*NIMEKOMA MIMI π* Chapter 10 Basi turudi kwenye ile pati. Yule jamaa aliyenisukuma kwenye pool alifukuzwa
Bishop ni mtu ambae hapendi mtu wake & vijana wake waumizwe au kudharauliwa! Huwa hawezi kuvumilia.
Haya Baada ya hapo pati ikaendelea kwa masaa mawili au matatu ivi alafu ikaisha. Kabla sijakaa sawa Tobias akarudi chumbani akaniambia, "Bishop anakuita"
"Kwani kuna tena?"
"Sijui, ila amekuita chumbani kwake mwenyewe
Nikasimama nikiwa natetemeka "Tobias, naogopa. Itakuwaje kama amejua mimi ni mwanamke? Ataniua siyo?"
"Nilikwambia uwe makini, mbali na ilo nilikuambia uondoke kabisa! So kitakacho tokea leo sina cha kukusaidia Akanlacha, akaondoka zake
Nikasema mbona nimeyabananga leo Mungu nisaidie! Nikavaa kofia nyingine haraka, nikatoka kuelekea chumba cha Bishop. Nilipofika nikagonga mlango taratibu. Nikasikia sauti yake nzito kutoka ndani ikisema "Ingia"
Kwani nili weza kuingia sasa?? Nilinata pale mlangoni kwa dakika moja ndipo nikajikaza na kufungua mlango Nikaingia kwa upole.
Nilimkuta amekaa kwenye meza anakunywa wine. Akauliza "Unaendeleaje?"
"Niko sawa, najisikia vizuri sasa"
"Good" then akanitazama kwa macho flani iviii ya mahaba nigaragaze. Macho yake yakatua kwenye lips zangu, akakumbuka tukio la pale kwenye swimming pool. Ghafla akashtuka na kusimama kama kapigwa shoti
Mnajua mpaka yeye mwenyewe akajishangaa maana haikuwa kawaida kwake kufikiria kiasi kile. Mbaya zaidi alikua anawaza lipsi za mwanaume mwenzie
Ndani ya dakika zile zile akabadilika akaniangalia kwa macho makali "Toka"
"Sawa" huyoo nikatoka mbio hata nyuma sikugeuka. Sikujua sababu haswa ya yeye kuniita lakini nilifurahi kwa sababu hakuniuliza lolote la kunitisha.
Basi Nikatoka moja kwa moja, nikaenda jikoni. Kule kulikuwa bado kuna chakula kilicho bakia kwenye pati, nikajipakulia zangu, nikala nikashiba kitumbo ndiii alafu nikarudi chumbani kwangu.
Kitu kingine kilicho sumbua kichwa changu ni kuhusu Michael. Yani nilim-miss vibaya mno Labubu wangu ivyo Nikampigia tena simu na bado hakupokea
Nikamtumia sms nyingi kama mvua na bado hakuzijibu. Nikapata hofu huenda kuna jambo baya limempata! Kwani haoni missed calls zangu na sms akazijibu?? Nilichoka mimi nikaona heri nijilalie zangu,
Sasa Asubuhi ya saa kumi na mbili, Bishop. akaamka. Alitaka kutoka peke yake kuna mahali alitaka kwenda nahisi pengine ni gym.
Alikuja moja kwa moja chumbani kwangu kuniamsha ili nimfungulie geti atoke. Aliponiita sikuitika kwa maana mda huo nilikua bafuni naoga.
Tangu nianze kuishi ndani ya ile nyumba yenye wanaume kila kona, nilichagua niwe naoga asubui mapema wakati wao wamelala ili nioge
kwa uhuru.
Mnajua kwanini?? Kwasababu wana tabia ya kuingia chumbani bila kugonga na hawa shindwi kuja mpaka chooni.
Sasa kwakua Bishop aliona kimya hajibiwi si akafungua mlango bhana! Na sijui ilikuaje sikufunga mlango kwa funguo
Mwamba hakuishia hapo, akaingia kabisa ndani ila hakuona mtu. Alikuta tu kitanda kimetandikwa vizuri na pale kitandani kulikua na uniform zangu na nguo za ndani. Kilicho mshangaza zaidi ni kukuta nguo za ndani za kike
"Hii siya kike hii??" Aliinyanyua akaiangalia na kuirudisha kitandani. Akiwa ndani ya maswali akasikia sauti ya maji yakimwagika bafuni.
Kwaakili yake alihisi pengine nimeingiza pisi ivyo akasogea taratibu mpaka kwenye mlango wa kuingilia bafuni. Alitaka kuhakikisha tu kama nilikua naoga na demu wangu au laa ivyo akafungua mlango taratibu akachungulia.
Akaambulia kuona mgongo flanii ivii wa maana, alafu kiuno nyigu. Wew akashindwa kuvumilia akafunga mlango kisha akatoka nje mapigo ya moyo yakimuenda kasi. Bahati nzuri hakuniona uso icho ndo ninacho kishukuru.
Bishop alishusha pumzi kwa nguvu akiwa na uhakika kabisa nili ingiza mwanamke kwenye nyumba yake. Kwa mda huo hakutaka kuuliza chochote, alifungua geti mwenyewe akatoka na
gari lake.
Alipofika mbele kidogo alipaki gari pembeni akatoa simu mfukoni na kuanza kuangalia video zote za kwenye kamera za jana usiku.
Kama mnakumbuka niliwaambia pale getini kuna kamera zaidi ya tano kwaiyo hata kama niliingiza mwanamke kwa siri lazima kamera zingenishika tu.
Ivyo ndivyo Bishop alivyodhani akiangalia video zote kwa umakini. Lakini haikusaidia kitu maana hakuna kitu cha tofauti chochote alicho kiona. Ndipo hapo wasiwasi wa kua mimi ni mwanamke ukamzidia.
Unajua nini kitatokea baada ya hapo?
Nakuja...........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi