Nikamwambia tena "Sijalia ni kitu tu kiliingia machoni
"Sawa basi. Ila Bishop anakuita. Sijui umezua nini tena leo ila be careful! Yupo chumbani kwake"
Nikasema "Sawa" nikaelekea huko.
Nilipofika Nikagonga mlango, akaniruhusu niingie. Bishop alikuwa anachezea laptop yake lakini macho yake yakiwa yakiniangalia! Na yeye akauliza
"Uko sawa?"
Nikajibu "Niko poa"
"Hauonekani uko sawal Alafu vidume hatuliagi!"Mara tu aliposema vile, akasimama akasogea karibu.
"ni mambo tu ya nyumbani hayako sawa"
Bishop Akanitazama na uso wa huruma kidogo "Okay! najua cha kufanya. Nifuate!" Akachukua funguo zake za gari akatoka nje nami nikamfuata bila kuuliza.
Tulipanda kwenye gari tukatoka. Sasa Wale wengine kina Tobias walibaki wakishangaa maana Bishop hajawahi kumtoa mtu yeyote kwa gari lake. Mimi ndiyo wa kwanza.
Sasa Bishop alinipeleka beach akaniambia kwakua sikua sawa alinipeleka kule ili nipumzike kidogo.
Nikamuuliza "Kwa nini?"
Akasema "Kwa sababu wewe pekee hujaonyesha kuniogopa! So sio vibaya kukusaidia!"
"Sawa"
"Ungependa kuniambia kinachokusumbua?"
Akaniuliza
"Hapana, sitaki kuzungumzia"
"Ok"
Tukanyamaza wote, Nikawa naangalia mawimbi na upepo wa bahari nikahisi roho imetulia. Tukakaa kimya zaidi ya masaa mawili, hakuna mtu aliezungumza. Hamuwezi amini Nilihisi poa sana, hasira zote na maumivu yote ya Michael yakaanza kunitoka.
Nilijua kwamba Michael hakuwa mtu sahihi kwangu japo nilijua kwa kuchelewa na kwa kupitia maumivu yasiyo na maana. Pia ule ukimya wa pale beach ilinisaidia kweli kufikiria vizuri.
Baadaye, Bishop akanipeleka kula hotelini. Tukaagiza chakula, tukala tumiwa kimya. Hakusema hata neno, nami sikusema kitu. Nilipenda ule utulivu kuliko kuongea, kwa sababu akili yangu ilikuwa imechoka
Nilidhani Bishop alinitoa out ili kunichangamsha kama alivyo sema ila kumbe sio! Ule ulikua ni mtego. Tangu Bishop ahisi mimi niwa kike hakua na amani kabisa.
Alikua anatafuta njia apate kuwa karibu na mimi ili aweze kunichunguza. Sasa nafasi ilipo jitokeza yeye akaitumia vizuri. Lakini kwa bahati mbaya hakugundua chochote. Maana mbali ya kuumizwa na mapenzi sikuonyesha tofauti yeyote kama mimi kweli ni mwanamke.
Kwalyo mpaka hapo Bishop akawa amefeli mpango wake na alikua na hasira kweli. Basi Baada ya kula, tukarudi nyumbani. Mimi ndiyo nilishuka wa kwanza kwenye gari.
So kutokana na stress na uchovu, mwili wangu si ukajipa bhana! Nikajikuta nimeanza siku zangu bila hata kujua na zilianza mapema kabla ya tarehe yangu.
Sikuwa nimegundua kabisa lakini Bishop aliona. Kidoa kidogo tu kwenye suruali yangu, akajua kabisa niko kwenye period. Na hapo ndipo alithibitisha kitu ambacho alikuwa na wasiwasi nacho tangu zamani, kwamba mimi ni msichana.
Alivyogundua uso wake ukabadilika. Akakasirika ghafla huku Moyo wake ukampiga kasi. Wazo la kwanza lililo kuwa kichwani kwake ni kwamba mimi ni mpelelezi nimetumwa nyumbani kwake kumchunguza, kumrekodi, kumweka matatizoni.
Na hapo ndipo mambo yaligeuka kabisa. Unajua nini alichonifanyia baada ya hapo? Ngoja nikuambie.....au nakuja........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
MIMI SIKUACHIπ₯° 24 MPAKA 25 ( MWISHO WA SEASON 1)
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 24 Basi bwana nakumbuka nilikaaa uku nyumbani week.2...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 21 Basi mie nikaendelea na vipindi na jioni sana ndo...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 19 Daah nikasema.mwanangu iyo chupi.nimemnunulia fat...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 16 Basi nikapata kaumarufu kweli kweli pale chooni. ...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 14 Aseee mi nilimuangalia sana uyu demu. Nikamuona j...
7 MPAKA 9 π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Basi bwana tukivyotoka kula sasa. Mi nikaludi ndani i...
Sehemu ya : 1 π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦ Mapenzi jamani ni kitu cha ajabuπ€¦ββοΈ, ni bahati sana kwa mtu kumpata kirahisi yule aliepan...