JAMANI NIPE CHANCE KIDOGO Chapter 9 Abisai alikuwa kama mtu akuechanganyikiwa aliwaangalia kwa zamu, alimuangalia Leyla kisha akarudi kumuangalia Leyna
"Abisai unafanya hiki?
Kabla Abisai hajajibu alifika mama Leyna. Wewe kijana kwanini unamfanyia fujo binti yangu, akikosea nini?
Mama naomba hili swala niachie mimi. Alisema Leyna kisha akawageukia watu.
Jamani ondokeni basi hatugawi hela hapa.
Watu walianza kutawanyika lakini Leyla alijuwa bado analalamika kuhusu simu yake.
"Leyla tulia basi, Natuliaje wakati simu yangu imevunjwa na kumbuka simu yangu ni mpya hiyo.
*Najua
"Usonijinsi kwa mkato nataka simu na haya yote chanzo ni wewe Leyna bila shaka huyu ndio mwanaume wako cha wivu.
"Wewe nae sijui unamtangazia nani, si nimemwambia tulia.
Usinifikee kwanza mimi sina muda wa kubishana na wewe naongea na huyu.
Ilianza ugomvi kati ya ndugu mpaka mama yao
akaingilia kati. Sasa mnamgombania wenyewe kwa wenyewe.
amwambie "Mama sema na mwanao mwanaume wangu anipe simu yangu.
"Usijali nitakupa simu yako. Alijibu Abisai kwa upole. Leyna alimshika mkono Abisal wakawa
wanaondoka pale.
Wewe Leyna naomba nimfukuze nyumbani nakuja sasa hivi. Alisema mama Leyna. Sawa.
Walipofika mbele kidogo Leyna alisimama.
"Abisai umeona madhara ya wivu wako? "Hukuwahi kuniambia kama una ndugu unae
fanana nae
Yule ni pacha wangu anaitwa Leyla na mimi Leyna.
"Uuuuh leo nimefanya kosa kubwa sana.
"Nilikuwa natamani sana hili litokee na leo kama imekuwa bahati leo nimelishuhudia.
Kwahiyo unejisikia furaha sana?
Kwa kiasi fulani labda utakuwa umejifunza Sasa unatakiwa kulipa simu ya mdogo wangu.
Hilo unajua alishindwa nitamlipa tena zaidi ya ile.
"Sawa bonge la bwana, niambie una jipya gani?
"Hakuna jipya ila nilikuwa naomba twende wote nyumbani kwenu nataka kumuomba mama
msamaha. "Kwa kosa gani?
"Huoni kosa nililofanya?
*Kuvunja simu ya Leyla?
"Ndio pamoja na kufanya fujo sehemu yake ya
biashara. "Kumbe unajua wewe ni mtu wa fujo?
Imetokea tu bahati mbaya. Usinipe hiyo sifa
nisije kunyimwa mke.
"Mke gani? Aliuliza Leyna huku akiwa anamuangalia usoni.
"Wewe
"Hivi kwa jinsi ulivyo na mawimbi yako unafikiri naweza kuolewa na mtu kama wewe? Mimi
nataka uhuru nikiingia kwenye ndoa niwe na
amani na sio kama nipo kifungoni
Abisai alimuangalia alafu akasema
"Kwahiyo hapa tunapotezeana tu muda?
Leyna hakutoa jibu waliendelea kutembea mpaka walipofika nyumbani alimkaribisha ndani
na kumpatia kinywaji.
Baada ya muda mama Leyna alifika na kukaa sebleni
Kijana kuna tatizo gani kati yako na binti yangu
Leyla?
Kabla Abisal hajajibu swali Leyna alinyanyuka.
*Acha niwaache muongee nipo jikoni. Baada ya Leyna kuondoka Abisai akaanza kuongea.
Mama kwanza kabisa naomba nitangulize.
samahani, naomba unisamehe kwa kile kilichotokea. Sikujua kama ni Leyla nilimfabanisha na Leyna.
"Kwani wewe na Leyna mnaugomvi?
Hapana mama..... Abisai alijibu kisha akasita
kidogo, mama Leyna alikuwa akimuangalia kwa makini ikionyesha alikuwa makini kusikia kile alichotaka kusema.
"Nakusikiliza baba
"Mimi na Leyna ni marafiki na nia yangu sio mbaya kwake nataka kumuowa lakini kuna baadhi ya mambo hayapo sawa najaribu kurekebisha.
"Wewe ndio huyo Abisal unaemnyoosha? Abisai hakuwa na jibu alimuangalia tu. "Umesema nia yako ni ipi?
"Ni kumuowa mama.
Mama Leyna alishusha pumzi kisha akaachia tabasamu la mbali.
Mimi sina tatizo kama nia yako ndio huo basi
fanya haraka ufuate taratibu. Abisai alifurahi kusikia hivyo.
"Asante mama nashukuru kwa kukubali ombi langu japokuwa sikuja rasmi.
"Usijali mwanangu, unakaribishwa.
Baada ya maongezi Abisai aliondoka na kwenda kwenye kijiwe cha samaki akamkuta Leyla
amekaa
"Leyla..
"Abeee...
Nisamehe kwa tabia niliyoifanya ila nitakipa
simu yako. Nitatumia pesa kwa Leyna. Hapana yani ni bora nikupe namba ya
kunitumia uniletee simu au pesa mkononi yule mtu sijawahi kumuaminibksbisa kwenye mambo ya pesa.
Abisai alitabasamu
Sawa usijali kesho mapema sana nitakuletea pale nyumbani.
Sawa.
Ilifika usiku Leyna, Leyla na mama yao walikuwa
wanakula. Mama yao akasema.
"Yule kijana anaonekana ana heshima sana na ni kijana anaejielewa.
"Mmmmmh... Leyna aliguna.
"Una huna nini?
"Haujui upande wake wa pili. " Awe na upande wa kwanza au wapili mimi sijali
Leyna yule ndio chaguo lako na mumeo mtarajiwa akileta posa unaolewa maana yeye ndio mwanaume anaeweza kuishi na wewe "Unasemaje mama?
Nina imani umenisikia vizuri sana. Abisai ndio
mwanaume wa kukuowa hao wengine utaenda kuangalia mkato wa chumba alafu utarudi au utaishia kuuliwa nikaitwa kuja kuchukua mzoga wako.
"Mama unaongea nini?
Anachosema mama ni kweli.....
Na wewe nyamaza hauna unachojua juu ya yule mwanaume.
Alichokuonesha pale imetosha kumjua na kumsoma ni mtu wa aina gani.
"Usiniambie kama kufurahia zile fujo zake alizokufanyia? Hivi unajua mimi ananifanyia zaidi ya kile akichokufanyia. Unamaanisha ana wivu na wewe.
*Tena uliopitiliza mpaka anakerwa yani.
Basi mwenye wivu ndio mwenye mapenzi, kama hiyo bahati ingenlangukia mimi basi ningefurahia tu maana ni dalili ya kupendwa.
"Una kichaa wewe mapenzi gani ya kujibishana mbele za watu, anataka kujua upo wapi, upo na
nani, umevaa nini, kuangaliwa kidogo kesi na mbaya zaidi nikitoka kidogo anaibuka kama mzimu, yani inakera sana Na jinsi alivyo king'ang'anizi basi nikisema simtaki anakataa
kabisa kuniacha,
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni