*AFANDE NILEGEZEE KAMBA ππ«π«* *SEHEMU YA SITA* Kabla hata sijamjibu kitu, akanirukia na kuanza kunishika shika hadi Mwili wangu ukaanza kulegea.
Ninacho jua siku hiyo alinitengeneza kisawasawa. Alikua anafanya utadhani hatafanya tena. Nikaona hapa nisipo toa machozi hawezi kuniacha. Nilijikuta sio kulia tu mpaka kuomba niliomba "Afande tafadhali nilegezee kamba utaniua.....
Akanijibu "ukitaka nikuache sema unafuta kauli yako lasivyo tunaendelea mpaka kunakucha"
Wee mbona Nikakubali na kusema kile alichotaka niseme ndipo akaniacha. Tena alinisukuma pembeni kama mzigo.
"Haitajirudia tena kulala na tapeli! Ni leo tu sababu nilitaka kukufunza adabul..........vaa nguo zako, toka humu ndani Hiki si chumba chako"
Nikainuka taratibu nikavaa nguo zangu kwa aibu Akanipeleka kwenye chumba kingine "hiki ndicho kitakuwa chumba chako" alisema
Eti mimi niwa kulala stoo??? Mimi Ginah??? "Stoo??"
"Nimekuhurumia sana ningekulaza barazanil... ukitaka kuoga au kutumia choo utatumia vyumba vingine, ila kulala ni hapa"
Nilibaki nashangaa Nikamuuliza, "sasa nitalalaje chini? Hakuna hata godoro"
"We tapeli, hapa umekuja kulala??? Hela nitakayo kulipia deni lako utaifanyia kazi haitoki kirahisi! Hakuna pesa ya buree"
Nilihisi vibaya sana "please sijala tangu jana, naweza kupata kitu cha kula?"
"oooh kweli? Subiri kidogo"
Nikafikiri anaenda kuniletea chakula, kumbe akarudi na mihogo mibichi mkononi na maji kwenye kidumu
"hichi ndicho chakula chako. Mpaka siku nitakayo amua kukubadilishia ratibal Alafu inakaa sana tumboni
"Unanitegemea nile mihogo mibichi?"
"kama huwezi acha. Lakini ukitoka hapa, unaenda moja kwa moja selo. Kumbuka makubaliano yetu. Umenielewa?"
Nikainama kichwa nikasema, "ndiyo"
"sasa ratiba yako ipo ivii, Kila siku lazima uamke saa kumi na moja alfajiri. Ukiamka, unasafisha nyumba yote, unapiga deki, unafagia hadi nje ya fence. Baada ya hapo, unafua nguo na vyombo. Nikiamka saa moja asubuhi, nataka nikute tayari umeniandalia kahawa nyeusi (black cofee). Na usithubutu kupika hadi nikikuambie mwenyewe. Utakula mihogo hii mibichi na maji mpaka nikuambie vinginevyo. Umenielewa?"
Nikajibu "ndiyo" kisha Akatoka bila kusema kitu kingine.
Pale pale Nilianza kulia. Nilimkumbuka baba, nilikumbuka nyumbani Nikaanza kujilaumu. Nikaamua nijipe moyo kwamba nimalize huu mwezi mmoja, kisha nirudi kwetu niolewe, maana mateso haya yalikuwa ya kutisha
Nililala nalia mpaka asubuhi. Kumbuka mimi ndiye mtoto wa pekee nyumbani kwetu, nimetoka kwenye familia yenye pesa. Kazi zote za ndani zilikuwa zinafanywa na wasichana wa kazi, mimi sikuwahi kupika, kusafisha, wala kufua. Nilichojua ni kula, kulala na kwenda club.
Na pia sikuwa mtu wa kuamka mapema. Saa kumi na moja asubuhi kwa mimi ndiyo muda wa kurudi nyumbani kutoka club, si muda wa kuamka.
Kwa hiyo nililala mpaka... Elton (OCS) akaamka, akaoga, akajiandaa kuenda kazini. Aliposhuka chini, alitarajia kukuta kahawa yake nyeusi mezani ila guess what?? mimi bado nilikua nimelala! Nilikuwa sijafanya chochote.
Akapandwa na hasira kali. Akaja moja kwa moja
store alikoniweka. Akanikuta bado nimelala. Akaniangalia kwa hasiramaana yeye hawezi kuanza siku bila kunywa kahawa. Akaenda jikoni, akachukua ndoo ya maji baridi akarudi nayo store.
Unajua alifanya nini? Akanimwagia maji yote! Nikashtuka kama nimepigwa shoti ya umeme, nikainuka haraka. Nikamuona amesimama mbele yangu, uso umejaa hasira.
Akauliza "we tapeli unajua saa ngapi saa hizi?"
"samahani, nimechelewa kuamka
"umechelewa kuamka?? Nilikuambia uamke saa. kumi na moja, usafishe, halafu uniandalie kahawa nyeusi. Iko wapi kahawa yangu?"
"naenda kukuandalia sasa hivi!.....sorry......soryy"
Nikaenda mbio jikoni, nguo zangu zikiwa zimelowa maji. Lakini sikua najua hata namna ya kutengeneza kahawa nyeusi! Jiko lenyewe kuwasha ni mtihani. Wakati wote nyumbani
kwetu, mimi sikuwahi hata kuingia jikoni.
Sasa fikiria, nitamtengenezeaje kahawa huyu jamaa mwenye hasira hivi??.
Unajua nini kitatokea?
Nakuja....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi