*AFANDE NILEGEZEE KAMBA ππ«π«* *SEHEMU YA KUMI NA MOJA* Ile simu ya Siku ya kuripoti kituo cha polisi ikafika. Nilipaswa kwenda peke yangu, ila Elijah akaniambia atanipa kwa gari
Nilipofika nikaenda kuripoti kama kawaida, huko nikakutana na Afande Ruth. Mara ya mwisho hatukuonana, kwa hiyo tulizungumza sana tukipiga stori. Alifurahia kuniona nikiwa sawa.
Wakati mimi niko kwa Afande Ruth, Elijah aliamua kumtembelea Elton ofisini kwake. Ila Elton hakuwa na mood kabisa. Alikaa tu kimya, uso wake ulikuwa kama mtu mwenye mawazo mengi. Na ninajua kabisa alijisikia vibaya kwa sababu Elijah ndiye aliyenipeleka kituoni.
Elijah naye aligundua cousin wake hana furaha "Nimegundua hujafurahia kunilona, na tangu usikie nilimleta Gina, umekuwa mkali. Kama unampenda tu sema"
"Sina mapenzi naye Elton alikataa
"Sasa mbona unanikasirikia?"
"Just nimechoka hakuna cha zaidi"
"Wewe mwenyewe unajua Sijazoea kuona unaninyamazia hivi"
"Elijah, kama unavyoniona niko busy sana. Kama huna kitu cha maana cha kusema, tafadhali niache nifanye kazi
Elijah akainuka kwa hasira, akatoka ofisini.
Alipofika nje kituoni, akanikuta nimeshamaliza kuongea na Afande Ruth nipo namsubiri.
Nilimuona kabisa hakuwa sawa. Elijah ni mtu mtulivu, hawezi kukasirika kirahisi, kwa hiyo nilijua kuna kitu kibaya kimemkera.
"Elijah, nini mbaya? Mbona uso umebadilika?"
"Ni Elton, lakini usijali. Najua namna ya kudeal naye. Ameharibu mood yangu nzima. So Badala ya kurudi home, twende tukale ice cream kidogo ili tu-relax, sawa?"
"Sawa"
Tukapanda gari, Elijah akanipeleka sehemu nzuri sana ya ice cream. Nilifurahia mno, tulikula tukacheka. Baadaye akaamua twende mall.
Akanionyesha vitu vingi, akanifanyia shopping.
kidogo sababu sikutaka vitu vingi.
"Elijah, asante sana
"Usijali, chochote kwa ajili yako"
Baada ya hapo tuliamua kurudi home maana Ilikuwa jioni. Lakini tulipofika hatukutarajia kumkuta Elton nyumbani. Alikuwa amewahi kurudi, na japokuwa hakusema chochote, niliona
kabisa ndani yake amekasirika, Alijaribu kuficha, lakini macho yake yalionyesha ana wivu na hasira
Mimi nilichofanya tu ni kuingia store kama kawaida, nikawaacha yeye na Elijah sebuleni.
"Sasa uko sawa, tunaweza kuongea?"
"Nilionekana kama sikua sawa?" Elton akajibu.
"Bro, nilivyokuja ofisini ulikuwa tofauti. Hukuongea kabisa. Nilijua kuna shida"
"Tuachane na hayo! siku yako imekuwaje?" Elton aliuliza kimtego
"Siku yangu Imekuwa poa sana. Nilitembea sehemu tofauti, na nilikua na Gina
Elton akanyamaza sekunde chache kisha akasema, "Basi mara nyingine ukitaka kumtoa house girl wangu out, niombe ruhusa kwanza"
"Kwanini? Ni mtu mzima, sio mtoto"
"Kwanza kabisa, Gina ni mtuhumiwa. Ndio maana hatakiwi kuondoka Arusha hadi mwezi uishe. Unanielewa? Sasa vipi kama angekimbia? Ungetueleza nini polisi? Ndiyo maana sitaki umtoe bila ruhusa yangu
"Sawa nimekuelewa, ila haonekani kama anataka kukimbia. Alafu Hiyo ndio sababu pekee? Ama kuna nyingine?"
"Unadhani kuna sababu gani nyingine? Nimekwambia mara nyingi, sina hisia yoyote kwake. Nachojali ni kwamba mimi ndiye nimemtoa kituoni, mimi ndiye nitalipa deni lake. Kwa sasa niko responsible kwake hadi mwezi uishe. Hicho tu"
Baada ya kusema hivyo, Elton akachukua laptop yake akaenda chumbani. Elijah akabaki anatabasamu kimyakimya, maana alijua cousin wake tayari ameshafall, ila anajifanya mjanja kukataa.
Lakini ukweli ni kwamba Elton hakulala usiku. huo. Kila alipogeuka kitandani, mawazo yake yalikuwa juu yangu. Alikumbuka kila kitu, ile
mara ya kwanza tulivyofanya mapenzi kwenye gari, na ile mara ya pili ndani ya nyumba..
Yale matukio yalimvuruga kichwa. Na kila muda ulivyokuwa unasogea, kiburi chake kilianza kupungua polepole.
Basi aliposhindwa kulala kabisa, Elton akaamua anifuate. Akaamka, akatembea kimya hadi store. Akafungua mlango akanikuta nimejilaza tu bila. kufunga macho.
Nikamuuliza "Unahitaji kitu?"
"Hapana, nataka tu kujua kwanini ulitoka na
Elijah bila ruhusa yangu
Sikuwa na cha kumjibu. Wakati huo nilikuwa nimeshikwa na homa, mwili unatetemeka. Nilihisi kabisa nimechoka, labda kwa sababu ya kula kitu vya baridi.
Pia wiki kadhaa nilikuwa nalala sakafuni pamoja na kwenye vumbi. Nakumbuka mara kadhaa Elton alinimwagia maji baridi.
Elton hakuliona hilo mwanzoni, akaniuliza tena, "Mbona umenyamaza?"
"Sorry"
Akasogea karibu zaidi, akanitazama vizuri "Wewe uko sawa kweli?"
"Ndio, niko sawa
Nilikataa Lakini aliona kabisa nasema uongo.
Akaweka mkono juu ya kichwa changu kuangalia joto, akashangaa jinsi nilivyokuwa wabaridi. Hapo ndo akajua naumwa. Bila hata kufikiria mara mbili, alinibeba mikononi na kunipeleka chumbani kwake
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi