunabishana kweli
Mwisho akanambia basi nenda nyumbani nikitoka hapa nitakuja maana hapa sio Bar kusema utaagiza soda na wewe bado kashamba kashamba sana " yaani huyu anae ongea hapa ni mpenzi wangu ambae kila siku ananiahidi kunioa huyu, tuna karibia kufunga mwaka kwenye mahusiano yetu na nina mpenda sana tu ukiacha hela zake mana kanahela za kuoga haka kajamaa ...
Maneno yake yaliniuma ila nikahisi ni ka sababu amelewa tu ndo mana anaongea hivi hajawahi kabisaa kunivunjia heshima ..
Ilibidi tu niinuke kuondoka mtoko ushaingia doa kwanza sehemu enyewe inalaana kibao mie sio vitu vyangu hivi jamani hivi mume wa mtu anawezaje kwenda sehemu kama hii jamani au mie ndo mshambaa??
Akamwambia veda anisindikize sikuwa mbishi Veda akanitoa mpaka nje akaita boda akanilipia kabisa nikamuuliz sasa mnawezaje kuja sehemu kama hii jamani??" Nilijikaza sana uvumilivu mwenzangu ulinishinda, hata hakunipa jibu akanambia Nenda kapumzike"
Akageuka kuondoka zake dah nikaondoka yule boda akawa ana cheka tu akanambia hujazoea eeh, nikasema hata kwa bunduki aisee siwezi kuzoea huu uchafu akanambia kawaida tu wanaume wapenda anasa wakikosa hivi vitu wanaweza hata kufa kwa alosto aisee....
Moyo ukapasuka kwahiyo na D ni mpenda anasa eeh...
Inaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
