MR ARROGANT ๐๐ฅ* ______________________________________* *SEHEMU YA KUMI NA SITA*
Paul alibaki ameduwaa mlangoni, macho yalimtoka kwa kile alichokiona.
Leon na jasmi nao walishituka , haraka Jasmine alijiondoa mikononi mwa Leon huku uso wake ukiwa umejaa aibu, alitafuta mahali pa kujificha lakini Leon lakini hakujua aende wapi Leon alimshika mkono wake, huku akimuangalia Paul kwa jicho kali.
โPole, samahani sikutaka kuingilia.... nimegonga lakini sijui tukiwa nikajua umetoka ... Yani hakuna mtu ndani. Paul aliongea kwa sauti ya chini yenye kigugumizi, ila macho yake hayakuacha kuonyesha mshangao.
โUnataka nini hapa?โ Leon aliuliza kwa sauti ya amri, akimuangalia moja kwa moja bila kupepesa macho
โNilikuwaโฆ nilikuwa na ripoti ya uhasibu, boss alafu nilimfuata lile faili uliotakiwa kuweka saini. Paul alijibu huku akiinua karatasi aliyokuwa nayo mkononi.
" Kwani kufuata faili ni kazi yako au ni kazi ya Jasmine.
" Niya jasmini lakini lilikuwa kinahitajika haraka alafu Jasmine sikumkuta ofisini kwake.
Leon akavuta pumzi ndefu, akamwachia Jasmine taratibu lakini bado akamgusa mkono kana kwamba hakutaka kumwacha aende mbali.
โWeka hiyo mezaniโฆ na usiwe na mazoea ya kuingia ofisini kwangu bila kugonga mlango tena. Hii ni amri.โ
Paul akakosa maneno, akashusha macho na kuweka karatasi juu ya meza kisha akatoka haraka.
Ndani ya ofisi ukimya ulirudi tena, ila hewa ilikuwa nzito kwa hisia. Jasmine akainua macho yake polepole, akawa anamuangalia Leon.
โBossโฆ umeona sasa? Haya mambo yakijulikana ofisini tutaharibu kila kitu.
Leon akasogea karibu zaidi, akashika uso wa Jasmine taratibu kwa mikono yote miwili.
โNasema tena Jasmine, siogopi chochote. Sijali mtu atajua nini. Nilichojua ni kwamba nakupenda na sitaki kukuficha tena. Lakiniโฆโ alinyamaza kidogo, akimtazama kwa makini, โโฆkama hutaki, bado naweza kuweka siri hii kwa ajili yako.โ
Jasmine akapumua kwa nguvu, moyo wake ukicheza kwa kasi.
โMimi sina hofu juu yako, Leon. Nimekupa moyo wangu. Ila watu wakianza kuongeaโฆ sitaki kuonekana kama nimepata kazi kwa sababu ya mapenzi.
Leon akatabasamu kwa jeuri yake ile ya kiasili.
โKwa sasa wewe ni secretary wangu. Lakini karibia nikupandishe cheo. Jasmine, unastahili kila kitu, na siyo kwa sababu ni mwanamke wangu, bali kwa sababu ni wewe.
Jasmine alijikuta anatabasamu, akamkumbatia tena bila kujizuia. Mapenzi yao yalikuwa kama moto uliowashwa kwa petroli moto ambao hakuna mtu angeweza kuuzima tena.
" Baby acha nikaendelea kufanya kazi .
" Sawa ila badae nitahizaji tukutane sehemu nahitaji muda wa kutosha kuwa na wewe kivuruge wangu.
" Sawa mr arrogant.
Leon alimbusu kwenye shavu kisha Jasmine alitoka ofisini kwa Leon.
Alipotoka nje alimkuta Paul kasimama na alikuwa akimuangalia kwa mshangao mkubwa. Jasmine alimpita kama vile hajamuona.
Paul alipokuwa anatoka ofisini alikuwa bado amechanganyikiwa. Alijua siri kubwa sasa, siri ambayo ingeweza kutikisa kampuni yote kama ingesikika nje.
" Nina miaka kumi kwenye hii kampuni sijawahi kumuona Leon akiwa na mwanamke tena inaonekana yupo kwenye mahaba mazito sana.
Akiwa bado anafikiria simu yake ya mkononi iliita alitoa mfukoni akaangalia kwenye screen akakutana na jina boss Leon . Alipokea haraka .
" Ndio boss.
" Njoo ofisini kwangu.
Aliongea Leon kisha akakata simu. Paul kijasho shembana kilimtoka alihisi mambo si shwari maana Leon alimuacha akiwa kakasirika sana.
" MUNGU wangu naomba usimamie kibarua changu maana huyu jamaa hatabiriki hata kidogo .
Paul alimuomba Mungu kwanza ndipo akasogea karibu na mlango. Alipiga alama ya msalaba kisha akagonga mlango.
โIngiza!โ sauti ya Leon ilisikika ndani.
Polepole Paul aliingia, akafunga mlango kwa heshima akaingia ndani. Leon alikuwa amekaa kwenye kiti chake cha kifahari, mikono yake ikiwa juu ya meza.
โPaulโฆโ Leon alianza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo.
โBoss.โ Paul akaitika, akijaribu kuficha hofu yake.
โUnajua kosa kubwa ulilofanya leo? Leon alimuuliza huku akiwa anamuangalia usoni.
โNdio boss naomba radhi. Sikudhamiria kuingiliaโฆ ilikuwa bahati mbaya,โ Paul alijibu huku akiweka mikono yake nyuma kwa unyenyekevu.
Leon akatabasamu kwa jeuri, tabasamu lile lisilotabirika, lenye kuchanganya hofu na mvuto.
โBahati mbaya? Au ulikuwa na nia ya kunifunania? Wewe ni mfanyakazi wa muda mrefu hapa, najua vizuri jinsi unavyofanya kazi yako lakini mbona unataka kunivuruga?
โBoss, tafadhaliโฆ sitasema chochote. Nimekuhudumia kwa miaka kumi sasa, hujawahi kuniweka mashakani. Naomba uniamini hii siri itaishia hapa. Naapa.
"Sawa . Wewe ni mwanaume nina amini hili uliloliona litaishia ndani ya kuta ya hiki chumba.
" Nakuahidi boss wangu nitakufa na siri yangu.
" Safi sana. Hebu kaa hapo kwanza tuongee.
Paul alivuta kiti akakaa .
" Paul hivi upo kwenye uhusiano?
" Ndio nina mke na mtoto mmoja wa miaka miwili.
" Waoooo hongera sana. Vipi maisha ya kuishi mwenyewe na kuwa na mwenza wako?
" Maisha ya kuwa na mwenza ni bora sana.
Leon aliachia tabasamu
" Boss kwahiyo Jasmine ndio shemeji ?
" Ndio yeye ndio ubavu wangu ila sitaki watu wajue kwa sasa mpaka pale itakapokuwa rasmi kwetu.
" Hongera ndio maana siku hizi unaonekana una furaha sana.
" Paul ni siku chache tu nimeingia kwenye mahusiano na Jasmine lakini najiona nipo tofauti, kuna hali fulani ya amani naipata moyoni mwangu.
" Ni kweli inaonekana zamani haikuwa hivi.
" Ila na kusisitizia kuwa makini na hii siri.
" Usijali boss.
" Sawa unaweza kwenda kuendelea na kazi.
" Sawa, sawa boss. Uwe na kazi njema.
' na wewe pia.
Paul alitoka ofisini kwa Leon akiwa haamini .
" Daaaah kumbe manvenzi ndivyo yalivyo?yanaweza kumbadilisha simba akawa paka eti leo Leon amekaa na mimi tutaongea kama marafiki sababu ya mapenzi tu.
" Aiseee hongera iende kwa mwanamke jasiri Jasmine amejua kutoa dozi.
Offer offer offer
Soma yote kwa sh 800
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni