FROM BANGI TO BABY ๐๐ SEHEMU YA 15
D alitoka hukoo kasi akataka kumpiga Veda Tinner akazuiaaa nae alitoka ..
"Veda wewe kumbe ni mshenziii eeeh!!" Veda yupo kimyaa ananikata jichoo kaliii yaani hamtazami D anaembwatukia jicho lote lipo kwangu mie aibuu nilikuwa naogopa hapa Veda sidhani kama atarudi tena kazinii hicho tu ndio kilikuwa kinaniogopesha lakini et Kuogopa D kuniona nipo na mwanume mmh hata sikuwa na woga huo ...
"We malaya twende harakaaa nyumbani " akanishika mkono kunivuta aah wapi
"Mie siendii" nikarudi nyuma kwa nguvu mkono wake ukaniteleza
Aliponiona namkazia wee hasira yake ikapanda mara miaa
โUnasemaje weweeeโ akapaza sauti,
"Siendi nawewe"
Akaniinulia mkono Ili anipige Tinner na Veda wote wakawahi Tinner akamzuia
Sijui nilipata wapi ujasiri ule, nikamkazia macho bila kuyumba
โNipige basi, โ nikasema kwa sauti iliyokuwa inatetemeka yaani hasiraaa
โNipigeeeeโ
โD acha ujinga, sitaki ugomvi nyumbani kwangu"
D akanigeukia tena, macho mekundu ya hasira mwenyewe alikuwa anatetemeka
โUnanifanya mjinga yaani unaniacha ndani unakuja hapa kufanya ujinga na mwanaume mwingine tena rafiki yangu hivii Vero unajielewa wewe??"
"Utajua wewe!!"
โUnachezewa na mwanaume nyuma yangu halafu unataka nikunyamaze?โ
Nilicheka kwa uchungu, machozi yakianza kunijaa.
โNyuma yako? Vipi kuhusu wewe na wale wanawake ile siku ulijari hata kidogo kuhusu mimii โ nikamuuliza sauti inatetemekaa
โkwa hiyo huyu mjinga ndio alikukalisha chini akakuambia hayo ili kukujaza kichwa nawewe ukamuamini, Unajua anatumia wanawake wangap kwa siku huyu, embu nenda kwenye kila casino sio tu Tanzania, hata Uganda ujue anajulikana na kila malaya"
Veda alimkata jichoo hiloo akasogea karibu yake
"Aisee.... kama ukishindwa kutengeneza upande wako, Embu sepaa usitafute kunichafua kwa nguvu"
D hakuuliza alirusha ngumii, Bahati nzuri Veda akakwepa uwiii yaani leo mie nagombaniwa tena na mtu na Boss wakee hehehe Nyie haka ka moments rahaa
"Tafadhali sitaki ugomvi kwanguuuuu embu naomba D ondoka Tafadhali ondokaa....Veda Please huu sio wakati sahihi Tafadhali nakuomba kaka yangu"
Yaani Tinner bwana alipo kuwa anaongea na D alifokaa hee hadi na mie niliogopa halafu alipo geukia upande wa Veda mweeh akashusha sauti akaongea kama anambembeleza
Veda akanitazama kwa jicho la kuibia tukagongana macho akanitazama kwa muda kidogo afu hakuongea kitu akaondoka zake akatoka nje ya Geti daah nikajikuta hadi nashusha pumzi, nikaona ngoja niende zangu wakati naingia ndani D akanirushia neno
โBasi kaa na huyo! Halafu tuone unaniletea dharau mie, nimekufanyia mangap wewe unamuona huyo Veda msafiii tuulize sieee tunao mjua weweee"
Hata sikuyajari maneno yake nikafunga zangu mlango nikabaki nasikia tu Tinner anamfukuza D namsikia tu D anasema sitaki anitafute tenaaa kwa lolote ..
Nikajua tu huyu analingia vitu vyangu na anajua nina vihitaji sana sasa atajua mwenyewe mie nishachoka bwana weee ..
Baada ya muda Tinner akaja ndani kama kawaida yake mie nimekasirika yeye anachekaa kweli kwelii
"Yaani Tinner niache huu hata sio Muda wa utani, kwanza unisamehe kuleta matatizo nyumbani kwako"
"Hata usijali shoga angu, Kwakua Veda ndio kaleta matatizo aaah mwenzio nime enjoyyy hatari "
Nikatabasam tu hata hamu ya kucheka sikuwa nayo
"Enhee una mpango gani sasa"
"Hata sijui kwakweli akili naona imesimama sijui nitapata vipi vitu vyangu yaani hapa Nishaaribu kila kitu "
"Embu tulale pakikucha tutapata jibu, halafuu na Veda ndo nini kumtunishia vile kifua boss wake jamani si atafukuzwa kazi yulee??"
"Yaani Tinner nilivyo chokaa hakia Mungu sitaki kufikiria chochote yeye ana yake na mie ninayangu atajua mwenyewe "
"Hayaa tulale shoga"
Usikuu aisee ulikuwa mrefuuu wenye mauza uzaaa kibaooo kifupi sikupata usingizi kuna muda nilijikuta tu namuonea huruma Veda mbona amejiharibia kazi kwa sababu yangu ..
Itaendelea....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni