MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 19 - 20
Nikamuonesha mume wangu ile sms akaanza kucheka, kisha akasema “Huyu itakuwa anaota, embu twende akatupeleke kwa huyo mzee…
“Na vipi kuhusu mtoto, maana simuamin sana shangazi yangu, nataman asijue kama nimejifungua…
Mama yangu atakuja kukaa nae, na hapo mtoto alikuwa ana miezi kama nane, kweli mama yake akaja kukaa na mtoto wangu tukaenda mpaka nyumban kwa shangazi, tukamkuta amedhohofika sana, mpaka alikuwa anatia huruma…
“Shangazi tumekuja kukusalimia na utupe habari za Yule mzee anataka arudishiwe mahari shilling ngapi, na gharama zake? Nikauliza…
Namna shangazi yangu alivyomuigizaji akaanza kulia kisha akasema “Sikutegemea kama mngekuja, mzee ame kuja kunisumbua sana, si unaona hata tv sina, nimeuza ilinikulipie deni mwanangu, kama una hela hata kidogo nipe nimrudishie mzee wa watu, maana alikugharamia sana, alafu mwanaume anakuja kukuchukua bila kukutolea hata mia…
Nikatabasamu kisha nikamuambia “Unaweza ukanipeleka kwa huyo mzee, nikaongee nae, na kama anakudai nikamlipe ili asikusumbue tena…
“Haumjui Yule mzee mwanangu ni mtu katili sana, sitaman uende ukaonane nae, asije kukufanyia kitu kibaya…
Nikashangaa ni kuanzia lini shangazi yangu ameanza kunionea huruma, maana hanaga hio kawaida ya kuona huruma hata kwa bahati mbaya…
Wakati wote mume wangu alikuwa kimya anachezea chezea simu tu bila kusema neno lolote lile, baada ya kama dakika kumi na tano, mlango ukagongwa nikatoka mimi kwenda kufungua, nikashanga nakutana na wajeda wawili pamoja na kijana mmoja akiwa ameshikiliwa…
“Embu sema ukweli, tv ya huyu mama imeenda wapi..
“Huyu mama alienda kuchukua mkopo kwenye tawi langu, na kikawaida huwa tunakukopesha alafu rejesho ni kila wiki, ila hakuwahi hata mara moja kuleta rejesho, ndio tukaja kuchukua tv, akasema yule kijana, shangazi akataka kuanza kujitetea, mume wangu alimkata jicho kisha akamuambia
“Najua haunijui mimi ni nani, ila mtu yoyote yule anamkwaza mke wangu ananikwaza na mimi pia…
Kisha akaamuru Yule kijana aondoke, kumbe wakati anachezea simu, alishaamrisha watu wake waanza kiufuatili hiyo taarifa na majibu ndio yalikuwa hayo…
Basi wale wajeda wakaondoka zao, mume wangu akampa simu, sikuwa najua kuwa alikuwa anampa simu kwa nini, kumbe alikuwa anamuonesha picha za kwake yeye na baba yake, shangazi likamshuka shuu, kisha mume wangu akasema “Ulikuwa unamuongelea baba yangu kama katili, sitokusamehe kwa mara nyingine ukitamka ujinga kama huo, na kingine usije ukathubutu kupiga simu ya mke wangu, maana nikiona namba yako, nakuahidi nitapambana na wewe ipasavyo, kisha akanishika mkono tukaondoka zetu…
Basi maisha yetu yakawa yanaendelea kama kawaida, na tukaja kusikia shangazi amefariki, ila mume wangu hakutaka mimi niende akaenda yeye kuniwakilisha, baada ya hapo maisha yetu yakawa yanaendelea kama kawaida…
SIKU ZOTE KWENYE MAISHA
Hakuna linalodumu, hata kama ukiwa umepitia mema na mabaya kiasi gani, jipe moyo na kujiambia kuwa na hili litapita na siku zote ukiona kunazidi kuwa kweusi jua kunaelekea kukucha…
MWISHO…
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi