NIMEKOMA MIMI π* Chapter 13 Baada ya kugundua kuwa mimi ni mwanamke, alishuka kwenye gari
Wakati huo nilikuwa sijui hata kinachoendelea. Nikajibu "Una maanisha nini?"
Akarudia tena kwa hasira "Ni nani aliyekutuma?"
Nilikuwa nimechanganyikiwa hata sijagundua kama tayari anajua ukweli wote. Alipoona nasua sua kujibu akatoa bastola akaninyooshea mfukoni
Weeeh nusu nikojoe wapendwa ndo nikagundua mambo yameharibika. Nlitetemeka mpaka figo huku machozi yakianza kunitoka.
"Hakuna aliyenituma hakuna!"
"Hii ni mara ya mwisho nakuliza! Ni nani aliyekutuma?"
Namna alivyonielekezea bunduki, nilijua kabisa hatanii. Pale pale Nikapiga magoti nikaanza kumuomba sana, nikimwambia hakuna mtu aliyenituma lakini hakuni amini kabisa. Na ili kunitisha, Akainua bastola juu akapiga risasi mbili hewani Pahl Pahl Kisha akanielekezea tena. This time akiwa tayari kufyatua ubongo. wangu
"Sema alie kutuma, 12. 3. 4."
Nikasema huku nikilia "Hakuna mtu aliyerituma, nimekuja hapa kutafuta kazi tu. Tafadhali nisamehel
Lakini bado hakuamini, Macho yake yalionesha kabisa yuko serious na amechoka na majibu yangu. Sikua nala kufanya zaidi nilifumba macho taratibu, machozi yakinitoka nikisubiria kufa.
Nikaanza kukumbuka familia yangu ambayo siku ihudumia vizuri sababu muda wote nilikua namfikiria tu Michael, Nikajuta sana, nikaona kabisa ndo naenda zangu akhera Ivoo
Bahati nzuri zile risasi mbili alizopiga hewani zilisikika na akina Tobias. Chap wakaja nje wakiwa wamejikoki maana walizani wamevamiwa. Lakini wakashangaa nimewekwa. mtu kati, na pistol nimenyooshewa
Tobias akajua kabisa hapa mambo yameshaharibika. Akanitazama kwa yale macho ya kusema "Nilikwambia". Akaji fanya kama hajui vile
"Boss Kuna nini?"
"Huyu ni spy katumwa aje kunipeleleza.......! Unajua kama ni mwanamke?"
Wengine waliposikia vile walishangaa wakabaki
mdomo wazi wasiamini. Tobias pekee ndo hakuonyesha kushangaa "Mimi sijui chochote. Sasa unataka kufanya nini naye?"
Bishop akasema kwa hasira "Nitamuua"
"Usimuel Ukimuua hutajua aliyemtuma. Acha aishi kidogo, utapata ukweli
Bishop akamtazama Tobias akimuuliza, "Unajaribu kumtetea?"
"Hapana simtetel, ila ukweli ndo huo. Ukimuua. sasa, hutajua ni nani yuko nyuma yake"
Bishop akanyamaza kwa dakika moja, akifikiria. Baadaye akashusha bunduki yake akaichomeka nyuma ya jeans.
Bila kuongea chochote Akanivuta kwa nguvu akinipeleka nyuma ya nyumba. Kumbe kule nyuma kulikuwa na chumba kidogo kama gereza na mimi sikuwahi kujua maana Mara nyingi nilikuwa jikoni au chumbani tu.
Basi mtoto wa Banza nikafungiwa huku nikiambiwa sitakula, kunywa tena kila siku nitakula mateso mpaka niseme aliyenituma ni nani. Sasa nimtaje nani jamani wakati hata sikua. nimetumwa na yeyote
Yanu ilikuwa siku mbaya sana kwang, Asubuhi niligundua labubu wangu ananicheat alafu jioni siri yangu imevuja nikaishiwa kufungwa
Vipenzi, Nililala njaa usiku mzima hata mma sikupewa. Na icho kigereza kichafu, kuna baridi kali & mbu kibao. Mbaya zaidi Nilikuwa kwenye siku zangu na sikua na chochote cha kujisitiri. Aisee Nililia sana usiku kucha kama mwehu..
Asubuhi Bishop akarudi, safari hii akiwa nΠ° sanduku mkononi. Alinitoa kwenye kile kigerezani, akanikalisha kwenye kiti, akifungal mikono yangu na miguu kwa kamba. Kisha Akafungua lile sanduku sasa, mwenyewe. analiita sanduku la kazi
Ndani kulikuwa na vifaa special kwaajili ya mateso. Nilivyoviona tu mwili wote ukasisimka. nikasema leo nafwa huku najiona
Na jinsi Bishop ambavyo hakutaka mchezo, akatoa spana moja kubwaa akanionyesha. "Nitakung'oa jino moja hadi lingine. Usijali nitafanya polepole ata usiwe na presha. We unachotakiwa kufanya ni kuniambia jina la alie kutuma uje kunichunguza kwenye nyumba. yangu
Nikamuuliza "Nikikwambia ukweli utaniacha niondoke?"
"Ndio, nitakuacha uishi"
Nikacheka kidogo "iyo si kweli. Utaniua hata baada ya kujua ukweli. Lakini nisikilize... nimechoka. Kichwa kimejaa mawazo chungu nzima. Asubuhi niligundua boyfriend wangu. amenicheat. Nilifanya kila kitu kwa ajili ya yule. mpuuzi. Nilikuja hapa kufanyia kazi ngumu kama mwanaume, eti nimnunulie iPhone 17, viatu, nguo, kila kitu. Nilihatarisha maisha yangu kwa ajili yake. Lakini kumbe amenidanganya.
Nilipaswa nitumie pesa zangu kwa wazazi wangu kijijini ili wale vizuri, walale vizuri. Lakini nilimchagua yeye badala ya familia yangu, na mwisho wa siku kanidanganya. Kwa hiyo ukiniuliza nani alinituma, naweza kusema ni boyfriend wangu. Nilikuja hapa kufanya kazi kwa ajili yake. Na kama unataka kuniuwa, niue tu. Nimechoka... Sitaki kuishi tena. Badala ya
kunitesa, nipige risasi sasa hivi. Niuel
Nilisema hayo machozi yakitiririka maana kweli nilishachoka. Basi Bishop alinitazama kwa muda akiwa amechanganyikiwa. Hicho hakikua alicho tarajia kuwa ningekisema. Aliweka vifaa vyake. pembeni Akaondoka bila kusema kitu.
Alirudi ndani Akamulta Tobias pembeni,
akamuuliza, "Unajua kitu chochote kuhusu huyo msichana?"
Tobias akadanganya "Hapana, sijui chochote"
"Nataka uniletee taarifa zote kuhusu yeye. Chunguza hadi anapoishi uniletee habari zote. Nakupa masaa mawili tu
Tobias "Sawa Boss" kisha akaondoka.
Na hapo ndipo mambo yalipoanza kubadilika kabisa... mnajua kwanini?
Nakuja...
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi