VYOTE NDANI GONGA94
MPISHI ANA UTAMU WAKE SEHEMU YA 7
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
" Ni jani hili ama hua hakika, japo silifahamu ila limenivutia "nilizungumza kisha nikaondoka nikiwa na hilo ua mkononi mwangu.
" Ni marufuku kwa kijakazi ama mkazi wa ikulu kuchuma chochote ndani ya jengo hili, mali zote ni za mfalme wa himaya hii " nilisikia sauti ukingoni mwangu ikizungumza.
Ile kugeuka., si ndo kumuona mlinzi kauzu, wacha nianze kutimua mbio .....
" Naona bahati haipo upande wangu " nilizungumza huku nikisimama nikikodoa kwa aibu pale nilipogundua nimezungukwa na watu ambao naweza sema majemedari wa zamani enzi hizo...vile nilikuwa sielewi nikaamua nitulie kusomewa mashtaka.
" Ni vema kama utanifuata kwa hiari yako ama laah nitatumia nguvu " alizungumza yule kamanda mtukutu....sikuwa na budi zaidi ya kumfuata..hapo nimenywea mapepo yote pembeni..Amara mimi siamini nilipoa kupita maelezo ๐, ni vile sionekani ama laah huwenda ningekuwa kituko machoni mwenu wasomaji.
" Mtukufu mfalme, mbele yako tupo wajakazi wako watiifu " alizungumza kamanda kauzu.
" Napokea mashtaka yenu " ilisikika sauti ikijibu.
Unadhani kipo nilichokielewa, fanya kama mnaniona hivi mie Amara form four felia ๐ aiseee ni balaa.
" Mbele yako tumemleta mpishi mkufunzi wa ikulu, kabobea kwenye upishi wa kila chakula " alizungumza kamanda kauzu.
" Sawa mwaweza kunyanyua vichwa " alizungumza mtu aliyesemekana ni mfalme..
" We mwehu ni mfalme ama nakosea huwenda sioni vizuri " nilizungumza kwa sauti, ile sijakaa vizuri nilishtushwa na mtama wa pembeni...wacha nikae chini kuugulia maumivu ya makalio ๐.
" Uwe na heshima ni marufuku kufungua mdomo mbele ya mfalme bila ruhusa yake, ni vile u mgeni mahala hapa lasivyo ningekukata kichwa na kuwapa fisi " alizungumza kamanda yule.
" Ni kauzu huyu zaidi ya dagaa hakika, hashindwi kunikamua kiumbe huyu " nilijisemea kimyakimya huku nikijiokota pale.
" Mwaweza kuondoka mahala hapa nitawapokea tena siku ya kesho, namna nina uchovu siwezi kuwasikia " alizungunza mfalme huyo huku akijitupia kItandani.
" Ni wazi viuno vyangu vilimpagawisha vilivyo na ile dog niliyompatia " nilizungumza.
" Unasema nini wewe nini dog ? Ni lugha gani unayoutumia wewe " aliuliza yule kamanda mstaarabu....nikaishia kumuangalia tu bila kumjibu yoyote...moyoni mwangu nikishukuru kutosikiwa na kauzu ama laah angenikata kichwa hakika.
Nakuja
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mpishi-ana-utamu-wake-sehemu-ya

