*1 - - - - - 5* πππ’ π‘π π π₯ππ ππ’ πͺπ π§πππ§π’π ___________________________________ SEHEMU YA 1 MWANZO....... "Ni aibu Mwanaume mwenye meno 32 kulalamika mkewe hajamuandalia chai
Mwanaume anayetamani kutengeneza familia na Mimi ajiandae kuogesha Watoto wake, kama anapenda wali wenye nazi ajue atanisaidia kukuna..... vyombo pia ataosha hata Mimi pia nitafanya majukumu yake....nisiwe muongo Mimi pia napenda kutafuta pesa. Kuna wakati tutalala njaa kwa sababu tumeshinda kazini wote kutafuta pesa "
Bryant Kobe alijikuta akiachia tabasamu kwa upuuzi aliokuwa ana zungumza Tasha Mrembo wa Tiktok. Hakuishia hapo alimfollow kwa lengo la kuwa ana sikiliza pumba zake π.
"Nimejikuta nikihisi hasira kwa maneno anayo zungumza huyo mjinga mafundisho ya uongo yanayo tolewa mtandaoni yamefanya mabinti wengi wawe na viburi....na ndio najikuta napoteza hisia na mapenzi " Bryant Kobe alizungumza huku akizidi kumkagua kagua Tasha aliyechafua hali ya hewa kwenye mtandao wa Tiktok.
"Kwa upande mwingine yupo sahihi kuna Wanaume hata kuflash haja zao wakiwa chooni hawawezi kisa na maana ameoa π Mwanaume kama huyu nikimpata namnyoosha " Secretary Annie alizungumza.
"Na ndio maana hauna mahusiano mpaka sasa "
"Vipi? wewe hayo mahusiano unayo π" Annie alijikuta akiachia kicheko.
"Nafikiria kufanya mabadiliko ya Wafanyakazi wote kwenye hili Kampuni huenda ukawa mmoja wao hivyo kuanzia sasa kabla hujajibu au kukosoa chochote hakikisha unatuliza akili yako kwanza " Bryant Kobe alionesha hasira zake wazi wazi.
"Sa...sa...samahani " Annie alijishusha huku akibetua midomo kimya kimya,
Kauli aliyoizungumza Tasha ilikuwa gumzo mtandaoni ....watu wengi walitamani kujua historia yake.
Ni mtoto wa Kishua, msomi, Mrembo na kubwa zaidi hana kashifa mbaya sehemu yoyote ile.
Ni Mwanamke anayeamini katika usawa, hivyo tegemezi katika nyanja yoyote ile
Mida ya usiku Bryant Kobe akiwa kajipumzisha chumbani kwake aliingia Tiktok kwa mara nyingine tena.
Lengo lake lilikuwa ni kusikia pumba gani Tasha kazungumza tofauti na ile ya asubuhi.
"Mahusiano siyo ajira π kuna watu wanaingia huko kwa matarajio ya kujenga, kung'aa, kupata shepu na kumiliki simu za bei mbaya. Ni upuuzi kufikiria hivi ...nachotaka kusema hapa ni kwamba watu tufanye kazi....kitu kingine Mimi ukiniita ghetoni kwako nije kukufanyia usafi nitafanya kwa moyo mkunjufu ni kijua mwisho wa siku utanipa mshahara wangu. Msimamo wangu ni ule ule, siwezi kumfanyia usafi mpenzi wangu bure. Nitafanya hivi kwa Mume wangu kwa sababu ni nyumba yetu sote lakini siku nikiwa sina mood sitarajii kuulizwa leo hufanyi usafi ....."
"Mpuuzi huyu alianza vizuri lakini kamaliza vibaya...." Bryant Kobe aliongea pekee yake kisha akaachana na Tiktok.
Kitendo tu cha kufumba macho usingizi ulimpitia, alikuwa kachoka sana.
Kulivyo pambazuka alikunywa chai kisha akaelekea Shopping center ya Raba, ni mtu anayejipenda sana na mara nyingi anapenda kwenda na fasheni.
Raba zilizokuwa zinapatikana hapa zilikuwa ni za jinsia yote na rika lote .
Wadada wengi waliokuwa mahali hapa hawa kusita kumuangalia....wenye kutamani wampe K zao bure walinyoosha vidole vyao ndani ya mioyo yao.
"Ni CEO wa Kampuni ya Danone wanayo sambaza maji bora ya kunywa π" Binti mmoja aliongea kwa sauti ya chini.
Basi baadhi ya mabinti walianza kutafuta fursa kwa kumuonesha tabasamu.
Vile ana moyo mgumu kuhusu mademu wala hakutikisika.
Akiwa katika kuchagua chagua huku na kule aliparamiana na Tasha mrembo wa Tiktok π€.
Alimanusura simu ya Tasha idondoke chini lakini Bryant Kobe aliidaka. Na ndipo macho yao yaligongana π.
ITAENDELEA.......
SEHEMU YA 2
Endelea......
"Simu yako hii hapa " Bryant Kobe alizungumza baada ya kuchoka kugonganisha macho
Tasha alipokea kisha akaitia kwenye pochi yake, ni wazi kabisa hakutaka idondoke chini alijiandaa kuondoka lakini alisubirishwa.
"Hujui hata kusema ahsante nimeiokoa simu yako" Bryant Kobe aliongea.
"Mwanaume ni jukumu lako kuikoa kama ingetengeneza mpasuko hata kidogo tungefika Polisi "
"Kwanini " Bryant Kobe aliuliza kwa mshangao
"Miguu yako haikuwa makini hasara kidogo tu ingekula kwako.... camera za hapa zingetusaidia kuongea nani mhalifu na nani mwema, uwe na siku njema" Tasha aliongea kisha akaondoka.
Tayari alishajitengenezea umaarufu hivyo watu wote walikuwa wananong'ona kuhusu yeye na masomo yake anayoya fundishaga.
Bryant Kobe si mtu wa kusumbuliwa na vitu kama hivi, aliendelea na kazi yake ya kutafuta Raba kali baada ya kumaliza alielekea nyumbani kwao.
"Tafadhali sana siku ya leo naomba usiende sehemu yoyote ile kutakuwa na ugeni " Zara (Mama wa Kambo wa Bryant Kobe) alizungumza.
"Ulitakiwa kunipa taarifa mapema sina uhakika kama nitavunja ratiba yangu " Bryant Kobe aliongea akataka kuondoka lakini Zara alimtegea mguu, ili aweze kuendelea na safari yake itamlazimu akanyage mguu wa Mama yake wa Kambo. Hakuwa tayari kufanya hivi hivyo alikaa kusikiliza.
"Ulivyokuwa na miaka 5 ulipenda kuzunguka huku na kule watu wakuone kisa tu umevaa viatu vipya usiniambie hii tabia haijafa bado, usinifanyie hivyo umeshakuwa mvulana mkubwa sasa tunza hivyo viatu ndani utavaa wiki ijayo kama utaendelea kunisumbua itanilazimu ni kalie kwenye kaburi la Baba yako π" Zara aliongea.
"Huna haja ya kufika mbali, nitavunja ratiba zangu zote kwa ajili ya wageni wako " Bryant Kobe aliongea kisha akakaa kwenye kochi.
Zara ndio kutabasamu baada ya kuona anasikilizwa.
Basi kwa kushirikiana na Wafanyakazi wa ndani waliandaa chakula kwa ajili ya wageni.
Kilikuwa ni chakula kingi sana na hata Bryant Kobe alishindwa kuelewa ni kina nani hao wanakuja.
Aliingia Tiktok aone kuna habari gani mpya zinaendelea.
Alikutana na Tasha akiwa anajicheza cheza na wimbo wa Amanda ulioimbwa na Zuchu π.
Alisikia kuboreka zaidi π aliachana na Tiktok kisha akaanza kufanya kazi zake za ofisini.
Hatimaye muda wa Wageni kuja uliwadia.
Ilimlazimu Bryant Kobe kwenda nje kukarimu Wageni akiwa na Mama yake wa Kambo.
Moyo wake ulidunda kidogo baada ya kumuona Tasha akiwa na wazazi wake.
"Karibuni...." Zara aliongea akiachia tabasamu.
"Tumekaribia....." Mama yake Tasha aliongea huku akimkodolea macho Bryant Kobe π kuna namna alimuelewa haraka sana.
"Bryant Kobe salimia π" Zara ndio kumkumbusha.
Basi Bryant Kobe alisalimia kishikaji tu ni mtu asiyependa shobo sana.
"Huyu ndio Phillips Kobe " Baba yake Tasha aliuliza
"Hapana, yeye bado yupo masomoni....huyu ndio Kijana wa kwanza wa Kobe bila shaka umewafananisha eeeh π€" Zara aliongea.
"Nafikiri...." Baba Tasha aliongea kisha akaelekea ndani.
Basi kwa pamoja walikaa mezani kula. Ulaji wa Tasha ulikuwa mbaya sana kiasi cha kumkwaza Bryant Kobe.
Mama Tasha aliligundua hili, vile kamuelewa Bryant Kobe hakutaka akwazike hata kidogo. Alipenyeza mguu taratibu amkanyage Tasha ajirekebishe, bahati mbaya alimkanyaga Bryant Kobe.
ITAENDELEA.......
SEHEMU YA 3
ENDELEA.....
"Sa...samahani π£" Mama Tasha alijitetea
Watu wote walimgeukia kujua nini kinamfanya ajitetee.
Bryant Kobe alivunga haelewi chochote, aliendelea kula. Hakuwa mlaji sana ukilinganisha na watu wengine.
Tasha hakusita kuchukua nyama zake zote.
"Nadhani wewe si mpenzi wa nyama "
"Ndiyo, huyu si mpenzi wa nyama ukilinganisha na Philips Kobe " Zara aliwahi kujiongelesha.
Baada ya chakula kumalizika vyombo vilitolewa mezani.
"Bryant Kobe unaweza kumtembeza Tasha mazingira ya huko nje " Zara aliongea, bila shaka watu wazima wakongwe walihitaji kufanya mazungumzo.
Bryant Kobe hakuwa na noma alianza kumuonesha Tasha mazingira ya nyumbani kwao.
"Vipi unataka kuhamia hapa kwanini nimeambiwa ni kuoneshe mazingira ya hapa"
"Kichwa kikubwa akili hamna siku zote wazazi wetu hutuondoa kwa namna hiyo wakitaka kuzungumza mambo yao ya siri au ulitaka kuambiwa wee mvulana toka tuna mazungumzo " Tasha aliuliza.
Bryant Kobe hakujua ajibu nini, alimpuuza Tasha akaendelea kumtembeza.
"Nyumba yenu nzuri sana, kwa kuwa nyie ni family friend ipo siku nitakuja hapa kurekodi kipindi changu "
"Kipindi kipi? hicho unacho zungumzaga Tiktok, ukweli ni kwamba unatia ajbu sana. Kwa muonekano wako huo ulipaswa utengeneze kizazi kinachojiamini katika suala zima la utafutaji pesa na si kuongea pumba kama zile....kuna namna unafanya Wanaume waone siyo kitu. Ukweli ni kwamba kupitia mafundisho yako hayo kutakuwa na wimbi kubwa la mpasuko katika ndoa za watu " Bryant Kobe alionesha hasira zake waziwazi.
"Nilitarajia kuiona hii hoja yako kwenye sehemu ya comment na si kama hivi unavyo fanya..... mafundisho yangu yapo sahihi na nitaendelea kusambaza ulimwenguni kote. Mwanamke si Mtumwa wa Mwanaume vipi inauma kuambiwa huu ukweli...." Tasha aliuliza.
"Upo kwenye mahusiano π" Bryant Kobe aliuliza kabla hajatoa hoja yake.
"Sipo kwenye mahusiano, vipi kwani"
"Naomba uyashike maneno yangu na uikumbuke siku hii...." Bryant Kobe aliongea Kisha akamsogelea kwa ukaribu zaidi.
Tasha alifungua masikio yake kwa umakini pia, alihitaji kusikia anacho ambiwa
"Hakuna Mwanaume atakuja kukupenda wala kukutamani utazeeka pekee yako ukijitahidi sana kuficha aibu itakulazima kuoa Mwanamke mwenzio atakaye weza kufanya kazi sawa na wewe"
Tasha aliachia tabasamu bila kujalisha ukali wa maneno ya Bryant Kobe.
"Mwanaume yoyote yule ni kimtaka nampata hata wewe ni kisema unioe sasa hivi na ufanye kazi zangu zote nazotaka utafanya " Tasha aliongea kisha akaondoka huku akicheka.....kiwango chake cha kujiamini kiko juu sana kupita maelezo.
"Bila shaka anatawaliwa na pepo la upweke, Mwanamke mwenye malengo ya kuitwa mke wa mtu hawezi kuzungumza hivi " Bryant Kobe aliongea akionekana kumpuuza kupita maelezo.
Hakutaka kuharibu siku yake, alishika simu yake akampigia Philips Kobe (Mdogo wake waliochangia Baba tofauti Mama)
"Unarudi lini? kuna namna naboreka sana siku kuisha bila kukuona wewe "
"Upweke mbaya, unanimiss sana kwa sababu upo single , mbona Secretary Annie ni mrembo fanya mpango chapu bhana" Philips Kobe aliongea.
"Nani kakueleza furaha yangu inategemea Mwanamke?....kama unamini hivi basi utateseka sana . Masharti ya Mama yako yananishinda, kuna muda ananipangia muda wa kurudi nyumbani...nimeshakuwa mvulana mkubwa eeh, nikimvimbia anatishia kwenda kulia kwenye kaburi la Baba yetu"
"Nilimuambia akuchunge kwa ajili yangu punguza hasira, nadhani wiki ijayo nitakuwa hapo π" Philips Kobe aliongea.
Basi waliongea mawili matatu kisha wakaagana.
Bryant Kobe anaamua kurudi ndani, anafarijika kuona Wageni wanataka kuondoka.
"Karibu nyumbani kwetu, hakikisha unakuja hata siku moja. Tasha ni Kijana mwenzako italeta picha nzuri kama mtakuwa mnatembeleana mara kwa mara " Mama Tasha aliongea akiwa kamshika mikono Bryant Kobe.
Tasha ni kubetua tu midomo kimya kimya, yupo radhi kupoteza muda wake kwa kutazama movie na si kukaa na kuzungumza na huyu kidume.
"Nikipata muda nitakuwa nafanya hivyo " Bryant Kobe aliongea kwa ufupi.
"Hebu msaidie Tasha kubeba pochi yake, anaonekana kuchoka " Zara ( Mama wa Kambo wa Bryant Kobe) alitoa maelekezo.
Macho yalimtoka Bryant Kobe kwa kazi aliyopatiwa eti abebe pochi ya Tashaπππ............Maana nicheke kwanza
ITAENDELEA.......
SEHEMU YA 4
ENDELEA.........
Bryant Kobe alitaka kugoma lakini kwa jinsi Mama yake wa Kambo alivyo mtazama hakuwa na namna.
Aliichukua pochi mikononi mwa Tasha kibabe.
Hakusubiri kuambiwa alisogea mpaka kwenye gari.
Basi Tasha aliingia kwenye gari baada ya kuhakikisha amekaa vizuri alinyoosha mkono wake.
Bryant Kobe alimkabidhi pochi.
"Natarajia kuona comment yako kwenye mafundisho yangu nayotoa kila siku. tengeneza hoja nzito nami nitakujibu kwa hoja " Tasha alimalizia kuongea kwa kukonyeza.
Bryant Kobe hakupendezwa na ukonyezaji wake aliondoka.
"Hivi Bryant Kobe ni Kijana wa aina gani " Tasha alimuuliza Baba yake kwa sababu hakuonesha kumshobokea Mwanaume huyo.
"Ni Kijana makini sana....naweza kusema anafaa kuwa kiongozi wa familia au Serikali "
"Pia anaonekana kujali sana watu, ni Kijana mzuri sana jamani...ikitokea mmepata Mtoto nitaringa sana π€" Mama Tasha alijisemesha.
"Na ndio maana sikukuomba mtazamo wako....kitu unacho kiwaza ni cha ajabu sana " Tasha aliongea.
Mama mtu aliishia kubetua midomo, siku zote yeye na Binti yake huwa wana tofautiana mitazamo.
Upande mwingine Bryant Kobe akiwa ana pambana kutafuta usingizi alijikuta akikumbuka maneno ya Tasha.
"Mwanaume yoyote yule ni kimtaka nampata hata wewe ni kisema unioe sasa hivi na ufanye kazi zangu zote nazotaka utafanya "
"Anajiamini nini huyu....ngoja nione mwisho wake. Aina hii ya watu wanaojiamini kama yeye huwa wanaishia vibaya " Bryant Kobe aliongea.
Kulivyo pambazuka asubuhi aliwahi kuamka. Si mtu wa kupenda kulala sana.
Kicheko cha Mama yake wa Kambo π π kilimfanya asite kidogo kuendelea na kitu alichokuwa anataka kukifanya
"Bryant Kobe hebu sogea hapa, huu ujumbe ni wa kwenu π .....Tasha aliyekuwa hapa jana kajua kunifurahisha π€£π€£" Zara aliongea akionekana kufurahi.
"Hivi mnajua ni kwanini Wanaume wengi hukasirika kupita kiasi pale wanapoombwa pesa?. Leo nitawaibia siri.... Wanaume wengi huogopa kusema ukweli kuwa hawana pesa....unapomuomba pesa na yeye hana, unamfanya ajisikie vibaya zaidi hivyo kuliko ukazane kumuomba pesa itapendeza kama mara moja moja ukiwa unamtumia anaweka akiba ili siku ukimuomba asikose pa kushika" Bryant Kobe alirudisha simu baada ya kumaliza kusikiliza, alijitia amefurahi lakini ndani ya moyo wake alisikitishwa na mitazamo ya Tasha.
"Kuna sehemu naenda ndio maana nimeamka mapema, baadae " Bryant Kobe aliongea kisha akaondoka.
Zara wala hakumzingatia, alikuwa na kibarua cha kuwatumia marafiki zake hii video iliyomvunja mbavu.
Bryant Kobe akiwa kwenye gari lake alifanikiwa kumuona Tasha akiwa kavaa kigauni cheupe.
"Nitamkomesha...." Bryant Kobe alijisemea kisha akaongeza kasi ya gari, kwa makusudi alipita kwenye maji yaliotuama.
Waaaaaaa π©π© gauni ya Tasha iligeuka kuwa rangi ya udongo....pamoja na yote alijitahidi kadri ya uwezo wake kuikariri plate number ya gari lililomfanyia makusudi.
ITAENDELEA...........
SEHEMU YA 5
ENDELEA....
Moja kwa moja Tasha alimtumia namba rafiki yake anayependa kucheza na mambo ya magari.
"Nipo barabarani bado, sitaondoka mpaka utakapo niambia mmiliki wa hilo gari ni nani β" Tasha alimsisitiza rafiki yake.
Baada ya dakika kumi kupita alitumiwa majina ya mmiliki wa gari lililomwagia maji machafu na mahali anakoweza kumpata.
"Bryant Kobe anaonekana kuvutiwa na Mimi hizi chokochoko siyo bure, anyway anachokitafuta atakipata " Tasha alijisemea kisha akasimamisha bajaji.
Ilimlazimu kurudi nyumbani, kwa wakati huu alipendeza kuliko mara ya kwanza.
Anaamua kuvunja ratiba zake zote sababu ya vurugu aliyofanyiwa na Bryant Kobe.
Moja kwa moja alielekea nyumbani kwao. Zara anaachia tabasamu baada ya kumuona. Anatamani sana binti huyu amilikiwe na Philips Kobe (Mtoto wake wa damu).
"Ukiwa unasubiria chai kuta unatazama hizi picha, huyu ni Kijana wangu Philips Kobe hapo alikuwa na miaka 18" Zara aliongea kisha akaondoka.
Tasha hakuwa na namna zaidi ya kutazama, bahati mbaya au nzuri kati kati ya picha hizi kulikuwa na picha ya Bryant Kobe enzi hizo ana miaka 21.
Tasha alijikuta akiitazama picha hii bila kukoma, alipoona kama atafumwa hivi aliiweka kwenye pochi yake.
Basi Zara aliweka chai mezani, walianza kuburudika huku wakipiga stori za hapa na pale.
"So, mpaka sasa haupo kwenye mahusiano " Zara alitupia mtego.
"Sipo na wala sijataka kuwa....na mambo mengi sana nikisema nianzishe mahusiano kwa sasa nahofia kusema nitayatelekeza "
"Hapana, ni vile tu hujakutana na mtu wa kuziteka hisia zako, endelea kujipa muda " Zara alishauri.
Basi kati kati ya mazungumzo yao, Bryant Kobe alifika.
Moyo wa Tasha ulishtuka hasa akikumbuka kaiba picha ya huyu kichaa.
"Natumaini umekunywa chai huko ulikotoka " Zara alikumbusha kwa sababu alikuwa ameandaa kidogo sana.
"Usiwe na hofu, Mgeni karibu" Bryant Kobe aliongea kwa ufupi kisha akapiga hatua aondoke.
"Nimekuja hapa kwa ajili yako" Tasha aliongea.
Basi Bryant Kobe ilimlazimu kuelekea bustanini kwa ajili ya mazungumzo.
"Mb.....wa wewe mwenye kichaa π kwanini ulinimwagia maji machafu??? naomba uniombe msamaha haraka iwezekanavyo au nikupeleke Polisi" Tasha alifoka.
Bryant Kobe alimtazama kwa nukta kubwa kisa na maana kamuita Mbwa.
"Acha kunitazama namna hiyo, fanya haraka kuniomba msamaha"
Bryant Kobe alinyoosha mkono akamkwida Tasha ni hivi alimkunja kisawa sawa kisha akamsogelea wakawa pua na mdomo.
"Mwanaume hapandishiwi sauti wala kutukanwa hadharani....hilo tusi ulililo ni tupia ulipaswa utukane kimoyo moyo na si hadharani " Bryant Kobe alifoka.
Kitendo cha Tasha kurefusha tu mdomo ajibu mashambulizi alijkuta kazigusa lips za Bryant Kobe.
"Mb.....wa huyu ni kisema ni mheshimu bila kuzifanya chochote lips zake atakuja kunifokea Tiktok" Bryant Kobe alijisemea ndani ya moyo wake kisha akafungua mdomo wake.
Alianza kumpiga denda Tasha aliyeonekana kuridhia.
Zara akiwa kabana nyuma ya mti alitoa macho kwa anakiona.
Alijisahau kabisa kama mahali hapa kuna siafu.
"Nini hiki π©" Alijiuliza kwa mshangao baada ya kuhisi anang'atwa.
"Msaadaaaaaaaaa " Alipiga kelele.
Ndipo Bryant Kobe alishtuka, aliachana na Tasha akakimbia kutoa msaada.
Tasha aliishia kuzishika lips hakuamini kama kapigwa denda kizembe.
Akiwa katika kutafakari jongoo kubwa kupita maelezo lilimpandilia, ukiangalia vibaya utasema ni nyoka.
"Msaadaaaaaaaaa" Alipiga kelele
"Siafu siyo kitu....nenda ukamsikilize Mgeni " Zara aliongea.
Basi Bryant Kobe alimrudia Tasha, wacha ampuuze baada ya kuona jongoo lipo kwenye mapaja yake
"Toa hili dudeeee "
"Kutokana na mafundisho yako ulisema Wanaume wa siku hizi hawawezi hata kuua mende ....... fanya kujiokoa mwenyewe" Bryant Kobe aliongea kisha akakaa pembeni kusikilizia.
Tasha alikusanya ujasiri alichukua pochi yake akalisukuma jongoo kuleeeeee kwa nguvu zote....
Siku ya leo ilikuwa mbaya kwake π£ ndiyo jongoo lilikwenda kule lakini vitu vyote vya kwenye pochi yake vilimwagika, wacha picha ya Bryant Kobe ionekane hadharani alitamani dunia yote igeuke kuwa bahari..........
ITAENDELEA.........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi







Maoni