*NIMEKOMA MIMI π* Chapter 7 Basi nikaanza kupika fasta ili nimalize mapema, lakini kusonga ugali wa watu kumi sio mchezo
Ila nilijitahidi ivo ivo nikamaliza kwa muda. Baada ya kumaliza kupika, kilichobaki ni kupakua chakula. Nikatafuta sahani kabatini, nikakutana na sahani tatu tu na bakuli moja. Alafu upande wa pili wa kabati Nilikutana na masinia makubwa matatu. Nilipoyaona sikuyajali sana, nikaendelea kutafuta sahani nyingine.
Wakati nipo kwenye harakati za kutafuta Dennis akaingia jikoni "Bado hujamaliza kupika? Tumengoja sana, tunanjaa balaa
"Nimemaliza kupika, kinachobaki ni kupakua tu"
Akanijibu "sasa unasubiri nini?"
"Sioni sahani nyingine, kwani Mnatumia nini kula?"
Dennis akatabasamu kidogo "Hujaona yale masinia pale kabatini?"
"Nimeyaona"
"Basi tumia hayo, Sisi wote tunakula kwenye masinia kasoro Boss Bishop"
Nilishtuka maana Nilidhani kila mtu anakula kwenye sahani yake, kumbe si hivyo. Haya Nikaandaa chakula kwenye masinia mawili, moja likiwa na ugali mkubwa, lingine likiwa na mchuzi na nyama.
Unakumbuka niliwaambia pale dining kulikuwa kumetandikwa jamvi?...enheee Basi sasa wale majamaa wanakaa chini kula pamoja kwenye. sinia
Kila siku wanakula hivyohivyo. Ndio maana sikupata sahani nyingi kumbe ni masinia. wanatumia
Nikawa nawashangaa vile walivyokua wanakula, apo kila mtu kavua t-shirt, wapo tumbo wazi
wanafinya ugali kama hawana akili nzuri Dennis akaniangalia akasema "Unangoja nini sasa? Njoo ule"
Nilikuwa nina njaa pia na chakula chote kilikuwa
kimeisha jikoni, Nikaona nikae tu nile nao lasivyo nitashinda njaa. Ila bwana kula na vidume sio rahisi. Ni walikuwa wanakula kwa spidi alafu sasa
hawajali hata kama chakula nicha motol
Hamuwezi amini niliishia kula matonge mawili tu na kipande kimoja cha nyama. Maana kufunga na kufungua masinia yapo empty, watu ni wanajipepea na t-shirt zao
Baada ya kula nikachukua yale masinia nikayaosha yote kisha nikasafisha pale tulipo lia chakula. Sema wali enjoy sana msosi wangu coz hawakuacha kunisifia
Kama kuna Mmoja alisema "We jamaa unapika vizuri kama demul Umetoa sotojo kali kweli! Ni kula kujilamba"
Mimi nikacheka kidogo tu nikasema "Asante" alafu nikaondoka haraka sababu sikutaka mazoea nao ill wasije kunishtukia..
Kuna mda Tobias aliniita, nyuma ya jiko nahisi hakutaka maongezi yetu watu wayasikie. Mkononi Alikuwa ameshikilia karatasi.
tangu umefika hapa, "nimekuangalia nimegundua kitu"
Nikauliza "Kitu gani?"
"Najua wewe ni mwanamke. Nimeishi na mama pamoja na mdogo wangu wa kike so najua. tofauti ya mwanaume na mwanamke. Huwezi kunificha"
Nilishtuka nusu ya kuzimia. Yani siku hiyo hiyo nilisha qundulika mapema kiasi iko?? Chap Nikaanza kumuomba "please usinifukuze, maisha yangu yanategemea hii kazi
"Ivi wewe huogopi? Unadhani Bishop akijua
wewe ni mwanamke atafanya nini? Hii ni hatari sana. Tena ushukuru kwamba mimi ndio nimegundua wa kwanza maana kama Bishop mwenyewe angejua basi mda huu ungekua upo
kaburinil... Inabidi uondoke, Usiku tukitoka na wewe uchukue vitu vyako uondoke kimya kimya. Nikirudi nataka usiwe hapa
Nikajibu kwa huzuni "Sawa" lakini moyoni sikuwa tayari kuondoka. Ni siku yangu ya kwanza kazini, mshahara ni mkubwa nisingependa pia kumpoteza Michael.
na
Basi Jioni ilipofika Bishop, Tobias, na wale vijana wote wakaondoka, Sikujua wameenda wapi na kusema kweli sikuwa najali. Kitu pekee nilichokuwa nafikiria ni namna ya kubakia pale
tu.
Badala ya kuondoka kama alivyonielekeza Tobias, mimi nikabaki pale kimya nikingoja arudi niendelee kumuomba. Mda huo Lily nae akapiga simu utadhani alinusa kuwa nipo matatizoni.
Nilipo pokea akasema, "we shege Mbona hukunipigia kunambia kilicho jiri huko?"
" Usijali, mambo ni sawa, ila kuna tatizo
"Tatizo gani tena? Hata siku moja hujamaliza tayari unaanza matatizo?"
"Si Ivyo, Tobias amenigundua mimi ni mwanamke
Lily Alishtuka "Umesema nini??"
"Ndiyo, amegundua na amenambia niondoke haraka sana"
"Basi ondoka! Unangoja nini huko?"
"Siwezi kuondoka, hii kazi ndio maisha yangu. Nikiondoka nitapata wapi tena kazi?? Michael si ataniacha mazima kisa nimeshindwa kumhudumia?...hapana! nitajaribu kuongea na Tobias akirudi
Lily akasema, "Mungu wangu, wewe unapenda matatizo! Bishop ni hatari sana, please rudi nyumbani kabla hajakudhuru"
"Usijall, nitarudi lakini si sasa Nikakata simu, nikajilaza kitandani nikijipa moyo kwamba kila kitu kitakwenda kuwa sawa.
Ilipofika saa nane usiku nikasikia honi getini, Nikaruka fasta nikaenda kufungua. Bishop na vijana wake walikuwa wamerudi. Walionekana wamechoka sana sijui ni kitu gani walitoka kufanya usiku ule wa manane.
Sasa Tobias aliponiona bado nipo pale alishtuka na kukasirika maana alinishaniambia niondoke. Sikujali macho yake, Nikafunga geti pale bila wasiwasi.
Wale vijana wakaingia ndani moja kwa moja kulala, ila Bishop akaniangalia na kusema "vijana wangu wamesema chakula chako ni kitamu sana. Nataka kuonja
"Sasa hivi?"
"Ndiyo! Unadhani ni saa ngapi?"
"Mhhh..... Ungependa nipike nini?"
Akanijibu "kile kile ulichopika mchana, ugali na nyama Kisha akaingia zake ndani
Bishop alipoingia tu ndani, Tobias akanigeukia "Unajua hii kitu ni hatari kiasi gani? Shege, Boss Bishop ni hatari
"Ninajua please niache nifanye kazi hapa! Nina shida ya kazi ndo maana nang'ang'ania kufanya. kazi hapa
Tobias akavuta pumzi kidogo "Sawa, nenda kaandae chakula cha Bishop then Kesho nitakupa jibu la maamuzi yangu
Nikatabasamu na kukimbilia jikoni, apo Ilikuwa saa nane usiku mjue. Na Bishop alitaka msosi
Unajua nini kitatokea baada ya hapo?
Nakuja
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi