MADAM NIPE KIDOGO BASI* *________________________________________* *SEHEMU YA SITA*
Basi wakaanza kufanya mitihani, na katika kipindi chote hicho Kendrick hakuwah kunionesha ishara yoyote ile wala kunivunjia heshima kwa aina yoyote ile…
Basi siku zikaenda na hatimae maisha ya mitihani kwa watahiniwa yakaisha, na baada ya mitihani ndio walipanga kuwa wafanye maafali, michango ilishachangwa na wiki inayofuata baada ya wiki yao ya kufanyia mitihani kupita, ikafika siku ya maafali, yalikuwa ni maafali ya kipekee sana, kwa maana walialika wapiga bendi, wanafunzi wakaandaa maigizo na vichekesho mbali mbali, kulikuwa pia na vipaji vya kila aina, na moja ya maigizo yalinishangaza sana, maana muhusika mkuu alikuwa ni Kendrick, igizo lake lilikuwa kuhusu dharau ambayo wanawake ambao wanaumri mkubwa kidogo kudharau vijana wadogo, igizo lilianza vibaya ila lilimalizika na mafundisho makubwa…
Lilianza hivi “ alikuwa anaonekana daktari ambae alikuwa ni wa field akiwa anaingia kwenye kituo chake cha kazi kwa mara ya kwanza, alipokelewa na daktari wa kike, ambae kwa makadirio alikuwa ana umri mkubwa sana kuliko Yule kijana…
Walimchagua binti ambae alikuwa ana mwili mkubwa sana, ili kuendana na maudhui ya maigizo, na Kendrick ambae alikuwa anaonekana kama mdogo wake wa mwisho na Yule mwanaume, Yule kijana alipomuona Yule daktari macho yake yakawa yanagoma kuangalia pembeni, ni dhahiri kuwa alivutiwa nae sana, na kingine alikuwa anahisi kama atakuwa ameyafanyia ukatili mkubwa sana macho yake, kwa sababu alihisi kuwa ameona kitu cha thamani sana, Yule mwanamke alimuangalia kwa bashasha kisha akasema “ karibu kijana mdogo, mimi ndio nitakuwa nakaa na wewe na ndio nitakuwa nakuelekeza kila kitu kuhusu kazi yako……
Yule kijana mdogo akatabsamu tyu na majukum ya kikazi yakawa yanaendelea, kwa kuwa kijana alikuwa karibu na mwanamke ambae alikuwa amemvutia sana, akawa anafanya kazi kwa juhudi sana bila kumkera..
Yule mwanamke alikuwa anamateso ya aina mbili, ya kwanza yalikuwa ni kuhusu familia yake, nay a pili yalikuwa ni kuhusu mahusiano yake, Yule kijana akawa anapambana sana kumuweka sana, na muda mwingine kufanya hata majukum yake, na kila wakati alikuwa ndio kama msaada na faraja yake…
Kuna wakati Yule mwanamke alikuwa anakuja kazini, anakaa sehemu alafu analia tu, kijana akawa anapambana sana kumfariji na kujitahidi kumuweka sana, siku moja Yule mwanamke akamuamini na kuomba kuongea nae…
Akaanza “ mdogo wangu, yaan kama hauna mpenzi naomba usije ukaingia kwenye mapenzi kamwe, maana ni mateso makubwa sana , yaan kuna muda najihisi mwenye hatia sana na mjinga wa mwisho kwa kukubali kuingia kwenye mapenzi, maana ni upuuzi na maumivu ya hali ya juu…
Yule kijana akamuangalia kwa sekunde kadhaa kisha akasema “ ukiona unaishi na mtu na anakunyanyasa, basi jua huyo sio fungu lako, fungo lako na mwanaume wako wa kweli hawezi kukutesa kwa namna yoyote ile…
“ hizo ni kama hadithi za kale, kuna mwanaume gani kwenye hii dunia ambao hawachepuki, na kama hachepuki anapiga yaan kila mtu ni matatizo, yaan usiniaminishe kuhusu mambo ambayo hayapo…
“ kweli tena wanaume wenye mapenzi ya kweli wapo wapi?, embu nipe ushuhuda tu, huenda nikaelewa maana naona kama na wewe unanichanganya tu..
“ ni mimi, akajibu Yule kijana….
Yule bint akatoa macho bila kusema neno lolote lile, na yule kijana alijua taharuki ya Yule mwanamke, akaendelea kusema “ nakupenda sana nurse veronica….
ITAENDELEA……..
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni