*IN LOVE WITH ZURI* *Sehemu ya 11*
SONGA NAYO......
Haraka haraka nilitoka nje ambako nilimkuta Ethan akiwa ananisubiri, bila kusubiri chochote niliingia kwenye gari na safari ya kurudi nyumbani ilianza, ni mida ya saa moja na nusu hivi
"Dah kuna watu wazuri walah.."
Tukiwa njiani tunaelekea nyumbani, Ethan alianza kuongea nilijua tu amevutiwa na Nancy hakuna kingine
"Ah unajua Ethan me hapa nilipo nimechoka sana, nahitaji kupumzika tu, hizo sifa ulizoziona kwa Nancy nenda ukamuadithie kaka Idress..."
"Nilijua tu, yani wewe ndio unachoniboa hicho.."
Ethan alilalamika, kwa kuwa sikutaka kuzungumza nae nikabakia kimya huku nikiendesha gari langu taratibu, lakini kichwani mwangu nilikuwa namuawaza Zuri tu namna ambavyo nimevutiwa nae huyu mtoto
Hatimae bwana kwa uwezo wa mungu tulifika nyumbani salama Kabisa, kwa kuwa tulikuwa tumekula huko tulikotoka hakukuwa na haja ya sie kula, zaidi tulijiunga seblen kuangalia taarifa ya habari
Muda wote hayo yanaendelea sikuwa natulia kabisa kwenye sofa, yani macho yangu yalikuwa kwa zuri tu na sio kwenye TV, mwamba nilikuwa nimekamatika haswa kwa huyu binti walah
Hawa watoto wa kipemba wakiamua kumkamata mtu wanakukamata haswaa huwezi kuchomoa au kufurukuta labda uwe mzee wa totozi, ila napo lazima ukamatike tu
'Mama me naenda kupumzika.."
Zuri alimuaga mama yangu
"Sawa uwe na usiku mwema Zuri..."
'Nawe pia.."
Alisema kisha na bila kusubiri akashika njia kuelekea chumbani, huku nyuma mie nikibaki nikimtazama tu huo msabwanda wake na kubaki nikimeza mate kama sina akili nzuri
"Goodnight mom.."
Baada ya kuhakikisha zuri ameishia maeneo ya pale seblen na mimi nikamwambia mama usiku mwema, mama bila hinaya akajibu na bila kusubiri nikashika njia mpaka chumbani kwangu na kubaki nikizunguka tu
Nilizunguka kama dakika tano hivi nikasogelea
kabati langu na kutoa moja ya gauni, zuri sana hili gauni nililinunuaga miezi miwili iliyopita kwa ajiri ya kumkabizi Zuri
Ila kutokana na aibu nilizokuwa nazo nilishindwa
kabisa hata kumkabizi zawadi yake, sasa siku hii ndio nimelitoa baada ya kukaa sana kwenye kabati
Basi nikalichukua na kuliweka kwwenye mfuko flan hivi ambao ni maalumu kwa zawadi kisha nikaingia bafuni na kuoga, baada ya kuoga vizuri nikapiga pamba zangu nilijua fika Zuri akiniona hawezi kuchomoa
Basi nikavaa zangu bila kusahau unyunyu aweee nikajipulizia pale kisha nikabeba mfuko wangu wa zawadi na kutoka, ile natoka tu nakutana uso kwa uso na Ethan nae ndio alikuwa anaenda chumbani kwake kupumzika
"Mh, unaenda kwa shemu nini..??"
Huyu kijana huwa hawezi kukaa kimya kabisa, nilichofanya ni kumkalia kimya kisha nikaondoka zangu nikimuacha akiwa ananiangalia tu
Basi bwana nailiweza kufika kwenye chumba wanachotumia na kuanza kujiuliza uliza sijul nibishe au vipi, nilikaa pale kama dakika tano nikaamua kugonga mlango
"Ingia..."
Sauti tamu ya Zuri kutoka chumbani ilisikika, sikutaka kuingia kirahisi hivyo nikagonga mlango mpaka mara tatu akatoka akiwa amechukia sana
"Ila Anita sijui unapenda kunisumbua tu, mtu nakwambia ingia bado unaendelea kugo..."
Alinyamza baada ya kuniona ni mimi
"Ah kaka Frank..??"
Aliishia kuongea hivyo, kwa muda huo mimi mikono yangu yote niliiweka nyuma ya mgongo wangu, hivyo hakuona ile zawadi
"Nimekusumbua ee..??"
Nilimuuliza
"Ah hapana hapana.."
'Ohoo sawa me nilikuwa napita tu ila kuna zawadi yako nimekuletea hapa, nilienda kule kutembea tembea nikaliona hili gauni nikaona so mbaya kama nikikuletea..."
Nilisema huku nikimkabizi.......
Itaendelea..
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni