Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

SIMPENDI MFANYAKAZI WETU ?EPISODE 1

31st May, 2025 Views 109

SIMPENDI MFANYAKAZI WETU
?EPISODE 1
?
?Kwa majina naitwa happy adui yangu mkubwa kwenye maisha yangu ni mtu maskini mimi natoka katika familiya ya kitajili sana na nawachukia chukia sana maskini sababu sijuwi nawaonaje ila siwapendi tu nikiwaona naona kama nmeona kinyesi hivi... tena kibaya zaidi nilikuwa nawaona tu mitaani lakini mama akaamua amlete maskini nyumbani kabisa jina lake ni Rashid ametokea ndani ndani uko sijuwi ni mwisho wa upepo lakini nilitokea kumchukia sana haiwezekani nyumba ya matajiri anakuja maskini mmoja .....
?
?
? HISTORIA YA RASHID
??????????????????????
?Maisha ya Rashidi hayakuwa rahisi hata kidogo. Alizaliwa katika familia maskini, kwenye kijiji ambacho kilisahaulika na dunia. Baba yake alifariki akiwa mdogo, na mama yake, mwanamke jasiri lakini aliyekandamizwa na umasikini, alijitahidi kuwalea yeye na wadogo zake.
?
?Alikuwa na ndoto. Alitaka kusoma, kuwa mtu mkubwa maishani, lakini ndoto zake zilivunjwa vipande vipande pale alipomaliza darasa la saba na kukosa kabisa njia ya kuendelea mbele. Baba mdogo wake, aliyepaswa kumlea baada ya kifo cha baba yake, alimchukia na kudiriki hata kumfukuza kwa maneno ya kejeli .....
?"Huna akili, hata kama ningekuwa na pesa,ningekukodia majambazi wakuue unatumalizia hewa ,hewa imekua nzito sababu ya uwepo masikini mbwa taka taka
?," alimuambia siku moja kwa dharau.
?
?Rashidi aliona ndoto zake zikififia. Alijua kuwa hakukuwa na msaada wowote. Hakuna aliyemjali. Kila siku alishuhudia mama yake akihangaika, akienda kwenye mashamba ya watu kulima kwa ujira wa chakula kidogo tu. Wadogo zake walimwangalia kwa macho ya tumaini, wakidhani labda angeweza kuwaokoa kutoka kwenye janga la umasikini.
?
?Lakini angewezaje, wakati hata yeye alikuwa akihangaika?
?Hatimaye, alichukua uamuzi mgumu. Aliamua kuondoka kijijini, kutafuta kazi mjini. Alianza kuuza maji kutembeza tembeza karanga
?
?Bahati mbaya, mjini hakukuwa kama alivyotarajia. Alihangaika mitaani, akifanya vibarua vya hapa na pale kubeba mizigo sokoni, kufagia maduka, na wakati mwingine hata kulala njaa.
?
?Tuanze sasa baada ya kumjua RASHID
????????????????
?
?Siku moja, wakati akiwa amechoka na kukata tamaa, alikutana na mama yangu. Alikuwa akitoka sokoni, mikono yake ikiwa imebeba mifuko mizito ya vyakula. Rashidi, kwa uchovu wake wote lakini aliwaona vijana wakinyemelea mizgo ya yule mama .....
?mara ghafla wale watu walikwapua na kuanza kukimbia
?"msaaada jamaani " mama alipiga ukunga ..na kukaa chini huku kakishikilia kichwa chake .....
?
? Rashid alitoka mbio mbip na kuanza kuwakimbiza walikatisha vichochoro vingi lakini Bado alikuwa yupo nao sambamba alizidi kuwakimbiza waliweza kusalimu amri na kusema chukua vitu vyako na uende tuache na maisha yetu
?
?" kwanini mnaiba sasa?
?" kaka ni maisha tu tunapambana"
?" siku mtachomwa moto "
?" tutabadilika tusamehe kaka"
?"bahati yenu! Haya tokeni hapa"
?Akawatishia walitoka mbio sana yeye akabeba vitu na kurudi navyo ....
?
?Mama akiwa kakata tamaa maana hata pochi yake yenye kadi ya benki pamoja na vitu vingine kama simu na hela vilikuwa vishachukuliwa hivyo ilikuwa kajikatia tamaa tu ...mara akasikia sauti
?" mama pole lakini shukuru mungu nimewakamata chukua vitu vyako "
?
?Mama aligeuka haraka na kumkuta kijana Rashidi akiwa nyuma yake na anamkabidhi vitu vyake mama alifurahi sana ....
?.
?Mama yangu alimshukuru sana Rashid . pia mama Aliona macho yake yalivyochoka, lakini yenye heshima na ujasiri.
?
?"samahani mwanangu unafanya kazi gani"
?"mama maisha ya kuuunga unga popote kambi . Tunapambana angalau mkono uende kinywani ". Mama alimuonea huruma na akakumbuka nyumbani kuna kazi nyingi ambazo mimi siwezi kufanya pekee yangu na kila siku nilikuwa nafanya kizembe zembe sasa akaona amchukue kama fadhila kwa wema alio mtendea ....
?
?
?"Unatafuta kazi?" mama yangu aliuliza.
?
?"Ndiyo, mama. Kazi yoyote, bora nipate mahali pa kulala na chakula," Rashidi alijibu kwa sauti ya unyenyekevu.
?
?Mama yangu alimtazama kwa muda, kisha akatabasamu kwa huruma
?"Njoo nyumbani kwangu," alisema. "Tutakupa kazi."
?
?Na hivyo ndivyo Rashidi alivyoingia kwenywe maisha yetu. Kazi aliyopata ilikuwa ya kuwa mfanyakazi wa ndani house boy. Alikuwa na sehemu ya kulala, chakula cha uhakika, na mazingira salama si unajua sisi matajiri hatuna dogo.
?
?Lakini hakujua kuwa sehemu moja ya maisha yake ingekuwa jehanamu.
?Nilikuja kuwa kama jinamizi lake.
?
?Basi majira ya usiku mama aliingia na mlinzi alifungua geti baada ya kusikia honi. Na nilifurahi sana maana mama sijamuoana takribani siku nzima na navyompenda mama yangu huniambiii kitu
?
?Nilimkimbilia na kumkumbatia mama yangu lakini Ghafla nikasikia mlango ukifunguliwa niligeuka kwa mashaka ghafla akatoka rashidi akiwa kabeba rambo yenye nguo zake alikuwa kapauka usoni kama anafanya kazi dampo ..
?
?"kheeee mama huyu marambo ni nani tena mbona kapauka uso kama anafanya kazi dampooo"
?
?" acha maneno ya hovyo bila huyu kaka sijuwi ningeweka wapi sura yangu.
?
? Nilipolwa vitu vyote hyu ndo malaika mlinzi wangu wa leo "kisha akamwambia rashidi huyu anaitwa Happy ni mwanangu mpendwa akanigeukia
?
?"huyu ni Rashid kuanzia leo atakuwa mfanyakazi wetu hapa . Mkaribishe na muonyeshe mazingira kesho asubuhi atalala kile chumba alichokuwa analala mjomba wako"
?Nilichukia chumba kile ni kizuri jamani na kina tv leo maskini huyu alale kwenye hiki chumba kweli wakati katoka huko na ananuka majasho ya kimaskini leo alale nyumba ya kitajiri kweli .....
?
?Tuliingia ndani lakini mimi sikupendezwa naye hata kidogo kutokana na alivyo ni vile tu damu zetu haziendani hata kidogo .......na kweli namchukia tu.
?Tulipoingia ndani baada ya kumuonyesha chumba
?
?" Rashidi hilo jasho lako la mtaani hutakiwi kuingia nalo kwenye familia hii ya kitajiri ,maana maskini kama nyinyi mnatakiwa mlale dampooooo".
?
?Rashid hakunijibu chochote zaidi zaidi alishukuru na kuniuliza "bafu iko wapi?"
?Nilimlekeza kwa hasira kisha nikaenda kumcheki mama na kuwa na mazungumzo naye ......
?
?CHUMBANI KWA MAMA ......
?????????????????
?"Nina uhakika hata hana elimu ya maana," nilimwambia mama yangu
?
?"Lakini, mwenzako amejituma, na ni kijana mwema na sioni kama ni mtu mbaya," alijibu kwa utulivu.
?
?"sawa mama wewe unasema hivo lakini unaweza kufuga na kulea jambazi likaja kutuua maana wabaya wanajificha kwa watu wema "
?."nenda ukalale tutaongea kesho sawa ,usiku mwema nenda kalale byeee nakupenda mwanangu "
?
?" byeee mom uwe na usiku mwema"nilitoka na kurudi chumbani kwangu nilichukua mitooo na kutupa tupa huku na kule na kun'gata meno
?" huyu maskini nitamkomesha sio siri.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY???15

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA? Sehemu 13.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY ???11

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 29

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

LOVE Part 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 28

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA Sehemu nne.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 26

mrindia rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 25

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest