NAKUPENDA BILA MIPAKA 158 -- 160
Aliendesha na kuniambia “nisamehe kwa kukuteka asubuhi, nisamehe maneno yalinitoka asubuhi lakini ilikuwa lazima nifanye vile. Wewe katoto ni kabishi sana. Huna hata huruma unataka mtu mzima mpaka nipige ukunga.”
Nilimtazama, anaongea anatabasamu, anatabasamu zuri sijawahi kuona akitabasamu. Si unajua huyu cha kuvimba, cha kuna, Mr serious eenh, nilijikuta nacheka na yeye akacheka akisema “umenilaza nje kweli, Haki ya Mungu Nazwi huna huruma.”
Nikacheka na kusema “nisamehe, sikujua. Nisinge kubali ulale nje kiukweli. Nisamehe sana na kuhusu utekaji nitafikiria lakini nina ushuhuda boss.”
Akanitazama na kucheka kidogo akisema “eti nina ushuhuda, eneh ushuhuda gani tena?”
Nilitabasamu na kusema “leo wakati nikiwa jikoni nilipokea mzigo, nilipoenda kutazama ulikuwa na Abaya nzuri za ndoto zangu kusema kweli namshukuru sana Mungu.”
Akacheka na kusema “muone.”
Nilicheka tu na akasema “Unaweza kuniita Gallen?”
Nilimtazama kwa sauti ndogo nikasema “Mr serious.”
Akacheka akisema “whaaaat!!”
Nilimtazama na kusema “whaaat, Mr Gallen, Mr Gallen.”
Akacheka, Nilitabasamu.
Ni kama ndoto lakini ndiyo uhalisia, unaweza ukamuona mtu ana ringa, hataki kuongea na watu kumbe wala hata, kila mtu ana watu wake. Mr Gallen kumbe ni mtu wa furaha tu ila akiwa na watu wake pengine.
Bado tukiwa tunaendelea na safari, nilikuwa nimetulia tu, mawazo juu ya rafiki yangu yalikuwa yananizidia hata Mr Gallen tukiwa kwa foleni aliniita jina langu akisema “Nazwi, unaweza kuniambia nini kinakusumbua?”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:159
Nilimtazama na kushusha pumzi nikisema “hakuna shida hata.”
Alinitazama akisema “nikuteke tena au utasema.”
Nikatabasamu na kusema “ni kuhusu tu rafiki yangu, dada yangu anapitia wakati mgumu sana na mama yake.”
Alinitazama akasema “mama yake?, nini tatizo?”
Na alianza kuendesha tena, mimi nilianza kumuelezea kwa maumivu. Hata aliniambia “relax!!, relax!! Nakuelewa. Hii ni mbaya sana. Lakini hana haja ya kumkimbia labda kama akiona mazingira haya hayamfai kwasasa. Anaweza kufanya jambo na kila kitu kikawa sawa.”
Nilimtazama na kusema “afanye nini sasa.”
Alitabasamu na kusema “naweza kukutana naye si ndiyo?”
Nilimwambia kwa upole “bila shaka ila nitaongea naye kwanza maana nimekwambia hata bila ruhusa yake pengine hatopenda.”
Aliniambia kwa upole “ni kweli, ni kweli kabisa. Umefanya vizuri basi itabidi ufanye hivyo.”
Nikatabasamu na kusema “labda kesho.”
Akasema “ni sawa.”
Nilimtazama na kusema “na nilisahau kesho ni jumapili mapumziko. Mama itakuwaje?”
Alishusha pumzi na kusema “hata mimi sitaki iwe jumapili. Nitaongea na mama. Lakini si uje tu kwani unaenda wapi?”
Nilisema kwa upole “hapana, nipumzike sijapata siku ya kupumzika.”
Aliniambia “upo sahihi.”
NAKUPENDA BILA MIPAKA:160
Yaani tunaongea kama tuna mazoea vile kumbe wala. Hapa hatujaongelea busu hata kidogo. Tulinyamaza tena mpaka tunafika nyumbani. Alisimamisha gari kigizagiza cha saa mbili tena. Nikawa nataka kushuka aka funga milango.
Akawa ananitazama nikatabasamu na kusema “utekaji tena?”
Alinitazama tu na halafu alisema “Hey, Nazwi, nisamehe kwa kilichotokea ofisini.”
Nilijikuta napoa, aliniambia tena “Sijui, sielewi. Nashindwa kujizuia kabisa.”
Nilishusha pumzi na kusema “Tusahau hilo. Naomba niende.”
Akanishika mkono na kusema “una hakika unataka tusahau?”
Nilishindwa hata kumtazama. Akaniambia kwa upole “Nawezaje, Siwezi kusahau, I need More and more. Please can we?”
Enh, Muanko anataka vagi lirudiwe, sikuweza hata kumjibu, alisogea kidogo alinishika uso kwa upendo na mikono yake mizuri. Unashikwa tu unaona hapa ni sehemu yangu salama, unajua unahisi ule upendo halafu akasema “una midomo mizuri, una macho mazuri sana, ona sura yako you are so cute.”
Hata sijajibu, tayari alichukua midomo yangu, nilifumba tu macho yangu, alinibusu kwa muda na aliniachia akisema “hata sitosheki, ila unatakiwa kwenda.”
Ni kweli mama yupo nje na Priya. Niliinamisha kichwa changu, nikawa nataka kufungua nitoke. Aliniambia tena kwa upole “Nilishakwambia relax, am here for you Nazwi.”
Nikatabasamu, akaniambia kwa upole “kuhusu dokta, usimzoee, achana naye, fuata mambo yako.”
Niliitikia. Akashuka, akanifungulia mlango na kutoka zangu. Akaniambia “nakupeleka.”
Hata kugoma naweza sasa, kwanza hapa nipo hoi mwenyewe, natamani tena na tena na tena. Tulifika mpaka kwa mama na dada Dorice akawa anatoka. Aliponiona alitabasamu. Mama alisimama, Priya akasalimia “Shikamoo.”
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



Maoni