CHIMBA CHA MPANGAJI SEHEMU YA 28,
CHIMBA CHA MPANGAJI SEHEMU YA 28,
ILIPOISHIA.....
"""" Nasraaaaaa!!! Nikikushika nakuuua mjinga weweeee....
Aliongea Rehema huku analia na kufungua mlango wa gari lake..
Rehema aliondoka pale kituoni akiwa kama amechanganyikiwa...
Alifika katikakati ya mji na kupaki gari kwanza huku anawaza ni upande gani aende..
Alisoma mshale wa mafuta ya gari ulikuwa umeshuka sana..
Aliamua kupitia sheli na kujaza mafuta,
Taratibu alieondoa gari lake kuelekea nyumbani alipouacha Mwili wa mama yake saidi..
*****
Rehema alifika na kukuta geti lipo wazi ikimaanisha kuna gari liliingia mule ndani muda si mrefu,
Alishtuka sana Rehema na kupaki gari lake njee kisha yeye kuingia ndani kwa kujihami akiwa ameshika silaha yake mkononi..
Alifika na kusukuma mlango wa sebuleni kisha kuingia ndani.. Alitazama kila pande na kuona matone tu ya Damu lakini mwili wa mama yake Saidi haukuwepo..
"" "" Mungu wangu... Huu mwili umeenda wapi tena jamani...
Aliongea Rehema kwa mshtuko huku ameshika mdomo wake..
""" Kama kuna mtu humu ndani ajisalimishe upesi....
Aliendelea kuongea Rehema kwa hofu huku anatetemeka sana...
Rehema alipiga hatua hadi kwenye mlango wa kingia chumbani kwa saidi,
Aliusukuma na kuingia ndani, alitazama kila pande na kukuta kupo sawa tu,
*****
Alitoka na kwenda kwa Nasra....
Alisukuma pia mlango kwa hukihami na Hofu nyingi sana...
Aliingia ndani akiwa ameitanguliza bastola yake..
Alitazama kila pande lakini hakukuta kitu chochote mule ndani..
Chumba kilikuwa cheupe utadhani hakukuwa na mtu aliewahi kuishi mule ndani.
****
"" " Au huyu binti ni jini jamani.?? Aliwaza Rehema huku anatetemeka na kuufunga ule mlango wa Nasra...
Alienda kwa Saidi kisha kufunga mlango pia..
****
Alifunga na Mlango lwa sebuleni kisha kutoka na kufunga geti...
Alichukua funguo zote na kuondoka nazo..
Rehema alienda kwanza nyumbani kwake Area C na kuoga kisha kubadili nguo..
Alivaa Top Nyekundu na Skin-jeans ya blue kisha kuweka nywele zake sawa na kutoka kwenda maeneo ya Starehe kwanza kupeleleza kama angepata habari zozote kuhusu tukio..
Mara nyingi wahalifu baada ya tukio huwa wanakimbilia sehemu za Sterehe. Alimini lazima huko angepata tu taarifa zozote...
******
Baada ya Rehema kutoka tu nyumbani kwake, breki yake ya kwanza ilikuwa ni Royal Vilage ambapo kulikuwa na Live band kwa usiku ule..
*****
Baada ya Kudifa, Rehema alipaki Gari na kujiweka sawa kisha kuingia ndani...
Rehema alienda kaunta na kuagiza Chupa ndogo ya konyagi na Soda aina ya Siprite, ilikuwa ni soda baridi ili kupunguza makali ya pombe ile..
Alipewa na kulipia kisha kwenda kukaa kwenye kona huku anatazama bendi na mazingira yalivyokuwa....
****
Rehema alimimina unywaji wake kwenye glass na kuanza kunywa taratibu..
Baadhi ya watu walianza kumtazama Rehema wakishangaa ni Binti wa namna gani anakunywa konyagi kwa kujiamini kiasi kile...
Konyagi ilikuwa ni pombe kali mithili ya Gongo, ni nadra sana kuona binti akinywa pombe kali za namna ile.
*****
Kuna mtu mmoja alikuwa amekaa pembeni,
Baada ya kumuona tu Rehema, yule mtu alishindwa kuangalia Bend na kujikuta anamtazama tu Rehema..
Rehema pia alijua hilo na yeye pia alianza kumuangalia yule kaka kwa jicho la kuibia...
******
Yule jamaa alimuita muhudumu na kumnong'oneza huku akimuonyesha upande alipokuwa amekaa Rehema..
*
Baada ya kuelekezwa, yule dada alijiweka sawa na kwenda kumfuata Rehema..
****
"" " Dada Samahani.. Kuna yule kaka mwenye Shati ya Draft kaniagiza, anasema kama hautojali anaomba aje kukaa na wewe meza moja au unae mgeni unamsubiri.???
Aliongea muhudumua huku anamtazama Rehema..
" "" Bila shaka.. Mwambie aje tu, alijibu Rehema na kujiweka sawa...
****
Muhudumua alitabasama n kurudi kwa yule jamaa..
Alimuelekeza na jamaa alitoa noti moja ya Elfu kumi na kumpa muhudumu kama Asante..
***
Yule jamaa aliinuka na kwenda kukaa pembeni ya Rehema na kumuagizia konyagi nyingine kichupa kidogo kama kile cha mwanzo...
Aliagiza na kuku mzima wa kuchomwa kisha kuanza kupiga story na Rehema..
*******
"" " Dada, kwa majina naitwa 'Leonidas Msechu'.. Sijui wewe unaitwa nani Dadaangu..
Aliongea yule kaka
" "" Mimi naitwa Rachel Marco
Alijibu Rehema akidanganya jina lake.....
"" " Unajina zuri sana pia nimevutiwa na unywaji wako dadaangu..
Unajiamini sana na upo mwenyewe alafu unakunywa vinywaji vikali kiasi hiki, je ukizidiwa nani atakupeleka nyumbani??
Aliongea yule kaka..
*
" "" Hahhaahahha.. Ni kawaida tu, mbona huwa nakunywa lile kubwa na silewi.. Nimeanza kunywa muda mrefu sana ndio maana hazinipi shida..
Nakushangaa wewe mwanaume unakunywa Serengeti Lite, unalewa kweli au umekuja kupoteza muda.???
Aliongea Rehema huku anatazama sana Shati la yule kaka baada ya kuona matone kama matatu ya damu kwenye sehemu ya shati upande wa kushoto mwa kifua cha yule kaka....
"" "
Hapana bana.. Mimi nakunywa sana tu sema hapa nimeanza tu kulainisha koo.. Na leo nimepiga dili la pesa ndefu sana kwahiyo nipo tayari tunywea na ikiwezekana tuondoke pamoja tukatulie sehemu dadaangu au unasemaje.???
Aliendelea kuongea yule kaka...
.....
""" Kwani umepiga dili gani.??
Alidakia Rehema kutaka kujua kiundani zaidi.. Alishaanza kuhisi huenda kuna jambo anajua yule jamaa..
Dodoma ni mji mdogo sana ni rahisi kwa mhalifu kukamatwa kwa muda mfupi tu...
*****
"" " Hahaahha.. Ni dili za kiume tu, mtoto wa kike hupaswi kujua bana..
Wewe unatakiwa kula pesa tu, hutakiwi kujua zilipo toka..
Aliongea yule kaka..
" "" "
Hahahahahah. Jamani we kaka. Lakini kweli, wadada kazi yetu ni kula tu kwasababu hata kutafuta pesa hatuwezi acha tudange tu..
Aliongea Rehema na kufungua kichupa kipya cha konyagi kwasababu kile cha mwanzo alisha kimaliza..
Alimimina kidogo kwenye glass yake na nyingine alimimina kwenye glass ya jamaa kisha kumchanganyia na bia...
INGIA KWENYE CHANEL SOMA YOTE MWANZO MWISHO BURE CHA KUFANYA BONYEZA HAPA KWENYE LINK KISHA FOLLOW
https://whatsapp.com/channel/0029VaArYXf1NCrOwbZvYu2x
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni