Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya β Gonga94 Semajambo
Gonga94 Β· Stories
14 Nov 2025
494 views
VYOTE NDANI GONGA94
*NIMEKOMA MIMI π* Chapter 14 Kwa sababu Tobias alijua mimi na Lily
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
tuna ukaribu Ivyo haikumchukua muda kupata taarifa zangu zote. Alichokifanya ni kumpigia simu Lily na kumueleza kila kitu kilichonitokea.
Lily alishtuka sana maana Baada ya mimi kumtumia ule ujumbe kuhusu Michael, alijaribu kunipigia mara nyingi sana lakini simu yangu ilikuwa imezimwa. Asijue kuwa mda huo shoga ake nipo kwenye hatari ya kung'olewa jino kwa spana
Basi Lily akamueleza kila kitu, jinsi nilivyokuja Dar es Salaam, nilivyoanza kufanya kazi, jinsi nilivyokutana na Michael, na vile nilivyokuwa nafanya kila kitu kwa ajili ya Michael! Hadi kufika stage ya kufanya kazi ya mlinzi kama mwanaume kwa ajili yake.
Mnajua mpaka Tobias hakuamini kama mtu anaweza kufanya jambo kubwa namna hiyo kwa sababu ya mapenzi. Aliona ni upuuzi lakini hakutaka kusema chochote.
Baada ya kukusanya taarifa za kutosha toka kwa Lily, Tobias alirudi kwa Bishop kumueleza kila kitu alichoambiwa. Akamsimulia alivyosimuliwa na mwisho akamuuliza kama
"sasa utamfanya nini huyu msichana?"
Bishop akajibu "Kama ni ivyo sitamuua wala kumuumiza lakini sitamwachia aondoke"
"Kwanini? Kama hana nia mbaya, kwa nini usimuachie tu?"
"Kwa sababu tayari anajua mengi kuhusu hii nyumba. Anajua tunachofanya hapa ndani. Nikimuachia polisi wanaweza kumtumia ili awaambie kila kitu. Hata kama hakuwa na nia mbaya, siwezi kumuamini tena. Atabaki hapa mpaka mimi mwenyewe niamue cha kumfanya"
"Sawa, basi tufanye nini sasa?"
Bishop akamjibu "Nenda umtoe kwenye selo. Na pia Hatakaa tena getini nina wasiwasi atakimbia, Mpe chumba cha karibu na changu. Nataka niendelee kumchunguza zaidi maana bado simwamini"
"Sawa" Tobias akakubaliana nae
Wakati huo mimi nilikuwa nimechoka kupita maelezo. Machozi yalikua hayatoki tena, nilikaa tu kama zombie Mda sio mrefu Tobias aliingia na kuanza kunifungua kamba za mikono na miguu.
"Mbona unanifungua?" Nilimuuliza
"Bishop kasema nikuachie uende ukaoge,
ubadilishe nguo, upumzike"
"Kwanini sasa? Jana tu alitaka kuniua!"
"Kwa sababu jana alifikiri wewe ni npelelezi. Ila now amejua ukweli, ndiyo maana anakuruhusu utoke"
Nikamuuliza "Inamaanisha naweza kurudi nyumbani?"
"Hapana, Unabaki hapa ila tu kutoka nje ya hii nyumba ndo huruhusiwi"
"Unaweza kupumzika tu hapa. Alafu Sasa ivi tayari unajua mambo mengi kuhusu sisi unadhani Bishop anaweza kukuacha uondoke kirahisi?? Anaogopa polisi wanaweza kukutumia dhidi yake. Kwa hiyo kasema njia salama ni wewe kubaki hapa"
Nikasema "Sawa kwa sababu nilijua hata nikibembeleza Bishop hataniachia. Nilikubali tu.
Baada ya kunitoa kule Tobias akanisindikiza hadi kwenye chumba cha wageni kilicho kua karibu na chumba cha Bishop. Nikaambiwa nikaoge na nikapumzike, pia Nilikuwa nanuka kwa sababu nilikuwa kwenye siku zangu na sikuwa nimevaa chochote.
Basi Nikaingia bafuni moja kwa moja nikaoga. Nilipomaliza, nikakuta nguo zangu zote zimeshaletwa kule chumbani ivyo nikavaa. Ila sikuwa na pads kwa hiyo nikaanza kufikiria kwenda kumtafuta Tobias ili anisaidie.
Lakini kabla sijatoka, mlango ukafunguliwa ghafla bila hata kugongwa. Alikua Bishop kabeba mfuko mweupe mdogo. Akanipatia ule mfuko, nikautazama, ndani kulikuwa na pads. Nikasema "Asante"
lakini hakunijibu. Alikuwa ananitazama tu.
Kwakua sasa wote walijua mimi ni mwanamke, sikuona haja ya kuendelea kujificha. Niliachia nywele zangu na nikavaa gauni langu ambalo nilikua nalo toka mwanzo. Sio siri mimi ni karembo sana sema ndo ivyo sijajizingatia.
Saa ngapi Bishop asianze kuniangalia kuanzia juu hadi chini. Namna alivyonitazama ilionyesha kabisa ananitamani maana Daah! Jicho Alipogundua ananiangalia kupita kiasi, akageuka lilimlegea sio kitoto. Yeye mwenyewe haraka akaondoka kimya bila kusema kitu.
Embu kwanza.....nakuja..........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
MIMI SIKUACHIπ₯° 24 MPAKA 25 ( MWISHO WA SEASON 1)
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 24 Basi bwana nakumbuka nilikaaa uku nyumbani week.2...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 21 Basi mie nikaendelea na vipindi na jioni sana ndo...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 19 Daah nikasema.mwanangu iyo chupi.nimemnunulia fat...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 16 Basi nikapata kaumarufu kweli kweli pale chooni. ...
π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Sehemu ya 14 Aseee mi nilimuangalia sana uyu demu. Nikamuona j...
7 MPAKA 9 π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Basi bwana tukivyotoka kula sasa. Mi nikaludi ndani i...
Sehemu ya : 1 π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦π¦ Mapenzi jamani ni kitu cha ajabuπ€¦ββοΈ, ni bahati sana kwa mtu kumpata kirahisi yule aliepan...
*NIMEKOMA MIMI π* Chapter 14 Kwa sababu Tobias alijua mimi na Lily
tuna ukaribu Ivyo haikumchukua muda kupata taarifa zangu zote. Alichokifanya ni kumpigia simu Lily na kumueleza kila kitu kilichonitokea.
Lily alishtuka sana maana Baada ya mimi kumtumia ule ujumbe kuhusu Michael, alijaribu kunipigia mara nyingi sana lakini simu yangu ilikuwa imezimwa. Asijue kuwa mda huo shoga ake nipo kwenye hatari ya kung'olewa jino kwa spana
Basi Lily akamueleza kila kitu, jinsi nilivyokuja Dar es Salaam, nilivyoanza kufanya kazi, jinsi nilivyokutana na Michael, na vile nilivyokuwa nafanya kila kitu kwa ajili ya Michael! Hadi kufika stage ya kufanya kazi ya mlinzi kama mwanaume kwa ajili yake.
Mnajua mpaka Tobias hakuamini kama mtu anaweza...
π Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/nimekoma-mimi-chapter-14-kwa-sababu-tobias-alijua-mimi-na-lily