REALLY LOVE* *SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE*
cathe alisogea mpaka walipo hapo alishindwa hata kusalimia kiukweli alichanganyikiwa sana hakujua nini hatma ya maisha yake,
""kaa hapo" alisema baba cathe, nae cathe akaketi kwenye kiti
""baba yako amekuja kukuchukua cathe kama kukupenda nilikupenda pia nilikulea na nikakupa kila kitu sasa unaenda kwa baba yako rasmi, sio kwamba nakuchukia hapana nitaendelea kukupenda kama mwanangu, aliongea baba cathe kwa huzuni sana huku machozi yakimtoka alikumbuka mengi sana juu ya binti yake huyo alimpenda sana alimpa kila atakalo roho ilimuuma sana baada ya kujua kuwa sio mwanae aliumia sana.
"ulipo sitakitupa mdogo wangu "eva nitakusamehe makosa yote uliyonifanyia lakini sio kosa hili nakuapia nitakifa nakinyongo nawewe sitakusamehe eva alisema baba cathe kwa huzuni san huku akilia, simanzi na majonzi vilitawala kila moja alianza kulia kwa uchungu sana,
""mume wangu nisamehe jamani mimi" alisema mama cathe huku akilia sana
calor alimfata cathe na kumkumbatia alilia sana hakuamini kama anatengana nae alimpenda. sana mdogo wake.
"japo tunatengana lakini sitakuacha bado wewe ni mdogo wangu mama yetu mmoja nitakuwa nawewe bega kwabega sitakuacha alisema calor huku akimbembeleza cathe ambaye alikuwa analia sana
""najuta kuzaliwa mimi kaka najuta kaka naumia napitia maumivu ambayo hayaelezeki nimekosa seven nimemkosa devi nimekosa ndoa nimekosa maisha mazuri ona naenda kuishi mtaani mimi nahuyu kiumbe nitampeleka wapi kaka" alisema cathe huku analia kwelikweli,
""usijari mwanangu nitajitahidi kukulea usijari utaishi vizuri tu alisema mzee fahad, basi ikabidi mzee fahad aondoke na cathe rasmi, kuanza maisha mapya, familia hiyo iliachana
kihivyo
huku kwa mama seven alikuwa na wasiwasi sana muda wote alikuwa anazunguka zunguka muda wote
hivi hawa watoto watakuwa wapi jamanj yani sikuhizi wamefululiza sana kutoka halafu walivyokuwa washenzi hawasemi wanapoenda washenzi kweli yani kama sarafina muda wote kuzurura tu alisema mama seven huku akilalamika,
muda huohuo akaingia selina akiwa anatabasamu tu muda wote alifika na kumsalimia mama yake ""mjinga wewe ulikuwa wapi muone mikope
yake vile mibayaa" alisem mama seven
"jamani yani mama si uitikie kwanza salamu muda wote kutusema tu alisem selina
"sasa unataka usisemwe muone kwanza sura yake alisema mama seven
""mama jamani hebu niache nipumzike kwanza leo ninafuraha sana" alisema selina
***furaha gani alijliza mama seven
we si umenisema sikwambii hahahhahaha" alisema selina huku akikimbilia chumbani kwake.
**mitoto mijinga hii jamani kha alisema mama seven kisha akakaa kwenye sofa huku akipata kinywaji
muda ulienda nyumbani kwa mama fatuma alikuwa anawasha moto ia aanze kupita matembele ya usiku, mara akatoka fatuma ndani akiwa amenuna sana
""mama Ina sasa hivi sina simu sasa angalia saidi nitampataje wakati aliniambia ikifika saa kumi nimpigie anitumie ela alisema fatuma
""bwana weee toka hapa usinipigie kelele mie kama alitaka kukupa ela siangekupa pale pale umalaya tu ndo unakusumbua sasa ngoja ubebe mimba hapa alafu nitakuonyesha ubabe unaitwaje alisema mama fatuma huku akiendelwa kuwasha moto
muda huohuo akaingia mzee fahad akiwa ameongozana na cathe pamoja na calor, mama fatuma alishanhaa sana ikabidi asimame awatizame vizuri, hakuwafahamu kabisa japo aliwatazama
cathe huyu ndio mama yako wa kufikia nina mwanangu mwingine ambaye wa kwanz akitoka yeye ndio wewe, lakini yeye kuna sehemu yupo nitakupeleka kesho, alisema baba fahima kisha akamgeukia mama fatuma
""mama fatuma huyu ni mwanangu ambaye huwa natembeaga na picha yake nimempata hivi majuzi tu atakuwa hapa siku zote mlee mpende kama unavompenda fatuma, sitaki fujo naomba muishi vizuri alisema baba fahima, mama fatuma alibaki tu kushangaa sana hakutegemea kama mzee fahad atakuwa na mtoto mwingine
sasa mume wangu mbona mambo mengine hatushirikiani unanishtukiza tu lakini alisema amma fatuma kwa kulalamika
""mimi mwenyewe nimempata jana kwahiyo tusilaumiane kwanza niacheni nimechoka nataka kupumzika fatuma mpeleke mwenzio chumbani calor karibu sana hapa ndio nyumbani alisema mzee fahad
""asante baba alijibu calor, basi cathe akapelekwa ndani, muda wote alikuwa anabinua midomo tu hakupapenda mahali hapo hata kidogo
yani hapa ndo niweke begi langu kha si litachafuka alisema cathe kwa dharau, kauli hiyo ilimchekesha sana fatuma akaanza kucheka....
""sasa kama ungetaka usichafuke si ungebaki hukohuko peponi kwenu binti ukijaa hapa uwe na adambu lasivyo utanyooka mxiueeeeee" alisema fatuma kisha akatoka ndani humo huku anacheka sana
upande wa seven na fahima ilikuwa shida sana muda wote walikuwa wanabisha tu fahima hakutaka akae mbali na seven hata kwa sekunde
""nimesema hapa hutoki alisema fahima
""sasa mke wngu jamani ah" alisema seven kwa kuchukia
""bado eee tamka hadi iiii lakini hapa hutoki" alisema fahima huku akiizungusha funguo ya mlango,
""ila hako katoto kataninyoosha kwakweli" alisema seven mara hapohapo simu yake iliita alishangaa sana kauona mpigaji ni cathe
Itaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni