CAPTAIN MAVERICK NA MISSION YA MAPENZI❤ SEHEMU : 8
" Umejuaje kama kadi zangu zimefungiwa na sina pesa yoyote?" Gabriella alishtuka sana kusikia maverick anajua kila kitu
" Hua unaongea ukiwa umelala hii inachekesha sana "
maverick alianza kucheka
" Cheka ukimaliza Fanya unikopeshe hiyo pesa Nina shida nayo muhimu sana "
" Okay pesa sio shida ila uniahidi sio unaenda kufanya ujinga na utanirudishia sio Bure "
" Sawa nakuahidi nitakurudishia kuhusu matumizi yangu hayakuhusu "
Gabriella aliongea neno la mwisho kwa sauti ya chini
" Umesemaje ?"
Aliuliza maverick
" Nimesema asante sana kaka maverick " Gabriella alijichekesha Maverick aliingia chumba alitoka na kitita Cha lakini nne akamkabidhi Gabriella
Gabriella alifurahi sana hakutaka kupoteza muda alienda kujiandaa na kwenda kwenye Hilo duka Maverick alijikuta taratibu anaanza kumuelewa Gabriella
Zilipita week tatu maverick na Gabriella wakiwa wanaishi nyumba moja
Siku moja asubuhi Gabriella alipokea simu kutoka kwa Monica ambae ni mchumba wa Jonas rafiki kipenzi wa Tristan
" Besti nimekupigia nikukumbushe ile sherehe yangu na babe wangu Jonas itakuwa ni week hii ijumaa usisahau kuja kipenzi " alisema Monica
" Hata usijali mimi na wewe tena kipenzi changu nitakuwa mstari wa mbele "
" Nimesikia kilichotokea kati yako na Tristan pole sana "
" Asante kipenzi nimeshapoa "
aliongea Gabriella huku anatabasamu
" natumai utakuja bila kukosa "
Gabriella na Monica waliagana
" Bila shaka Tristan ataenda kwenye sherehe akiwa na yule mwanamke wake ,natamani nisiende lakini sitaki kuonekana dhaifu nitaenda kwa kishindo "
Gabriella alienda nyumbani kwa Veronica
" Kwahiyo unataka kuniambia utaenda kwenye hiyo sherehe ?" Aliuliza Veronica
" Ndiyo kwanini nisiende ,kwani nimeua au kuna kosa lolote nimefanya ?wakuona aibu ni Tristan na sio mimi "
" Lakini hauna partner na kule kila mtu atakuwa na partner wake usisahau Hilo "
alisema Veronica
" Hilo mbona jambo dogo sana kwangu nimeshafikilia nini Cha kufanya hata usijali shoga angu "
Gabriella aliongea huku anatabasamu akilini mwake alimuwaza maverick
Jioni maverick alirudi nyumbani akiwa amechoka sana alitabasamu baada ya kuona Gabriella anaandaa chakula mezani
" Karibu Rick mtu na roho yake nzuri mjini " aliongea Gabriella huku anatabasamu
" Mmmh najua tu Kuna kitu unatakae hauna lolote "
maverick alivuta kiti akakaa
" Kwani vibaya nikikuandalia chakula na wewe mpaka kuwe kuna kitu nataka "
Gabriella alimpakulia maverick Biriani
" Hiki Chakula harafu yake tu kinaonekana ni kitamu na mpishi Nina uhakika sio wewe Gabzilla "
maverick alimuangalia Gabriella usoni
" Nimejifunza kupika usinizalau bhana"
Gabriella hakuwa mjinga alinunua kile chakula kwenye mgahawa maarufu kwa upikaji wa Biriani na pirau tamu
Gabriella alipakua chakula kwenye sahani yake na kuanza kula walikula mpaka wakamaliza bila kuongea chochote kila mtu alikuwa busy na sahani yake
" Nimefurahi sana Leo chakula ni kitamu sana kupita maelezo ..haya niambie unataka nini maana najua hiki chakula sio Bure " maverick alimuangalia Gabriella usoni
" Mmmmh sio kitu kikubwa sana ila nilikuwa naomba kama utakuwa na muda ijumaa twende pamoja kwenye sherehe ya rafiki yangu "
" Sina muda mchafu wa kwenda huko kwenye sherehe ijumaa ni siku yangu ya ku relax " maverick alitaka kuondoka Gabriella alimuwahi akamshika mkono
" Rick please ..nakuomba jamani ni mara moja tu nawapa hi marafiki zangu then tunaondoka " Gabriella aliongea kwa kubembeleza
" Nimeshasema hapana na huwa nikisema hapana ni hapana kweli siwezi kubadilisha uamuzi wangu "
"unataka nikaaibike mbele za watu si ndo unachokitaka hicho "
Gabriella aliongea huku analia
" Sasa uanalia nini ? Kama hauto niambia kwanini natakiwa kwenda na wewe siwezi kukubali kwenda huko hata ufanye vipi ".
" Nitakwambia kila kitu kama hicho ndicho unachokitaka "
Gabriella alimuelezea maverick kila kitu mpaka kutengana na Tristan
" Pole kwa kilichotokea nimekubali kwenda na wewe kwenye hiyo sherehe lakini sio Bure " alisema maverick
" Unataka nini tena jamani tajiri yangu ?" Aliuliza Gabriella kwa kulalamika
" Chochote nitakachokwambia unipe basi inabidi unipe " maverick alimkonyeza Gabriella akaondoka
" Sijui hata huko kichwani kwake huwa anawazaga ujinga gani ,atajijua mwenyewe Cha muhimu ni kuwa amekubali kwenda " Gabriella alitabasamu
Siku ya sherehe haikukawia mida ya saa1 jioni Gabriella alifungua mlango wa chumba chake alianza kushuka ngazi kuelekea sitting room alikuwa amevalia gauni refu la hariri ya rangi ya baby pink lililombatana na umbo lake kwa ustadi wa hali ya juu. Gauni lilikuwa la mgongo wazi, na mikanda myembamba ya mabegani chini lilikuwa na mpasuo kuanzia usawa wa paja lake la kulia , nywele zake ndefu zilizokuwa zimesukwa upande mmoja zilisheheni marashi yaliyofanya kila aliyemkaribia asimame kimya kwa mshangaoGabriella alitembea kwa mwendo wake wa kunyata wa maringo huku anatabasamu Maverick, aliyekuwa amekaa kwenye sofa ya ngozi, alishindwa hata kupumua kwa sekunde kadhaa baada ya kumuona Gabriella, Alinyanyuka taratibu, macho yake yakimtazama Gabriella kila hatua aliyopiga Maybe alisogea karibu na kumpata mkono Gabriella
" Leo acha tu nikusifie umependeza sana .." maverick alimnong'oneza Gabriella
" Asante hata wewe pia umetoka chicha " aliongea Gabriella huku anatabasamu Maverick alikuwa amevalia suti nyeusi ya velvet, koti lililoshonwa kwa ustadi likiwa na vifungo vya fedha vilivyoakisi mwanga wa taa, na ndani ya koti alivalia shati jeupe la silk lililomletea muonekano wa kipekee. Tai ya batani ya rangi ya dhahabu ilimpa mvuto wa kifahari wa kisasa, na viatu vyake vya ngozi viling’aa kana kwamba vilikuwa vimetengenezwa kwa mwangaza wa mwezi.
Maverick na Gabriella waliongozana mpaka kwenye parking ya magari walipanda kwenye gari na safari yao iliishia nje ya ukumbi mkubwa wa sherehe Maverick alimfungulia Gabriella mlango na kumpa mkono Gabriella aliweka mkono wake kwenye mkono wa maverick alionekana kuwa na wasiwasi sana
" Wasiwasi wa nini mrembo na uko pembeni yangu ,wewe ni mrembo hata ukinuna ila unawaka kama nyota ukiupamba USO wako kwa tabasamu "
" Acha ujinga bhana hata huwezi kubembeleza na lisauti lako Hilo "
Gabriella alimpiga maverick kibao kidogo Cha kifuani
" Basi nitajifunza zaidi kwaajili yako "
maverick alimnong'oneza Gabriella
Gabriella alitabasamu kwa maneno ya maverick waliingia ukumbini kila mtu aliwaangalia kwa jinsi walivyopendezana
" Wow umependeza sana dear "
Monica alienda kumkumbatia Gabriella
" Asante kipenzi hata wewe pia umependeza sana "
Gabriella aliangaza ukumbini kama Kuna mtu alikuwa akimtfuta
" Kuna mtu unamtafuta ? Kama ni Tristan yule pale na mwanamke wake anaejishaua " aliongea Monica huku anamuonyesha Gabriella sehemu aliyokaa Tristan na Silvia
" Sikuwa namtafuta yeye bhana namtafuta shem Jonas Yuko wapi sijamuona "
Gabriella alizuga
" Yupo na marafiki zake utamuona muda sio mrefu ,Huyu Mr handsome ni nani ?" Monica alimuuliza Gabriella
" Jina lake ni maverick au unaweza kumuita Rick ni boyfriend wangu "
Gabriella alimsogelea maverick alimvuta mkono asimame kidogo kwasababu alikuwa ni mrefu kwake maverick aliinama kidogo Gabriella akamkiss kwenye shavu alifanya hayo yote kwakuwa muda huo Tristan alikuwa anaangalia upande wao.....
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi






Maoni