MUME WA RAFIKI YETU Episode 1
Ilikuwa ni wikiendi tuliyoingoja kwa hamu sana. Kwa majina naitwa Chautamu, mimi na rafiki yangu Aggy tulikuwa tumechoka na kelele za jiji, maisha ya haraka na mihangaiko ya kila siku. Tulihitaji kupumua. Na ilipokuja mualiko wa Sandra rafiki yetu wa karibu kabisa tulijua hiyo ilikuwa nafasi ya dhahabu. Wazungu huita golden chance .......
Sandra alikuwa ameolewa na kuhamia kijijini kwa mumewe, maeneo ya milimani kule Mbinga. Mara kwa mara alikuwa akitutumia picha akiwa kwenye mandhari ya kijijini, bustani ya kupendeza , na nyumba yao yenye paa la bati jeupe inayometameta juani. Tulijua Sandra anaishi maisha ya amani.
"Tunaenda lini kumtembelea shemeji na rafiki yetu sandra ?" Aggy aliuliza siku moja tukiwa tunakunywa wine nyumbani kwangu. Yeye na mimi tunapenda sana kuwa pamoja na kitu tunachokipenda ni utamu wa bakora tunyime kila kitu ila sio kiboko tunapenda sana....
Na kutokana na hivyo tumeliwa sana ndogo tena muda mwingine ndogo yangu inaliwa na mchumba wake na yake inaliwa na wangu hata hatukuoneana wivu ....
Endelea sasa ....,.
"Ndio maana nime kuita ," nikamwambia kwa tabasamu zito katutumia . "Kesho tunapanda basi, safari inaanza."Alitabasamu sana Aggy na kusema kuwa kesho ni lazima twende uko lengo letu ni kwenda kumsalimia rafiki yetu na kitu kingine tuliambiwa wanaume wavijijini wako vizuri kwenye michezo ya kusaka kunguni ...
Tuliondoka asubuhi na mapema. Safari ilichukua saa kadhaa, tulipitia milima, mabonde, misitu na vijiji vya kuvutia. Mwishoni, tulifika kwenye kituo cha mwisho ambako Sandra alitufuata kwa pikipiki iliyoegeshwa pembeni ya barabara. Kisha akatubeba hadi kwake ....
"Karibuni nyumbani kwangu jamani!" Sandra alitukaribisha kwa furaha, macho yake yakitabasamu kwa upendo ule ule tuliomzoea naye mjini.
Hatukujua kuwa muda mchache ujao tungekutana na kitu kilichotufanya tusahau hata uchovu wa safari.
Tulipofika nyumbani, mlango wa mbele ulikuwa wazi kidogo. Kulikuwa na harufu ya kahawa iliyokuwa inachemka jikoni. Lakini kilichotushangaza zaidi siyo kahawa, bali sauti nzito na ya kuvutia ya mwanaume aliyekuwa akipiga miayo ya nguvu akitokea uani.
Tuligeuka wote kwa wakati mmoja.
Alikuwa anakuja mbele yetu taratibu, mwili wake umetoka mazoezini jasho linamtiririka mabegani na kifuani, shati lake jeupe la kubana limezama kwenye misuli yake kama limechorwa juu ya mwili. Alikuwa amevaa bukta fupi ya kijivu iliyomuacha mapaja wazi mapaja yenye nguvu, yaliyobeba historia ya mazoezi ya miaka.
Macho yake yalikuwa kama ya simba anayechunguza mawindo. Ndevu zake fupi zilizonyooka vilivyo zilikuwa zimeshika tone la jasho kwenye kidevu. Alipotuangalia, alitabasamu taratibu tabasamu la mtu anayejua kuwa ana mvuto na ana mamlaka.
“Honey, hawa ndio marafiki zangu wa mjini niliokuwa nawasimulia. Huyu ni Chautamu na huyu ni Aggy,” Sandra alisema kwa furaha.
Shemeji Erick alitusogelea na kutupa mkono mmoja mmoja.
“Karibuni sana nyumbani kwetu. Naitwa Erick,” alisema kwa sauti iliyojaa ukomavu na utulivu. “Mmefika salama?”
Tulijibu kwa nyuso za tabasamu lakini mioyo yetu ilikuwa haijatulia. Mimi, Chautamu, nilihisi joto lisilo la kawaida, mkono wake ulipogusana na wangu. Ulikuwa wa joto, wenye nguvu, na wenye msisimko fulani ulioanzia kwenye vidole hadi kwenye mgongo.
Aggy naye alionekana kupigwa na butwaa, japo alijaribu kuficha. Alimwangalia Erick kwa haraka, kisha akatazama chini kana kwamba aliwaza jambo ambalo hakutaka ninyi wengine mjue.
Tulipoingia ndani, Sandra alituonyesha vyumba vya wageni. Kila kitu kilikuwa kimepangwa kwa utaratibu. Dirisha lililokuwa upande wa kitanda changu liliangalia moja kwa moja uani – uani ambako Erick alionekana muda mfupi baadaye, akiwa sasa hana shati kabisa, akifanya mazoezi ya kukimbia mahali pale pale. Misuli yake ilirukaruka na ngozi yake iling'aa kwa jasho.
Nilishindwa kujizuia. Niliangalia kwa muda mrefu.
Nilihisi hisia ambazo sikuwa nazo awali. Shemeji alikuwa zaidi ya kawaida. Alikuwa ni mwanaume kamili, wa kuvutia, asiyehitaji hata kuzungumza ili kukushika akili.
Lakini huyu ni mume wa rafiki yetu Sandra…
Nilitazama dirishani, na ghafla macho yangu yakakutana na ya kwake. Erick alikuwa amenikamata macho. Hakuyatoa. Tabasamu lake taratibu likaanza kuchanua… kisha akaniinamia kwa kichwa,
Nilihema pole pole. Nilifunga pazia. Huku mapigo ya moyo yanakimbia ......
Ngoja tusubiri Episode ya 2...
Watu wote wanaopenda kazi zangu wapo humu ambako ndiko kuna simulizi zangu zote kama ni mgeni utanijua kupitia humu ......hakikisha unanifollow
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni