MPISHI ANA UTAMU WAKE SEHEMU YA 17 – 18
Ila macho yangu hayakufanikiwa kuninasa kabisa.
Nilifanikiwa kuliona ua nililoliona siku ya kwanza nilipoingia ikulu humu, nikaishia kulitazama na kurejea chumbani kwangu.
Ajabu sikumkuta tena mfalme Jampioni ndani ya himaya yangu, hivyo nilifahamu yupo na mkewe wananyanduana usiku huu.
Sijui ni hisia gani nizipatazo ndani ya moyo wangu, sidhani kama ni wivu Amara mimi siwezi kuwa na wivu hata kidogo hasa kwa mwanaume nisiyempenda.
Ni kama nilikuwa nikijifariji tu, ni wazi sikuhitaji mfalme aondoke upande wangu, mara zote nilihitaji awe upande wangu ilihali si halali yangu.
Upande wa nyumbani anaonekana baba akiwa kwenye chumba chake cha maabara akiwa ameshikilia kile kifaa.
Kuna baadhi ya kemikali na mambo aliyokuwa akiyafanya juu ya kile kifaa.
Basi upande wangu huku nikajikuta naumia tu ni kama vile nakaribia kukata roho kama navutwa ama laah.
" Bado tu mume wangu, sitakuelewa kama Amara wangu hatarudi ndani ya wiki hii " alisikika mama Amara akizungumza.
" Nipe mida mke wangu nakubali nimetengeneza kifaa na kukihifadhi kizembe hadi kimemdhuru mwanangu ila si wa kulaumiwa peke yangu. Una makosa pia katika hili " alizungumza baba huku akimuangalia mkewe.
Basi namna mama hapendi kulaumiwa akaanza kuangua kilio.
Baba akaingia jukumu la kumbembeleza mama akaachana na kile kifaa. Hapo kidogo moyo wangu ukatulia ile hali ya kuvutwa ikakata kabisa.
Ikapita miezi na wiki zikawa zinazidi kwenda kasi....
Siku moja nikiwa jikoni naandaa supu kwaajili ya mfalme, nikaanza kuhisi kichefuchefu wacha nikimbilie nnje kutapika.
Sikutaka kuamini kama Amara mimi mpenda nyama leo hii naikinai ama ni mazingira mapya ? " Nilijikuta nikijiuliza.
Sikutaka kupiteza muda, siku hio sikuonja nyama wala radha ya pishi langu.
Nilipohakiki limeiva nilitenga kweye vibakuli kisha nikaelekea chumbani kwa mfalme.
Sikuona haja ya kugonga hodi kwa namna nilivyomzoea, ukizingatia mechi za kuchosha viungo anazonipatia sikuwa na wasiwasi.
Kama nilivyotegemea hakushangaa kuniona zaidi alinifurahia, nilimtengea na kukaa kando yake nikisubiri maoni ya nilichokiandaa.
Ajabu nikaanza kuhisi kichefuchefu kila alipopandisha kijiko cha supu mdomoni mwake.
" Aaaaasssssh " alisikika mfalme akilalamika pale nilipotapikia chakula chake.
" Una shida gani mama angu ? " Aliuliza mfalme.
Basi nikashuka chini kuomba rehema, namna alivoniwekea uso wa serious mazoea yakakata ghafla hapo nikaanza kuomba msamaha mbele zake.
Naweza sema upendo ama laah, mwanaume huyu hajui kununa eeeeh ?
Alikuja kuninyanyua na kuniketisha kando yake.
Haikuchukua muda kamanda kauzu alifika na mganga mkuu wa ikulu basi nikaanza kupimwa.
" Hongera mbinti una ujauzito wa miezi mitano " alizungunza mtabiri huyo huku akitabasamu.
" Ni mimi au mfalme ? " Nikauliza ni wazi nilikuwa nimevurugwa.
Nilizidi kwenda viral pale nilipogundua mfalme anakenua meno yake.
Wacha nianze kupiga kelele na kumrushia mito mfalme.
Mganga mkuu hakuweza kuhimili fujo hizo hivyo aliondoka.
" Shida nini mama ?, naenda kuitwa baba ni utukufu huu hakika " alizungumza mfalme huku akirukaruka kwa furaha.
Nilipoona ananikwaza nilimtoa nnje, japo ni chumba chake ila alikuwa mpole mie ndo nkawa mtawala 😀.
Taarifa za mimba zilipomfikia malkia Dorcas hakuonekana kushangaa ni wazi alilitambua.
Malkia waita alionesha fujo na jazba punde aliposikia habari hizo.
Hivyo akafunga safari moja kwa moja hadi kwenye chumba cha mfalme.
Nini kitajiri ?.
Endelea kufuatilia
SEHEMU YA 19 - 20
" Nitaitoa mimba ya huyo kimada sitakubali aniondoe kwenye jimbo langu kilaini namna hii " alizungumza malkia waita huku akizidi kuchanja mbuga.
" Si ajabu eeeh uliyoyasikia ?, sitegemei kusikia umefanya fujo kwa huyo kimada wa ikulu, kwanza asikusumbue mke ni mke tu na kimada atabaki kuwa kimada daima, japo sheria ipo wazi malkia asipozaa ndabi ya mika 10 anavuliwa cheo chake ila usijali nitaipindua sheria hio kwajili yako, sitafanya hivyo bure..... ila kwa sasa rudi chumbani kwako " alizungumza malkia Dorcas.
" Queen Dorcas ni mtu wa ajabu sana inaonekana, hajulikani ana akili za namna ipi kwani mara nyingi huingilia mbinu za malkia waita na kumzuia kufanya uhalifu ".
" Nitamuua kimada huyu endapo nitamkamata " alizungumza malkia waita huku akirudi kwa hasira chumbani kwake miguu yake akiipiga piga chini.
Siku zilienda tumbo langu likiwa linazidi kuwa kubwa.....
Kumbukumbu zangu za maisha yangu ya zamani familia na kilakitu zikaanza kunirejea nikiwa huko.
Hatimae mimba ikafikisha miezi tisa sasa.
Nikiwa juu ya kifua cha mfalme nikideka baada ya sita kwa sita nilishangaa nikitikwa na maji maji sehemu nyeti yakiambatana na maumivu.
Wacha nipige ukunga wa hatari.
Haikukuchua muda mganga mkuu alifika mahala pale kama mjuavyo kauli ya mfalme ni sheria ndivyo ilivyokuwa kule.
Basi shughuli ya kunifungulisha ikaanza wale wanawake walioingia leba ama wanaume walioshuhudia mtoto akizaliwa mnanielewa vema hakika.
Upande wa nyumbani anaonekana baba angu akiwa maabara sambamba na mama yangu.
" Lazima nipate matokeo mazuri siku ya leo nimehangaika kwa muda sasa " alisikika baba akizungumza huku mama akiwa anamuangalia kwa macho yaliyokata tamaa kabisa.
Shughuli ya kunizalisha iliendelea huku nikisikia maumivu ya hali ya juu.
" Sukuma sukuma " sauti za wakunga zilisikika zikinitaka nisukume mtoto atoke.
Japo nilijitahidi kwa hatia za mwanzo ila nikaonesha kuzidiwa na kuishiwa na nguvu.
Sifahamu nini kilijiri, kufumba na kufumbua nilijikuta kwenye dunia na mahala nilipopazoea sana.
Hapakuwa pageni kwangu, ni pa simenti si pa mbao na panavutia sana si pengine bali nyumbani kwetu.
Palibadilika kiasi tu.
Nilijikuta nikitabasamu pale nilipotazama pembeni na kumkuta mama yangu na baba yangu wakinutazama ni kama walikuwa wakinisubiri kwa hamu sana.
" Mama, baba !! " niliita. Basi wakanisogelea na kunikunbatia kwa upendo.
Maswali ya wapi ulikuwa nini kilijiri na niliishije hayakuisha siku hio.
Niwambieni tu, manake kwanza nicheke😀, niliwajibu na kuwahadithia yote isipokuwa yale ya minyanduano ni aibu kwa kweli.
Naina kuna jambo nimesahau kuwaambia na ni hili ;
Kule buana sijui korea au wapi nilifanikiwa kujifungua mtoto mzuri wa kiume na mwenyw afya.
Kutokana na mvutano na mambo ya kitaalamu ya baba, mwili wangu ulibaki kule na roho yangu ikaja huku, hivyo kule ilijulikana nimefariki japo mtoto alitoka salama.
Mfalme Jampio haishi kunikumbuka utamu wake wa bei ya jioni.
Kila akiniwaza haachi kunena " ama kweli nilimpata mpishi mwenye utamu wake ".
Upande wa malkia waita ilikuwa ahueni kwake pale nilipofariki ni wazi alikuwa akinichukia kupitiliza.
Malkia Dorcas aliiingia jukumu la kumtunza mjukuu wake aliyepewa jina ATASA 😀 kwa kuhofia huwenda waita atamdhuru kwa chuki zake.
Tukiachana na hayo hivi sasa nipo home japo ni muda mchache ila nimepata bwana wa maana kaelewa show na anataka kunioa mie, ni kama niliondoka na baraka za kule.
Yote kwa yote acha ibaki kuwa historia tu ila sitakuja kusahau yale niliyoyapitia, ama kweli sayansi ipo na Mungu yupo tusidharau hivi vitu.
THE END BY JJL STORIES 🥰.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

