*NIMEKOMA MIMI π* *Chapter 16&17* Ile siku jioni akili yangu yote ilikuwa kwa Bishop
Nilikuwa nakumbuka siku ya kwanza nilivyomuona, vile alivyonishika kule chumbani kwake, kila kitu kilikuwa kinanichanganya. Nilijisikia vizuri sana, mpaka nikaanza kutamani. tena anishike vile alivyonishika.
Nilikaa muda mrefu sana kabla sijapata usingizi, ilikuwa ngumu kulala kabisa. Saa tisa usiku, Bishop, Tobias na wale wanaume wengine waliondoka kama kawaida yao.
Kila siku wanaondoka usiku wa manane, wanarudi asubuhi, halafu mchana wanalala. Nilijiuliza sana, kazi gani hii wanayoifanya usiku kila siku? Ila sikuthubutu kuuliza maana nilijua hata nikijaribu kuuliza hawataniambia. Nilichojua ni kwamba wanafanya kazi haramu, basi
Basi Walipoondoka, niliweza kulala kidogo. Nilipoamka kulikua kumekucha kabisa na bado hawakua wamerejea. Nikaamua na kutoka nje ili kupunga hewa safi.
Nilipokuwa nje nikasikia mtu anagonga geti. Mda huo Mlinzi alikuwa ndani anafanya usafi Ivyo nikajisemea acha nifungue mwenyewe.
Si nikafungua bhana! Heeee eti Michael
amesimama palel Sikutarajia kumuona tena
hata kwa bahati mbaya. "Michael, unafanya nini hapa??? si salama, lazima uondoke sasa hivi nilihofia Bishop akimkuta pale anaweza kumdhuru
LakΔ±nΔ± hakutaka kuondoka Kwa hiyo umeamua kuniacha? Mimi kabisa??"
"Kwani si wewe uliyenicheat, unategemea nifanye nini sasa?"
"Kwa hiyo ukicheat kidogo tu hunisamei? Ulisema unanipenda daima, mbona unaonekana kama umesha nisahau?"
Nilimcheka nikasema "Michael, chochote tulichokuwa nacho kimeisha. Ulinidanganya, ukaniumiza! Ulitaka nifanyaje zaidi ya kuendelea na maisha yangu
"No, huwezi kuendelea na maisha, nani atanijali mimi? Mama yangu ni mgonjwa, nahitaji pesa, na wewe ni mpenzi wangu, ni lazima unisaidie"
Nikamuuliza "vipi yule demu uliyelala siku ile? Kwani huwezi kumuomba yeye pesa? Au nda kachacha
Michael akajaa hasira akanishika mkono "Sasa unajisikia kwa sababu unafanya kazi hapa? Kwa sababu wanakulipa vizuri? Umenisahau mapema hivi?
"Michael, tafadhali toka, tena Toka sasa hivi maana Sina cha kukuelezea"
"Siondoki! Mimi na wewe Hatujaachana mpaka. mimi nikuambie tumeachana. Kwa sasa bado wewe ni wangu, na ninahitaji pesa"
Nilishindwa kuamini huyu ndiye mwanaume
niliyempenda hadi nikajifanya mwanaume kwa ajili yake! Mtu ambaye hana hata chembe ya shukranit
"By the way, nani alikuambia niko hapa?" Nilimuuliza
"Lily amenielekeza
Nikamuambia "Sawa, ila Michael nisikilize vizuri, Nilikuwa nakupenda, hilo ni kweli. Lakini nilivyogundua ulinicheat, ulivyothibitisha kuwa
hukunipenda bali ulinitumia kwa pesa, pale pale nilikutoa moyoni. Mimi Sikupendi tena kijana!..... Kama mama yako ni mgonjwa, pole lakini nenda ukafanye kazi. Wewe ni mwanaume, fanya kazi, tafuta pesa, mshughulikie mama yako. Mimi sio
ATM ya kutoa hela jinsi unavyotaka. Sasa hivi najali maisha yangu na familia yangu. Tafadhali ondoka kabla mwenye nyumba hajarudi
Michael alikasirika, hakutegemea kabisa. nitamwambia maneno kama hayo Ghafla bila kutegemea akanipiga kofi kali sana, nikadondoka chini
Wakati ananipiga kofi, Bishop na wenzake ndo walikua wanarudi kwalyo Wakaona kabisa. alivyonipiga. Pale pale Gari likasimama, Bishop akashuka kwa hasira kali kama faru
Akamvuta Michael shati, akamnyanyua juu kama kisungura. Nilijua kabisa anaweza kumuua. Basi Michael akawa anapiga kelele "Usinigusel Unajua mimi ni nani?"
"Kwa nini umempiga? Hujui kama kumpiga mwanamke ni vibaya??"
Michael akajibu kwa dharau "Inakuhusu nini wewe? Huyu ni mpenzi wangu. Sina haja ya kuambiwa namna ya kumfunza adabu mpenzi
wangu
"So kumbe wewe ndo yule mpuuzi ambae hujui
nini maana ya upendo...... Bora umejileta mwenyewe" Bishop Akampiga Michael ngumi nne mfululizo, damu zikaanza kumtoka mdomoni na puani.
Kisha akamkamata tena huku akimwingiza ndani ya nyumba kwa nguvu. Kule alipokua. amenifungia siku ile??? Ennhee huko huko akampeleka Michael.
Baada ya Bishop kuingia ndani Tobias akaja akaniuliza "Uko sawa?"
"Niko sawa"
"Huyu alikuwa anafanya nini hapa?"
Nikajibu "Sijul, nilishangaa tu kumuona"
"Duuh! Sidhani kama Bishop atamsamehe, vile alivyoona akikuumiza imemkera sana. Nadhani atamdhuru
"Tufanyeje? Ongea nae amuache aende" "Hata nikiongea nae Hatanisikiliza labda wewe umfuate. Wewe tu ndiye anaweza kukusikiliza
Nikashangaa "Kwa nini mimi?"
"Huani tu vile Bishop anabadilika akiwa karibu yako? Kama huamini nenda mfuate alafu uone" sikuelewa Tobias ana maanisha nini kusema Ivi lakini nilifuata ushauri wake.
Nikaamua kweli kumfuata Bishop. Nikamkuta. yuko chumbani, bado amejawa hasira. Niliingia nikasimama pembeni nikichezea vidole vyangu kwa uoga.
"Tafadhali unaweza kumuacha aende? Anadal mama yake ni mgonjwa
Aliposikia Vile aliniangalia nikahisi kama. anataka kunirarua na yale macho yake. "Kwaiyo Unataka nimuachie ex wako?!"
"Tafadhali, mwache tu aende. Tayari umempiga na amejifunza. Kwani ni lazima umfungie kule nyuma?
"Muache akae huko! Angefikiria kwanza kabla hajakupiga mbele yangu
"Lakini na wewe si umempiga pia??"
"Ndio ila bado sijaridhika. Nataka kumfundisha jinsi ya kumheshimu mwananke!"
Akazidi kunishangaza jinsi ambavyo alikua akijibu. Nikamuuliza "Kwani maisha yangu binafsi yanakuhusu nini?"
Akatabasamu na kusogea karibu sana na mimi
akinishika kiuno bila uoga. "Kwa sababu ninazidi kuchanganyikiwa. Nimepoteza akili kwa sababu yako. Kila siku nakuwaza kichwani. Tangu siku ile ya swimming pool,lipsi zangu ziguse zako akili yangu,
haijapona. Na sasa ivi nimegundua wewe ni mwanamke ndo nazidi kupagawa kabisa. Siwezi kuvumilia kukuona ukicheka na Tobias au mtu mwingine maana Naumia. Nataka ucheke kwa ajili yangu. Ukiwa na shida, unitafute mimi. Nataka unipe muda wako, lakini hunipi. Hilo linauma. Je, ni kosa kuomba hivyo?"
Nilibaki nimesimama kama mshumaa, nikishangaa kama kweli ni Bishop huyo ndo kaongea maneno yalee ama naota! Na wala Sikujua nimjibu nini zaidi ya kuganda kama
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi