*NIMEKOMA MIMI π* Chapter 9 Kesho yake asubuhi niliamka mapema sana, maana ndo siku ya pati. Bishop
Basi niliamka mapena na kitu cha kwanza nilichofanya ni kumpigia Michael. Nilim-miss vibaya mno nikahitaji angalau nisikie sauti yake, lakini hakupokea simu. Sikuweza kuelewa ni kwanini hakupokea ila siku mind sana.
So niliweka tu simu pembeni na kuanza kazi.
Nlifagia eneo lote la nje, nikaandaa chai ya asubui kwa vidume vyote vile, alafu nikasafisha na ndani pia. Hadi namaliza kusafisha, watu wa decoration walikuwa washafika na kuanza. kupamba. Mda sio mrefu nao watu wa maakuli wakatia timu.
Baba la Baba Bishop alivaa suti nyeusi akawaka hatari! Alafu sio yeye pekee yake mpaka vijana wake walikua ndani ya black suit. Na dressing code ya ile sherehe ilikua ni nyeusi. Kwa haraka haraka utadhani walikua wana hudhuria kwenye mazishi kumbe ni party.
Mda sio mrefu na mimi nikapewa yangu, Tobias aliniletea akaniambia "vaa hii ili uonekane smart
"Ok asante" nikaipokea na kwenda kubadilisha. Ilinikaa vizuri na sijui hata vipimo vyangu walivijuaje.
Kwa juu nikavaa na kofia yangu kama kawaida.. Huwa nilikua Navaa kofia kila siku ili kuficha nywele zangu.
Basi bhana Wageni wakaanza kuingia. Ila cha
kushangaza wote walikuwa wanaume, palikua hakuna hata mwanamke mmoja mjue jinsi gani Bishop hakutaka mazoea na watoto wa kike. Sijui walimkosea nini jamani.
Kubwa kuliko walikuja na magari ya kifahari, yani ukiwatazama tu utajua ni watu wenye hela ndefu. Ila tu biashara zao sΕo za halali
Haya, Wakaanza kupata vinywaji, kusalimiana na wenzao kisha baada ya mazungumzo. wakahamia kwenye makulaji. Mimi Kazi yangu ilikuwa kuhakikisha kila mtu ana kinywaji na chakula mezani.
Nilichoka sana siku iyo maana tulikuwa
wahudumu watatu tu. Yani mimi na wengine wawili, alafu Wageni walikuwa wengi sana, so Ilikuwa ngumu kuwahudumia wote kwa wakati
Nakumbuka kulikuwa na jamaa mmoja alitaka champagne. Nikaenda kumletea, lakini kabla sijarudi nikaitwa na mwingine alikua anataka. wine. So nikampelekea huyu wa wine kwanza then yule wa champagne akawa wa mwisho.
Ile nampa champagne yake tu nikashtukia napewa kofi la uso, sijakaa sawa jamaa anaanza kunifokea kama mtoto mdogo. "Unajua nimekaa muda gani nikisubiri kinywaji??"
Nikasema kwa upole "samahani"
"What? Samahani??? Samahanii?!" ghafla akanisukuma nusu nidondoke bahati nzuri nilikua nina balansi ivyo sikudondoka.
Kuona vile hakutosheka mpuuzi yule akarudia
tena kunisukuma kwa nguvu na safari hil nikateleza nikaangukia kwenye swimming pool
Ile pati ilikuwa inafanyika nyuma ya nyumba ambapo kulikua na swimming pool. Na mjue ya kwamba mimi siwezi kuogelea kabisa, so nikaanza kutapatapa nikiomba msaada
Wa kwanza kuona ni Tobias! Chap alikimbia kuja upande wangu lakini alichelewa kwani Bishop aliruka wa kwanza kuja kunisaidia. Imagine Bishop karuka ndani ya maji kuniokoa! Alafu alikua chap maana alinidaka na kunivuta kunitoa pembeni ya swimming pool.
Lakini nilipodumbukia kwenye swimming pool kofia yangu nayo ikatoka, so nywele zangu zikaonekana sema uzuri nilikua nimezibana.
Sasa Bishop akaniangalia bila kunimaliza akajiuliza huyu ni mwanaume au mwanamke??? Mbona amekaa kama demu??? Kwakua nilikua nimebandika vile vindevu bandia, akajiaminisha kuwa mimi ni kidume. Bishop akapotezea, akaniweka chini akaanza kunipa huduma ya kwanza.
Aliweka mikono kwenye kifua changu akakibinya kwa nguvu ili nitapike maji. Lakini bado haikusaidia kitu, Akaona afanye njia nyingine. Haraka akashika pua yangu kisha akapuliza hewa mdomoni yani akafanya mouth to mouth . Lips zetu zikagusana bhana.
Saa ngapi jamaa asishtuke?? Ukweli lips zangu ni laini sana alafu ndogo kama za mtoto mdogo. Bishop akabaki ananitazama kama amechanganyikiwa flanii.
Bahati nzuri Tobias akasogea haraka, akamsukuma Bishop pembeni akasema "Acha niendelee mimi"
Kweli Bishop akasogea ndipo Tobias akanipa huduma ya kwanza kwa kubinya kifua changu hadi nikatema maji na kurudiwa na fahamu.
Tobias hakuchelewa, alinibeba moja kwa moja hadi chumbani kwangu, akaniweka kitandani. Akaniuliza, "Uko sawa?"
"Niko sawa"
"Unajua ilikuwa karibu Bishop ajue ukweli kuhusu wewe?"
Nikasema "sikutarajia"
Akanijibu kwa hasira kidogo "Nilikwambia uwe makini, sasa angalia! Bishop ameshaanza kuwa na mashaka, hasa kuhusu nywele zako"
Ndipo nikakumbuka "Mungu wangul Kofia yangu nimeiacha kwenye swimming pool!"
"Kwa sasa Usijali, Kwanza badilisha nguo alafu usitoke nje kabisa. Kaa hapa ndani
"Sawa"
Ndipo Tobias akatoka Nikabaki peke yangu. Nilikuwa natetemeka vibaya mno coz Nilihisi kabisa Bishop lazima atakuwa na mashaka.
Nikabadilisha nguo, na kuvaa nyingine kavu nikiwa najua kabisa mambo sasa yameharibika....
Je nini kitaendelea?
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi