MY HOT PILOT* (rubani wangu🔥) EP 11.
MTUNZI: SMILE SHINE
Mama alipokea nikamuita atoke nje,vicram alibaki tu akinishangaa, mama alitoka akatukalibisha ndani, niliomba niongee nae pembeni, tulitoka nililia Kwa mama mpaka na mama nae akaanza kulia, badae nikaamua kutulia nisimuumize mama yangu zaidi...
Nilimbembekeza nikamwambia plan ya vicram, mama alinihurumia mno,ila mama usijali Nina uenyeji kiasi mama Fatuma alinipeleka, naomba nikuachie simu yangu kubwa uifiche na uongee na mama Fatuma, atusamee Kwa ajili ya baba, amekisea sana, nilimpa no ya Siri na Kila kitu, nilimwambia pia Nina nyumba nimepewa na mama Fatuma, nitamuomba aitafutie mpangaji, afu pesa wawe wananiwekea kwenye acount yangu, Ili inisaidie huko ninakokwenda sijui pakuanzia, tuligongea mengi tukagawana pesa na namna ya kunisaidia endapo nitakuwa kwenye hatali nilichomia line Moja nikadondoka nayo Moja nikamuachia mama...
Vicram aliingia kumuaga Mzee, na uyo mwenzako Yuko wapi? Yuko na mama nje nafikili wanaagana, walipeana na pesa, apo Mzee akafurahi kweli, akatamani hata kubeba mkwe wake, Hawa mbona hawaji tutoke huenda wanalia, baba aliongea ikabidi watoke muda huo Mimi tayari nilikuwa kwenye gari namsubili vicram aje tuondoke, walitoka wakakutana na mama mlangoni anaingia ndani...
Mama milembe, uyo binti Yako Yuko wapi? yupo nje anamsubili mwenzie waondoke, nini? Inamaana haagi? Mama hakujibu kitu, ilibidi watoke nje wakaangaza hawanioni kumbe nipo ndani ya gari vicram akahisi wakaja kwenye gari, wakaniona, nikavunga tu, salha mke wangu njoo umsalie baba Yuko apa nje tuondoke, nilimkata jicho nikajikaza nikatoka nakusalimia kishingo upande na goti langu Hadi chini...
Mwanangu msafili salama, ukamuheshimu mme wako, na namba ya simu Yako nipe, nikajibu sina, wote wakanishangaa, nikajibu tu imevunjika, " baba usijal tukifika nitamnunulia Kisha nitakutumia namba zake muwasiliane, Mzee alijiongeza kuwa bado ninahasira nae, niliamua kuingia kwenye gari wamalizane wenyewe, baba aliamua kuniongelesha kisukuma Ili vicram asisikie,milembe usiniletee zalau nitakupigia mbele ya mme wako, umepata mme mzuri, unaleta kiburi Sasa kosa anipe malalamiko Yako, ukiachika ujue nakuozesha Kwa Mzee kurwa alikuwa anakutaka, kazidiwa tu mahali na huyu kijana Sasa kachezee ndoa Yako, nitakulaani hii ndoa ukiivunja Kwa ujinga wako hutokaa ukaolewa na mtu wa maana tena, Mzee aliongea hivyo huku alitena na mate chini kama ishara ya kiapo Cha radhi...
Nilijikuta nalia tu, Mzee akaondoka vicram alishangaa nalilia nini make hakuwa anaelewa kisukuma kabisa,tuliondoka kuekekea mwanza Ili tuwahi ndege ya jioni kwenda dar, tulifika tukaunga, salha mke wangu changamka basi, unalia muda wote mwisho utapata homa, Mimi sina shida niamini angalau hata kiasi...
Niliamua kupiga tu usingizi tumefika dar, ndo akaniamsha, akanipitisha mahali nikashangaa huku wapi? Nyumbani Kuna Sheree yetu hivyo tunapita utest nguo ya Sheree, nilichoka, tumefika bahati nzuri nilipata tena ilinipendeza mno, nikapigwa mecup,japo sikuwa na furaha ila nilipendeza mno, vicram alikuja kunicheki, kwanza akaganda, mpaka wakamshtua alijikuta amenikumbatia Kwa hisia mno, Kila mtu akamcheka...
Alinishika mkono tukapanda ndinga ya maana, hao mpakaaa ukumbi ulipo ulikuwa ni nyumbani tu, kumbe adi mama Fatuma alialikwa na king pia, tuliingia sikuwa na bwebwe kabisa Yani nilikuwa najilazimisha tu, muda wa zawadi nikamuona mama Fatuma na king aisee nilishindwa kujizuia nilimlilia mama angu huyu, mpaka akajuta kuja, tulilia pamoja, ilikuwa ngumu mno kunituliza, ilibidi wanitoe kidogo, king alikuja macho yake yalionekana kabisa Amelia sana, alikuwa pembeni analia kimya kimya, nilishang'aa huyu ananihurumia ama anamlilia mama🤔...
Nilikosa jibu badae mama alifanikiwa kunituliza aliomba aongee na Mimi tu, wote walitupisha tuligongea vingi ni Siri jamani, mtavijua badae, lakini Kuna hiki kilinishangaza, mama alinambia king Toka apewe taarifa zangu alizimia, na alivyopata fahamu hajaamini mpaka wamekunja wote, na hapo hayuko sawa kabisa nahisi anakupenda ila alikuwa anaficha Sasa hili kwake kimekuwa gumu, nilishangaa kwanza, ikabidi aitwe alikuja hata nguvu ya kuongea hakuwa nayo akazima aisee nilichoka...
Itaendelea...🔥
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni